" Jamii iliyostaarabika ni yenye kuheshimu Mawazo & Mitazamo ya wengine. Mchango wako katika kazi yoyote ulenge kujenga jamii yenye Kujitambua, Kujithamini na Kujiwajibisha "

 
Wednesday, August 22, 2012


Na watajwe ili wakome kutufisidi na kutufilisi


Hawra Shamte

NAKUBALIANA kwa asilimia 100 na ushauri wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kwamba waliohusika na kuhamisha fedha nchini na kuzipeleka nje ya nchi kuzificha watajwe. Nami naungana naye kushangaa kwa nini hawatajwi?

Nashangaa kwa sababu hii si silika ya Watanzania kunyamazia uovu au kutishika kuusema uovu au kuogopa kuwaadhiri waovu.

Kwanini waovu hawatajwi? Kwanini tumekuwa tukitishia tu kuwataja watu ambao tunasema tunao ushahidi wa kutosha kuwa wanaifisidi nchi, wanahawilisha rasilimali za nchi.

Wanaohamisha fedha nchini na kuzipeleka kuzihifadhi katika benki za nje, hata kama ni fedha zao na tujaalie kuwa wamezipata kihalali, lakini kimsingi hawa ni wahujumu wa uchumi wa nchi.

Ikiwa uchumi wa taifa masikini kama Tanzania unategemea mzunguko wa dola ya Marekani, inakuwaje mtu mmoja anachukua mamilioni ya dola (anayodai kuwa ni yake) na kwenda kuyaweka katika benki ya Uswisi au kwengineko kokote kulikovunjwa shoka mpini ukabaki?

Anachofanya ni kukandamiza mzunguko wa fedha nchini kwake na kwenda kuimarisha mzunguko wa fedha wa nchi zilizoendelea.

Hii ni tabia ya uchoyo na ulafi, ikiwa mtu umepata inakuwaje hutaki na mwenzako apate? Huyu angeweka mabilioni yake ya fedha nchini, si yangetusaidia wengi kama yalivyotusaidia mabilioni ya Kikwete?

Kwa sababu kinachofanyika ni kuongeza uwezo wa benki wa kukopesha wateja wake, kwa kuwa benki inakuwa na wateja wakubwa wanaoingiza fedha nyingi zinazokaa kwa muda mrefu bila kazi.

Pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa sheria ya uhujumu uchumi, pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa kuulizwa wamepata wapi hivyo ‘vijisenti.’ Lakini kama wamezipata fedha hizo kwa njia halali kwanini waogope?

Nadhani umefika wakati Watanzania tukatae kugawana umasikini, kama baadhi yetu wanao utajiri walioupata kwa nguvu zao, kwanini waogope kujidhihirisha kama wao wana fedha na kisha fedha zao waziweke pahali panapotambulika kisheria.

Hawa akili zao na roho zao ni mbaya kuliko wale waliokuwa wakifukia magunia ya fedha chini ya ardhi wakati wa uhujumu uchumi. Wanaofanya hivi bila shaka ni wezi, wanaogopa kugundulika kama wana mabilioni ya fedha wasiyoweza kuyaelezea jinsi walivyoyapata.

Lakini hii tabia ya kuficha ukweli haikuanza leo, wala si wabunge tu wanaohofia kuuweka wazi ukweli, kwani hata viongozi wetu kadhaa serikalini katika kadhia tofauti tumeshawasikia wakisema kuwa wahalifu wanawafahamu lakini wanawapa muda wajirekebishe.

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema kuwa amepelekewa orodha ya wauza unga, lakini anawapa muda mpaka Krismasi, ikimalizika atawashughulikia...

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema anawajua waliojichukulia na kujihodhia fedha za Madeni ya Nje za Benki Kuu (EPA) lakini akawapa muda wazirejeshe...

Hii imekuwa ndiyo tabia, yamekuwa ndiyo mazoea, umekuwa ndio utamaduni mpya tulioamua kuufuata; utamaduni wa kuwahifadhi waovu, utamaduni wa kutowataja wezi, utamaduni wa kuwaonea haya wahalifu, utamaduni wa kuwapa muda wajirekebishe.

Wengine wamejifunza utamaduni wa kuwavumilia wanaowachafua, lakini hili la kutowataja wanaofisidi mali ya umma, wanaohawilisha rasilimali za taifa, hapa tumekithiri ada!

Wanahamisha nyara za taifa, wanasafirisha mpaka wanyama tunawavumilia, tunawaangalia tu. Wanachimba madini yetu, wanatuachia mashimo yasiyozibika, sisi tupo tunawaangalia tu, eti tunajivunia amani na utulivu.

Ni amani gani aliyonayo mtu anayeishi kwa mlo mmoja kwa siku? Ni amani gani anayoipata mtu anayetafuta maji kuanzia saa nane za usiku mpaka saa 6 mchana, anasubiri chemchem ifumuke, achote kwa kata, tena kwa utulivu ili asiyachafue? Haya ndiyo maji anayotarajia kwenda kunywa yeye na familia yake. Anafanya hivyo kwa sababu ahadi ya kupelekewa maji hadi kwenye kaya yake bado haijatekelezwa kwa sababu Serikali haina fedha, lakini Serikali hiyohiyo inawaangalia baadhi ya wananchi wake na hata wawekezaji iliyowaalika waje nchini kuwekeza, wakihamisha rasilimali za taifa.

Ni utulivu gani anaoupata mama mjamzito ambaye katika zama hizi zenye maradhi ya kuambukiza ya kila aina, anapokwenda hospitalini kujifungua anakuta wanalazwa watatu katika kitanda kimoja?

Ni utulivu gani anaokuwa nao mwanafunzi wetu wa shule ya msingi pale anapoketi sakafuni na kuandika kwenye daftari lake hali ya kuwa amepinda mgongo na kukunja miguu?

Kwa hali hii ya kutodhibiti mali ya umma, hali ya kuwaacha wachache wakifaidi keki ya taifa, hali ya kuwaacha walafi wakikomba mboga yote na kuwaacha watoto wetu wakiwa na utapiamlo; kiasi kiongozi wetu aseme Tanzania ina rasilimali nyingi, lakini hajui kwanini bado ni masikini.

Atajuaje? Wakati wanayoyafanya hayo wanafanya kwa kificho? Wakati wanahamisha mamilioni ya fedha kwenda kuyaficha nje ya nchi kama wezi? Wakati watu hawako wazi na wala si wa kweli?

Masikini Tanzania imegeuzwa shamba la bibi, tena bibi mwenyewe keshafariki, shamba halina msimamizi, wajukuu wanajichumia hata vilivyo vichanga, visivyopea wanavipepea kwa moto, wanahamisha badala ya kula wao au hata kuwaruhusu wenzao kujichumia na kukidhi njaa, hamu na kuondosha ghamu zao. Hii ni hatari!


0655 849694






Na watajwe ili wakome kutufisidi na kutufilisi


Hawra Shamte

NAKUBALIANA kwa asilimia 100 na ushauri wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kwamba waliohusika na kuhamisha fedha nchini na kuzipeleka nje ya nchi kuzificha watajwe. Nami naungana naye kushangaa kwa nini hawatajwi?

Nashangaa kwa sababu hii si silika ya Watanzania kunyamazia uovu au kutishika kuusema uovu au kuogopa kuwaadhiri waovu.

Kwanini waovu hawatajwi? Kwanini tumekuwa tukitishia tu kuwataja watu ambao tunasema tunao ushahidi wa kutosha kuwa wanaifisidi nchi, wanahawilisha rasilimali za nchi.

Wanaohamisha fedha nchini na kuzipeleka kuzihifadhi katika benki za nje, hata kama ni fedha zao na tujaalie kuwa wamezipata kihalali, lakini kimsingi hawa ni wahujumu wa uchumi wa nchi.

Ikiwa uchumi wa taifa masikini kama Tanzania unategemea mzunguko wa dola ya Marekani, inakuwaje mtu mmoja anachukua mamilioni ya dola (anayodai kuwa ni yake) na kwenda kuyaweka katika benki ya Uswisi au kwengineko kokote kulikovunjwa shoka mpini ukabaki?

Anachofanya ni kukandamiza mzunguko wa fedha nchini kwake na kwenda kuimarisha mzunguko wa fedha wa nchi zilizoendelea.

Hii ni tabia ya uchoyo na ulafi, ikiwa mtu umepata inakuwaje hutaki na mwenzako apate? Huyu angeweka mabilioni yake ya fedha nchini, si yangetusaidia wengi kama yalivyotusaidia mabilioni ya Kikwete?

Kwa sababu kinachofanyika ni kuongeza uwezo wa benki wa kukopesha wateja wake, kwa kuwa benki inakuwa na wateja wakubwa wanaoingiza fedha nyingi zinazokaa kwa muda mrefu bila kazi.

Pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa sheria ya uhujumu uchumi, pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa kuulizwa wamepata wapi hivyo ‘vijisenti.’ Lakini kama wamezipata fedha hizo kwa njia halali kwanini waogope?

Nadhani umefika wakati Watanzania tukatae kugawana umasikini, kama baadhi yetu wanao utajiri walioupata kwa nguvu zao, kwanini waogope kujidhihirisha kama wao wana fedha na kisha fedha zao waziweke pahali panapotambulika kisheria.

Hawa akili zao na roho zao ni mbaya kuliko wale waliokuwa wakifukia magunia ya fedha chini ya ardhi wakati wa uhujumu uchumi. Wanaofanya hivi bila shaka ni wezi, wanaogopa kugundulika kama wana mabilioni ya fedha wasiyoweza kuyaelezea jinsi walivyoyapata.

Lakini hii tabia ya kuficha ukweli haikuanza leo, wala si wabunge tu wanaohofia kuuweka wazi ukweli, kwani hata viongozi wetu kadhaa serikalini katika kadhia tofauti tumeshawasikia wakisema kuwa wahalifu wanawafahamu lakini wanawapa muda wajirekebishe.

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema kuwa amepelekewa orodha ya wauza unga, lakini anawapa muda mpaka Krismasi, ikimalizika atawashughulikia...

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema anawajua waliojichukulia na kujihodhia fedha za Madeni ya Nje za Benki Kuu (EPA) lakini akawapa muda wazirejeshe...

Hii imekuwa ndiyo tabia, yamekuwa ndiyo mazoea, umekuwa ndio utamaduni mpya tulioamua kuufuata; utamaduni wa kuwahifadhi waovu, utamaduni wa kutowataja wezi, utamaduni wa kuwaonea haya wahalifu, utamaduni wa kuwapa muda wajirekebishe.

Wengine wamejifunza utamaduni wa kuwavumilia wanaowachafua, lakini hili la kutowataja wanaofisidi mali ya umma, wanaohawilisha rasilimali za taifa, hapa tumekithiri ada!

Wanahamisha nyara za taifa, wanasafirisha mpaka wanyama tunawavumilia, tunawaangalia tu. Wanachimba madini yetu, wanatuachia mashimo yasiyozibika, sisi tupo tunawaangalia tu, eti tunajivunia amani na utulivu.

Ni amani gani aliyonayo mtu anayeishi kwa mlo mmoja kwa siku? Ni amani gani anayoipata mtu anayetafuta maji kuanzia saa nane za usiku mpaka saa 6 mchana, anasubiri chemchem ifumuke, achote kwa kata, tena kwa utulivu ili asiyachafue? Haya ndiyo maji anayotarajia kwenda kunywa yeye na familia yake. Anafanya hivyo kwa sababu ahadi ya kupelekewa maji hadi kwenye kaya yake bado haijatekelezwa kwa sababu Serikali haina fedha, lakini Serikali hiyohiyo inawaangalia baadhi ya wananchi wake na hata wawekezaji iliyowaalika waje nchini kuwekeza, wakihamisha rasilimali za taifa.

Ni utulivu gani anaoupata mama mjamzito ambaye katika zama hizi zenye maradhi ya kuambukiza ya kila aina, anapokwenda hospitalini kujifungua anakuta wanalazwa watatu katika kitanda kimoja?

Ni utulivu gani anaokuwa nao mwanafunzi wetu wa shule ya msingi pale anapoketi sakafuni na kuandika kwenye daftari lake hali ya kuwa amepinda mgongo na kukunja miguu?

Kwa hali hii ya kutodhibiti mali ya umma, hali ya kuwaacha wachache wakifaidi keki ya taifa, hali ya kuwaacha walafi wakikomba mboga yote na kuwaacha watoto wetu wakiwa na utapiamlo; kiasi kiongozi wetu aseme Tanzania ina rasilimali nyingi, lakini hajui kwanini bado ni masikini.

Atajuaje? Wakati wanayoyafanya hayo wanafanya kwa kificho? Wakati wanahamisha mamilioni ya fedha kwenda kuyaficha nje ya nchi kama wezi? Wakati watu hawako wazi na wala si wa kweli?

Masikini Tanzania imegeuzwa shamba la bibi, tena bibi mwenyewe keshafariki, shamba halina msimamizi, wajukuu wanajichumia hata vilivyo vichanga, visivyopea wanavipepea kwa moto, wanahamisha badala ya kula wao au hata kuwaruhusu wenzao kujichumia na kukidhi njaa, hamu na kuondosha ghamu zao. Hii ni hatari!


0655 849694





Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

KUHUSU MIMI

JINA:Hawra Shamte
MAKAZI:Dar es salaam
NCHI:Tanzania
KAZI:Mwandishi

KUELEKEA BUNGE LA BAJETI 2006

QuickTopic free message boards
Bonyeza hapa ili uweze kuelezea: NINI MTAZAMO WAKO JUU YA BAJETI IJAYO YA MWAKA 2006/07 NCHINI TANZANIA?

VYOMBO VYA HABARI MTANDAONI

  • The Citizen
  • Mwananchi
  • Mwanaspoti
  • Business Times
  • Majira
  • Daily News
  • Nipashe
  • The Guardian
  • The Express
  • Kiongozi
  • Uhuru/Mzalendo
  • Arusha Times
  • BLOGI ZA KISWAHILI

  • Bangaiza
  • Mwandani
  • Pambazuko
  • Damija
  • Mtafiti
  • Martha
  • Gaphiz
  • Swahili time
  • Miruko
  • Dira yangu
  • Msangimdogo
  • Jeff Msangi
  • Kasri la mwanazuoni
  • Kurunzi
  • Baragumu
  • Mawazohuru
  • Fikra Thabiti
  • Mtandaoni
  • Motowaka
  • Mkwinda
  • Ngurumo
  • Nyembo
  • Bwaya
  • Omega
  • Tafakari za Maisha
  • Nuru akilini
  • Mtandawazi
  • Mhujumu
  • Vijimamboz
  • Wakati wa Ukombozi
  • Kijiwe Joto
  • Watoto Wetu
  • Jungu kuu
  • Kisima cha Weledi
  • Jarida la Ughaibuni
  • Bhalezee
  • Sauti ya Baragumu
  • Kona yangu
  • Furahia Maisha
  • Bakanja
  • Terrie Swai
  • Fatma Karama
  • Kazonta
  • Binti Afrika
  • Blogu ya Kilimo
  • Ukombozi
  • Mwafrika
  • Digital Africa
  • Blogu ya lugha mseto
  • BLOGI ZA WAAFRIKA

  • BLOGAFRICA
  • BLOGU ZA WAAFRIKA
  • DIGITAL AFRICA
  • MAMA JUNKYARD'S
  • MSHAIRI
  • KENYAN PUNDIT
  • MONGI DREAMS
  • ISARIA MWENDE
  • CUNNING LINGUISTICA
  • ETHIOPUNDIT
  • MOCHALICIOUS
  • UNGANISHA
  • DEMOKRASIA KENYA
  • CHANUKA
  • BANKELE
  • MAARIFA/AKIEY
  • AFROMUSING
  • NEHANDA DREAMS
  • BLACK LOOKS
  • YUMMY WAKAME
  • AFRICAN OIL POLITICS
  • NUBIAN SOUL
  • SANAA
  • VIRTUAL INSANITY
  • MENTAL ACROBATICS
  • KENYA UNLIMITED
  • JIKUMBUSHE KAZI ZANGU ZA ZAMANI

    April 2006 May 2006 June 2006 October 2007 November 2007 December 2007 May 2008 July 2008 October 2008 July 2009 August 2012 October 2012

    Imetengenezwa na

    Ukibofya hapa utapelekwa katika Blogi ya msangimdogo

    na inawezeshwa na