<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597</id><updated>2011-09-04T21:18:44.924-07:00</updated><category term='Profesa Haroub Othman'/><category term='mafuta'/><title type='text'>mnyongemnyongeni</title><subtitle type='html'></subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>16</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-2102238275485612446</id><published>2009-07-22T23:55:00.000-07:00</published><updated>2009-07-23T00:10:02.363-07:00</updated><title type='text'>Waislam, jukumu la kuanzisha Mahakama ya Kadhi ni lenu</title><content type='html'>WIKI iliyopita wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa papo bungeni alisema kwamba serikali haijalitupa suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi, lakini imependekeza kuwa kutokana na suala hilo kuwa la imani, liundiwe mfumo wake ambao hautasimamiwa na dola ili chombo hicho kiendelee kuwa nguzo muhimu ya dini ya Kiislamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pinda amesema kwa kuwa Mahakama ya Kadhi ni suala la imani, hivyo Waislam waiunde katika mfumo wao na serikali itatoa msaada kwa chombo hicho hadi kitakaposimama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amesema chombo hicho kikiundwa na kusimamiwa na dola serikali itakuwa inakiona kama chombo chake cha dola tu hivyo haitakuwa imetenda haki kwa Waislam na hata Watanzania kwa ujumla wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkuu amesema kwa kuwa inasemwa kwamba Mahakama ya Kadhi, au ofisi ya Kadhi msingi wake ni imani ya dini, hivyo anadhani si busara chombo hicho kikawekwa katika mfumo unaotakiwa kusimamiwa na dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli hiyo ya Waziri Mkuu ni wazi kwamba Waislam sasa wanapaswa kukianzisha chombo hicho wao wenyewe na kutafuta utaratibu mwafaka wa kuzifanya sheria na maamuzi yake yakubalike na jamii ya Waislam nchini Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi nakubaliana kwa asilimia 100 na tamko hilo la Waziri Mkuu Pinda, kwani ni wazi kwamba serikali itakapoianzisha mahakama hiyo itabidi iwe ni miongoni mwa vyombo vya serikali na itakayosimamiwa na serikali yenyewe na wala si Waislam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali mwaka 1968 iliivunja Jumuiya ya Kiislam iliyoitwa East African Muslim African Society (EAMWS) jumuiya iliyoanzishwa na Agakhan na ambayo viongozi wake wengi walikuwa ni wenye asili ya Kiasia.  EAMWS kama jina lilivyo ilikuwa ni jumuiya ya Waislam ya Afrika Mashariki.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kuona kuwa Waislam wa Tanzania kwa ujumla wao hawawakilishwi vema na EAMWS na kutoa malalamiko kadhaa wa kadhaa, ndipo serikali ilipoifuta jumuiya hiyo na kuwahamasisha viongozi Waislam waliokuwa Serikalini kusimamia kuanzishwa kwa jumuiya nyengine ya Waislam wa Tanzania.  Kwa msaada wa Sheikh Abeid Karume na Sheikh Rashid Kawawa waliwakutanisha masheikh wa Kiislam pale Iringa mwaka huo huo 68 na kuanzisha Baraza Kuu la Waislam Tanzania, na kwa kuwa EAMWS ilivunjwa kisheria, mali zote zilizokuwa za EAMWS zilimilikishwa BAKWATA.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kutokana na insafu hiyo, BAKWATA kwa Waislam ikawa inaonekana kuwa ni chombo cha serikali japokuwa serikali haiwachagulii kiongozi wala haiwalipi mishahara isipokuwa hutoa msaada pale inapoombwa kufanya hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na iktisadi hiyo na pengine matendo yasiyoridhisha au yasiyoisaidia jamii ya Kiislam kwa ujumla wake nchini, ndipo mara baada ya kufunguliwa milango ya mfumo wa kiliberali na ruhusa ya kuanzishwa kwa vyama vya kijamii katika miaka ya 1980, ndipo jumuiya nyingi za Kiislam zikaibuka kama uyoga.  Nia ikiwa kuziba mapengo pale ambapo Bakwata imeshindwa na pengine kuwafanya Waislam wawe wamoja zaidi.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislam mathalan, lililoanzishwa kwa jitihada za wasomi na masheikh mbalimbali wasiokubaliana na mawazo na matendo ya Bakwata, ilidhaniwa kuwa hilo lingeweza kujenga jumuiya yenye nguvu na kuwaunganisha Waislam wawe na sauti moja.  Hadi leo Baraza hilo lina umri wa  miaka 15 na bado halijapiga hatua, ndio kwanza linasimama dede na wala jitihada zake za kuunganisha jumuiya na taasisi za kiislam hazijafanikiwa kihivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jitihada nyingine za Waislam za kuwanyang’anya Bakwata mamlaka yao kwa Waislam nchini, walianzisha Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA).  Baraza hilo hadi sasa limebakia Kisarawe tu.  Waislam wanapaswa kujiuliza kwanini jitihada zao zinasuasua, watafute mbinu za kujikwamua na waache kuwanyooshea wengine vidole?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja iliyopo ni kwamba ikiwa Waislam hawaipendi Bakwata kwa madai kuwa ni kibaraka wa serikali, itakuwaje kwa Mahakama ya Kadhi endapo itaundwa na kuingizwa katika mfumo wa Serikali?  Je, itakuwa ni chombo cha Waislam au chombo cha Serikali?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi nadhani Waislam walikokotwa na ahadi za kisiasa zilizoanza kutolewa na Augustine Mrema wakati akiwa NCCR Mageuzi na baadaye hoja hiyo kupokwa na CCM.  Ukiiangalia kwa undani wake utaona kuwa ni hoja ya kisiasa tu ambayo hujengwa kwa maslahi ya wakati fulani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadhalika kuna madai ya kwamba zipo nchi zenye ofisi ya Kadhi Mkuu na Mahakama ya Kadhi ambazo zinasimamiwa na Serikali, hiyo ni kweli lakini ukiangalia utakuta kwamba idadi ya Waislam katika nchi hizo ni ndogo, hivyo serikali inachofanya ni kulinda haki za wachache (minority rights) lakini katika nchi kama Tanzania ambayo takribani idadi ya Waislam na wasio Waislam inakaribiana, kuunda chombo cha kisheria kitakachosimamiwa na dola kwa maslahi ya dini moja pengine ni hoja yenye ukakasi kidogo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli iko haja ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na ofisi ya Kadhi Mkuu nchini Tanzania lakini si haki kuishinikiza serikali kuanzisha mamlaka hizo, Waislam wenyewe wanapaswa wazianzishe na kuzisimamia, wanachopaswa kuitaka serikali kufanya ni kuzitambua tu kisheria na  kutoa msaada pale inapohitajika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo swali linalojitokeza ni kuwa ni nani atakayemfunga paka kengele?  Swali hilo linakuja kwa sababu nchini Tanzania Waislam hawana mamlaka moja wanayoiamini na kuitegemea kusimamia mambo yao, Waislam wamegawanyika si kwa madhehebu tu bali kwa makundi na kwa taasisi mbalimbali ambazo kimsingi nyingi hazikubaliani kimtazamo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawra Shamte ni mhariri wa siasa wa gazeti la Mwananchi.&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;br /&gt;0754 849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-2102238275485612446?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/2102238275485612446/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=2102238275485612446&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2102238275485612446'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2102238275485612446'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2009/07/waislam-jukumu-la-kuanzisha-mahakama-ya.html' title='Waislam, jukumu la kuanzisha Mahakama ya Kadhi ni lenu'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-2343228035243008049</id><published>2009-07-14T08:11:00.000-07:00</published><updated>2009-07-14T08:13:54.169-07:00</updated><category scheme='http://www.blogger.com/atom/ns#' term='mafuta'/><title type='text'>Mzimu wa Muungano tusipoutuliza utatukosesha amani</title><content type='html'>MAFAHALI wawili wakipigana ziumiazo nyasi.  Huo ni msemo maarufu wa Kiswahili ambao bila shaka una maana pana. Hivi sasa hapa kwetu kuna mafahali wawili wapiganao, yeyote yule atakayebwagwa au hata ikiwa kila mmoja mwisho wa siku atashika njia yake, lakini ni wazi kwamba nyasi zitakuwa zimegaragazwa.  Suala la mafuta ambayo yanadaiwa kuwapo Zanzibar limegeuka mzimu unaokuja na kuondoka, lakini hivi sasa unaonyesha kana kwamba umeamua kubaki kwetu, unatukokoteza, unaturudisha nyuma, unatutia wahka. Kwa kawaida mzimu wowote hutulizwa, hivyo ili na huu usiendelee kutuandama tunapaswa kutafuta njia za kuutuliza, kinyume cha hivyo utatukosesha amani.  Suala hili limekuwa likiibuka mara kwa mara kwa sababu tu kwa muda wote limekuwa likishughulikiwa kwa udanganyifu, inaonyesha kana kwamba katika kamati ya kushughulikia kero za Muungano inayoongozwa na Makamu wa Rais wajimbe wakiwemo, Waziri Mkuu kwa upande wa Bara na Waziri Kiongozi kwa upande wa Zanzibar, kuna watu ambao wanaogopana, au labda kuna upande unaouogopa mwingine na kushindwa kuambizana ukweli na kinachobaki ni kutoa ahadi za kisiasa tu zisizo na mwisho, “suala hili tunalishughulikia,” siku zinakwenda, miezi inapita, miaka inakatika, awamu zinabadilika, ahadi hiyo bado ingalipo.  Mara hii Wazanzibari wameamua kumtafuna jongoo kwa meno. Kasimama Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Yusuf Himid mbele ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Mkuu wa Shughuli za Serikali ndani ya Baraza, Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha akiwapo na akiwa kimya kumsikiliza.  Kwa sauti kubwa na ya hamasa, Himid akasema ‘Wazanzibari tumechoka kuburuzwa katika suala hili, sasa huu ni uamuzi wa Baraza la Mapinduzi kwamba mafuta tunayatoa rasmi katika mambo ya Muungano…” Kiongozi wa mambo ya Serikali Barazani yuko pembeni kaketi, kimya kanyamaza, anang’aa ng’aa macho tu.  Hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba Himid kapata baraka zote kutoka kwa wakuu wake kulisema jambo hilo, maana yake ni kwamba sasa watu wanataka kupimana nguvu. “Hii ni serikali ya Mapinduzi ati! Ikiwa hawa wenzetu hawataki kuelewa hivyo, itabidi sasa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itumie uamuzi wa nchi za kimapinduzi katika kuliondoa suala la mafuta na gesi asilia kwenye orodha ya mambo ya Muungano…”  Bara nako wakubwa wanasema yao, eti Wazanzibari wanajifurahisha, eti mwenye mamlaka ya kutoa jambo katika Katiba ya Muungano ni Bunge tu. Hee! Kasheshe!Mara hii hapatoshi! Huenda pakachimbika bila sululu.    Wazanzibari sasa wameamua kulishughulikia suala la mafuta na pengine mambo mengineyo yaliyoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano kutoka kumi na moja hadi 22, ilikuwaje yakaongezwa? Kwa idhini ya nani?  Katika vikao vipi? Hayo ni maswali yanayoulizwa na bado hayajapata majibu labda kwa sababu hakuna mjibuji au hayajibiki.      Wazanzibari sasa wanasema katika hili watatumia ukaidi, na kwa ukaidi hawajambo! Kwa ubishi kama wenyeji wa Kigoma, ubishi wao hawishi, wako tayari kukata kole la mnazi ili kuhesabu nazi zilizomo kwa sababu walishindana idadi yake wakati kole likining’inia mnazini, sasa kupata uhakika ni lazima liangushwe ili nazi zihesabiwe watu wote wakiona, huo ndio ukaidi wanaotaka kuuanzisha Wazanzibari na kwa hili husahau tofauti zao za kisiasa, hivi sasa itikadi yao moja tu, Uzanzibari na haki yao katika Muungano, likimalizika hili wataurudia ubishi wao wa zamani ule wa CCM na CUF waliouweka pembeni.  Hali hiyo inaonyesha kwamba viongozi wetu wameshindwa kulishughulikia suala hili, lakini kwa kuliacha hivi lilivyo kwa kila mwenye kinywa, sauti na nafasi kusema atakavyo, huenda lisitufikishe popote na badala yake kuzua mgogoro mkubwa au pengine tuseme kwamba sasa mgogoro wa kikatiba utaibuka na hautazimika mpaka zijulikane mbichi na mbivu.  Mara kwa mara wataalamu wa masuala ya siasa wamekuwa wakipendekeza kwamba tatizo hilo lianze kutatuliwa katika chanzo chake na si katika matawi, tatizo ni Katiba na Mkataba wa Muungano au pengine tatizo ni Muungano wenyewe.    Inashangaza kuona kwamba watawala hawataki na wala hawapendi mambo haya yaguswe, lakini ni vyema yakaguswa na kuzungumzwa leo kuliko kusubiri mpaka ukaidi na mabavu yatumike kwani kwa kuruhusu hayo kutokea, huenda tukagawana mbao!  Hiyo ni kuonyesha kwamba subira ya wananchi wa Zanzibar sasa inakaribia kufikia kikomo na hiyo inadhihirishwa kutoka vinywani mwa wawakilishi wao, haya mambo si ya kuyafanyia mzaha kwani Waswahili wanasema; ‘Mzaha mzaha, hutumbuka usaha.’    Binafsi nadhani mpira huu wa masuala ya Muungano sasa unapaswa kuchezwa na wakuu wa nchi husika, wasiachiwe Mansour Himid na Adam Malima kurushiana pasi kali na kuziumiza nyasi, kwani hawa ni vijumbe tu, tunawaomba wahusika waingie uwanjani walisakate kandanda!  Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa Gazeti la Mwananchi. hshamte@mwananchi.co.tz 0754 849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-2343228035243008049?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/2343228035243008049/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=2343228035243008049&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2343228035243008049'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2343228035243008049'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2009/07/mzimu-wa-muungano-tusipoutuliza.html' title='Mzimu wa Muungano tusipoutuliza utatukosesha amani'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-1690772416918992559</id><published>2009-07-14T07:55:00.001-07:00</published><updated>2009-07-14T08:05:21.563-07:00</updated><category scheme='http://www.blogger.com/atom/ns#' term='Profesa Haroub Othman'/><title type='text'>Fikra pevu kamwe haitakufa</title><content type='html'>NI vigumu kuamini, lakini ni kweli, wakati wake ulifika, aliitwa naye akaitika. Atakumbukwa kwa mengi mazuri, hasa kwa mchango wake kwa jamii.  Mpiganaji wa haki za binadamu na msema kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Haroub Othman Miraji (68) ni vigumu kwa anayemtambua kuamini kuwa ametutoka, amekwenda kwenye pumziko la milele.  Ingawa binadamu hapendi kuamini linapomtokea linalomuhuzunisha, au kwa vile ana tabia ya kupenda kusikia yale yanayompendeza tu, kifo cha Profesa Haroub kilitufanya wengi kutoziruhusu akili zetu kukubali ukweli, lakini bado ukweli unabaki pale pale, kwamba pamoja na kuwa tulimhitaji lakini Mungu alimhitaji zaidi, wakati wake ulifika, aliitwa na akaitika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama mpigania haki mashuhuri wa Afrika Kusini Steven Biko alivyowahi kusema kwamba ‘fikra njema ni ile isiyokufa na ni vema kufa kimwili kuliko kufa kifikra,’ fikra na mawazo ya Profesa Haroub yatadumu milele, ulioondoka kwetu ni mwili tu lakini fikra zake zitabaki kuwa hai kwa wanamapinduzi na wapigania haki za wanyonge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Haroub ni alama ya fikra pevu, mahiri na yenye busara.  Pamoja na wadhifa aliokuwa nao na heshima katika jamii lakini alikuwa mtu wa watu, tayari kuzungumza na kila aliyemkabili, hakubagua mdogo wala mkubwa, kwake yeye mwenye elimu na asiyekuwa na elimu hakuwa na tofauti katika misingi ya kibinadamu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliamini kwa dhati kwamba binadamu wote ni sawa, hakujikweza wala hakutakabari. Binafsi Profesa Haroub alikuwa ni chanzo changu cha habari (source).  Kila ninapotingwa na jambo hasa katika masuala ya siasa, mitafuruku na migogoro yake, Profesa Haroub ndiye aliyekuwa kimbilio langu, simu moja tu ilitosha kupanga naye miadi ya kufanya mahojiano na kama hayupo nchini atakwambia ‘niandikie maswali unitumie mtandaoni.’   Ukimwambia muda wa mwisho wa kuwasilisha, hakikisha kwamba majibu yako utayapata ndani ya muda mulioahidiana.  Ukimwambia nitakuja ofisini kwako saa tatu asubuhi, saa tatu kasoro robo yeye atakuwa ameshafika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Haroub alikuwa mahiri katika kudadavua suala la kisiasa Zanzibar na pia alikuwa rejea muhimu katika masuala ya katiba na sheria. Bila kigugumizi Profesa Haroub siku moja aliniambia kwamba ‘Katiba ya Tanzania imejaa viraka,’ nami nikaandika hivyo katika makala.  Hata hivyo hakuishia hapo ila alivieleza viraka vingi vilivyomo katika katiba na kisha kutoa ushauri.  Alisema kwamba kama nguo imejaa viraka kweli yaweza kuvalika?  Uking’ang’ania kuivaa bila shaka siku moja itakuadhiri.  Akaendelea kusema kwamba nguo yenye viraka vingi inapoteza uhalisia wake, inapoteza taswira yake ya awali, hivyo kama uliupenda mshono wake ni vema ununue kitambaa kingine ushone mpya.  Huo ndio mfano unaoakisi katiba ya Tanzania ambayo kimsingi haikidhi haja ya mfumo wa vyama vingi vya siasa kwa sababu yenyewe asili yake ni katiba ya chama kimoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kupigania mabadiliko ya katiba, Profesa Haroub alikuwa mstari wa mbele kupigania kuwapo kwa Tume huru za uchaguzi ili kufanyika kwa chaguzi huru na haki hapa Tanzania.  Kwa maneno mepesi ni kwamba alikuwa mwanademokrasia mtetezi wa wanyonge na mpiganaji wa haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuwa alikuwa muwazi na msema kweli, wapo viongozi ambao hawakumpenda na wako wengine walimnasibisha na chama cha siasa hasa cha upinzani, lakini kimsingi Profesa Haroub hakujifunga na chama chochote cha siasa na ndiyo maana akawa anaweza kukosoa na kusema kweli. Alichokuwa akikikosoa si chama bali ni mfumo wa siasa uliopo nchini na kwamba mfumo huo kubadilishika kwake ni lazima uanzie katika katiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na usomi wote aliokuwa nao, Profesa Haroub hakujitenga na watu wa kawaida, alishiriki katika shughuli na hafla mbalimbali alizotaarifiwa. Mimi alinifanya kama mtani wake, alikuwa akiweza kunipigia simu na kunambia; “hivi sasa niko kwenu Pemba, vipi nikuletee mashelisheli?”&lt;br /&gt;Profesa Haroub pamoja na usomi wake, alijichanganya!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitu kimoja muhimu nilichokigundua kwake ni kwamba pamoja na kuwa alikuwa tayari kushirikiana na vyombo vya habari kwa wakati wowote ule lakini alikuwa makini.  Neno lake kila siku lilikuwa ‘nisikilize kwa makini, usininukuu vibaya.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kwamba alikuwa na kazi nyingi, midahalo mingi na mihadhara mingi lakini utashangaa jinsi alivyokuwa na shauku ya kusoma.  Ofisini kwake hakuingiliki, vitabu kila pembe, vimefurika mpaka vimepitiliza, lakini hakuwa akisahau alipoweka kitabu.  Unapokwenda kufanya mahojiano naye na ukawa unataka kumrikodi ni lazima usogeze kidogo vitabu na makabrasha yatakayokuwapo mezani kwake au ukiweke kitonge (tape recorder) chako juu ya vitabu.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku moja nilibahatika kufika nyumbani kwake pale Chuo Kikuu, nako mambo hayakuwa tofauti sana na ofisini kwani mashubaka yote yalijaa vitabu, meza za ukumbini nazo zilikuwa na vitabu vilivyofunuliwa kuonyesha kuwa wapo watu waliokuwa wakifanya kazi ya kusoma na kuongeza ujuzi.  Kwa bahati nzuri mke aliyemuoa ni sawa na yeye, Profesa Saida Yahya Othman, naye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, hivyo wote walikuwa ni wapenzi wa kusoma, wakawa wamefanana sawasawa kama sahani na kawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimaumbile Profesa Haroub alikuwa ni mpole lakini makini, hakuwa msemaji ovyo na alikuwa ni msikilizaji mzuri, na hiyo ndiyo sifa ya mtu anayependa kujifunza, hakuwa mtu mwenye dharau hata kidogo, hata kama ulichomuuliza sicho, atakujibu kwa hekima kubwa huku akikuelekeza kilicho ndicho, kwamba ‘tatizo si hilo bali ni kitu fulani na ambacho nadhani kimesababishwa na kitu fulani.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1992 Profesa Haroub akishirikiana na wenzake, Fatma Maghimbi na Hassan Said walianzisha Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Zanzibar baada ya kuona kwamba jamii ya Kizanzibari inahitaji kufahamu haki zao na kuwa na taasisi ambayo angalau itasimamia kutendeka kwa haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Azma ya kituo hicho ambacho hadi umauti ulipomkuta, Profesa Haroub alikuwa mwenyekiti wake, ni kuhakikisha kuwa kila mkazi wa Zanzibar hususan masikini, wanawake, watoto, walemavu na makundi mengine yenye nafasi finyu katika jamii wanaelewa kuhusu haki zao za msingi na wanazifanyia kazi ili kujenga jamii inayofuata misingi ya sheria na inayoongozwa na utawala bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku moja nilizungumza na Profesa Haroub kuhusu uwepo wa kituo hicho na suala zima la utawala bora Zanzibar naye akasema; “ni vigumu kuwa na utawala bora ikiwa watu wanaoongozwa hawajui hata maana yake, hawaelewi umuhimu wa sheria na kwa ufupi hawajui haki zao. Hivyo dhamira kuu ya kuanzisha kituo hicho ni kuwashajiisha Wazanzibari kujua haki zao kwa kuwapa mafunzo kwa njia tofauti na pia kuwasaidia kutetea haki zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipozungumza naye alinambia kuwa kituo hicho kimedhamiria kuinua upeo wa wananchi juu ya masuala ya sheria, haki na wajibu wa mwananchi kwa nchi yake kwa kuendesha semina, warsha, mikutano pamoja na kutoa ushauri wa kisheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Haroub hakuishia hapo bali alieleza pia uzoefu wake kwa watu wenye madaraka na alisema “kuna tabia ya watu hasa wenye mamlaka kuchezea sheria, wanahisi kama kwamba sheria haiwahusu au hata kama inamuhusu anaweza kuipinda, ikiwa watu kama hao wataendelea kupewa mwanya katika jamii, suala la utawala bora litakuwa ni la hadithini tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Haitoshi kutamka kwamba unafuata utawala bora, au hata kuwa na Wizara inayoshughulikia masuala ya utawala bora, halafu wanaovunja haki za binadamu ni maafisa wa vyombo vya dola,” alisema Profesa Haroub.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ni baadhi tu ya matamshi yaliyotoka kwenye kinywa cha mwanadiplomasia, mwana demokrasia na mpiganaji wa haki za binadamu, Hayati Profesa Haroub Othman.  Kifo chake kimeacha pengo kwa Watanzania wote, wanazuoni na wanajamii aliojitolea muda wake na uwezo wake kuwatetea, kuwafumbua macho, kuwazibua masikio na kuwaonyesha njia ya kuelekea kwenye utawala wa sheria na unaoheshimu haki za binadamu.  Mchango wake kwa jamii ni mkubwa na bila shaka jitihada zake iko siku zitazaa matunda.  Uliokufa ni mwili tu, fikra na mawazo yake bado yataendelea kuwapo. Profesa Haroub aliiaga dunia Juni 28, mjini Zanzibar na kuzikwa Juni 29, 2009.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-1690772416918992559?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/1690772416918992559/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=1690772416918992559&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1690772416918992559'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1690772416918992559'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2009/07/fikra-pevu-kamwe-haitakufa.html' title='Fikra pevu kamwe haitakufa'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-5674740649485191573</id><published>2008-10-15T02:40:00.000-07:00</published><updated>2008-10-15T02:49:44.005-07:00</updated><title type='text'>Tumejifunza nini kutokana na uchaguzi mdogo Tarime?</title><content type='html'>KAMPENI rasmi za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime zilianza Septemba 21.  Kampeni hizo zilizofanyika kwa wiki tatu mfululizo hadi kukoma siku moja tu kabla ya uchaguzi uliofanyika Jumapili iliyopita, Oktoba 12 kwa hakika ziliwasimamisha dede Watanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila kukicha habari za kutoka Tarime zilipamba vichwa vya habari vya magazeti, nyingi hazikuwa za kufurahisha, zaidi ni vitisho na wasiwasi kwamba Tarime hapatoshi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vijembe na kejeli mara hii havikufua dafu kwani vilizidiwa na mapanga na mawe.  Wengi walijeruhiwa na wengine kupoteza maisha yao.  Kama vile haitoshi hata kiumbe asiyejua kitu kuhusu uchaguzi, mbwa aliyevishwa sare ya CCM, alikatishwa maisha yake kutokana na ushabiki usio wa kistaarabu.  Tuliouona Tarime haukuwa ushabiki wa kisiasa bali wa kihuni.  Tulisahau kauli mbiu ya kushindana bila kupigana.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali ya kawaida hiyo haikuwa demokrasia na pengine ni vigumu kuuita uchaguzi ule kuwa ulikuwa huru, pengine ulikuwa wa haki lakini haukuwa wa amani. Yaliyotokea Tarime yanaakisi hali ya kutokuwapo kwa demokrasia halisi Tanzania.  Demokrasia yetu bado ni ya ‘magubegube’ (ya kubabaisha).  Bado tunadhani kwamba ushindi ni lazima, wanasiasa wanajaribu kila mbinu kuhakikisha ushindi bila ya kuheshimu utashi wa wananchi. Bado wako wanaodhani kwamba wana haki ya kutawala au kuchukua viti vyote vya uwakilishi.  Bado demokrasia haijatuingia akilini mwetu kwamba ni uhuru wa kuchagua kiongozi unayemtaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bado tunadhani tunaweza kushinda kwa njia za wizi na ulaghai.  Bado tunafikiria kuwa kinachotakiwa ni ‘ushindi wa kishindo’ kumbe vile wananchi wanachotaka ni mwakilishi wao atakayetetea maslahi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napenda kuungana na wale wenye maoni ya kwamba demokrasia ya vyama vingi kwa Afrika ni demokrasia ngeni, pengine tunahitaji muda zaidi wa kujifunza au pengine si demokrasia stahiki kwa watu wa Bara hili wenye miundo yao ya asili ya utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inaonyesha kana kwamba demokrasia hii tuliyonayo ni demokrasia ya kupandikizwa na kulazimishwa kwetu, wenyewe hatujawa tayari.  Hata hivyo, bado hatujachelewa, kama kweli tunaipenda na tunataka iingie katika mizizi ya mifumo yetu ya uongozi wa umma, basi tuwe tayari kujifunza na katika kujifunza tujitahidi kujiepusha na mabaya, kwa mfano kutumia nguvu wakati wa kampeni na wakati wa uchaguzi, kutumia nguvu za dola za ziada na hata kufanya mbinu za kupata ushindi usio halali.  Hayo ni mambo ambayo kama kweli tunayo dhamira ya kufuata mfumo huu wa demokrasia uliopandikizwa kwetu, mambo hayo yamo ndani ya uwezo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Demokrasia hii tunayoiga haitaki mizengwe, ina misingi yake iliyo bayana, demokrasia hii haihitaji risasi wala mabomu.  Lakini ni demokrasia inayopaswa kufuatwa na watu wote katika jamii, wapiga kura, wanasiasa na hata Serikali.  Kama tutaizingatia misingi hiyo ya demokrasia ni wazi kwamba tutajiepusha kwa kiasi kikubwa na tafrani zinazotokea wakati wa uchaguzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi nadhani hatuhitaji Jumuiya ya Ulaya ituambie la kufanya, hatuhitaji wakaguzi wa nje waje watwambie kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki.  Hatuhitaji kufundishwa hayo, kwani hayo yamo ndani ya uwezo wetu, ni utashi na matakwa yetu na ni ustaarabu tunaoweza kuujenga tukitaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kuna jingine, ambalo pengine ni funzo kwa Chama tawala, kwamba wananchi wanaposema ‘hapana’ maana yake ni ‘hapana.’  Tarime wametupa fundisho, wananchi wa Tarime pengine ukali ni khulka yao, ni watu wasiokubali kunyanyaswa wala kuonewa, ni watu walio tayari kusimamia haki zao hata kama ikibidi wengine kupoteza maisha yao, hiyo ndiyo gharama ya demokrasia, lakini gharama hii ni kubwa mno na ambayo tunapaswa kuhakikisha kwamba hatuingii katika gharama za aina hiyo katika chaguzi zozote zile ziwazo hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini twapaswa kufahamu kwamba Watanzania kuna kitu wamejifunza kutoka Tarime na kama wataamua kutumia mbinu kama za wakazi wa Tarime katika kuhakikisha kwamba wanalinda haki yao ya kuchagua, basi bila shaka Tanzania patakuwa hapakaliki, patachimbika bila jembe!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala na viongozi wa vyama vya siasa wanapaswa waheshimu matakwa ya wananchi na wawape uhuru wao wa kuchagua.  Hakuna ubishi kwamba kila anayeingia katika ushindani anaingia kwa dhamira ya kushinda, lakini kushinda huko hakupaswa kuwe ‘kwa kucha na meno!’  Mwageni sera zenu wananchi watazisikia.  Kwanini hatuchukui mfano wa biashara?  Wafanyabiashara kama 10 wanakuwa wamejipanga katika mstari mmoja na pengine wote wanauza bidhaa za aina moja, lakini wakati huo huo wanaheshimu utashi wa wateja wao.  Mteja anaweza kumruka mfanyabiashara wa kwanza na akaenda kwa mfanyabiashara wa katikati au wa mwisho.  Na hiyo ndiyo dhana ya biashara huria na pia inapaswa iwe dhana ya siasa huria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia kama ambavyo kwenye biashara zipo za ‘kimachinga’ ambazo mmachinga utakapomuuliza bei ya kitu ni lazima ukinunue, usipokinunua utavurumishiwa gunia la matusi mpaka utamani ardhi ipasuke ujifukie.  Na siasa nazo ziko za namna hiyo pia, zile za Tarime ukiwa ni mfano mmoja wapo.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunakumbuka jinsi Mwenyekiti wa DP, mchungaji Christopher Mtikila alivyovurumishiwa mawe, kisa eti alitamka yasiyowaridhi wana-Tarime.  Hizo ni siasa za ‘kimachinga’ lazima ukubaliane na wanayoyataka wachuuzi. Lakini hiyo ni ilani iliyo kiambazani inapaswa kuzingatiwa, tayari moshi umeshaanza kufuka, tutahadhari nyika zisishike moto!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0754 849694&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-5674740649485191573?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/5674740649485191573/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=5674740649485191573&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/5674740649485191573'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/5674740649485191573'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2008/10/tumejifunza-nini-kutokana-na-uchaguzi.html' title='Tumejifunza nini kutokana na uchaguzi mdogo Tarime?'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-1734287972874526624</id><published>2008-07-31T07:47:00.000-07:00</published><updated>2008-07-31T07:49:20.744-07:00</updated><title type='text'>Mfumo wa uongozi na demokrasia Afrika, ni mkorogovyogo!</title><content type='html'>Na Hawra Shamte&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;UKIANGALIA mlolongo wa matukio, visa na mikasa ya viongozi wa Bara la Afrika, moja kwa moja utabaini kuwa mengi wafanyayo ni yale yaliyoainishwa katika falsafa za Niccolo Machiaveli, mwanafalsafa wa karne ya 15 aliyezaliwa Roma Italia.&lt;br /&gt;Katika masuala ya uongozi wa umma, Machiaveli aliweka mkazo kwa kiongozi kung’ang’ania kuendelea kubaki madarakani, alisisitiza kwamba ‘ufalme’ au uongozi ni lazima ulindwe kwa nguvu zote, hata ikibidi kutumia jeshi ama kuua.&lt;br /&gt;Kama ni utashi wao, viongozi wengi hasa wa Bara la Afrika wangependa waendelee kukaa madarakani daima dawama, kwao wao ukishakamata madaraka ni sawa na pingu za maisha, hadi ufe uzikwe.&lt;br /&gt;Mifano tunayo mingi, Wapo akina Yoweri Museveni, Robert Mugabe, Omar Al Bashir, Husni Mubarak na wengineo.  Sidhani kwamba ni lazima wajitangaze kuwa ni maraisi wa maisha, bali vitendo vyao vinatosha kuthibitisha hayo.  Je, demokrasia ya uchaguzi na kupishana madarakani inatumikaje Afrika?&lt;br /&gt;Pengine demokrasia ya aina hiyo si demokrasia ya waafrika, uongozi wa jadi ungetosha kujenga misingi ya uongozi na demokrasia, kwani hivyo ndivyo inavyoonyesha kihalisia.  Kila anayeshika madaraka ikiwa atalazimika kuondoka madarakani ataweka mazingira ambayo kama ataondoka basi nafasi yake ishikwe na angalau na mtoto wake, mifano ya hao tunayo mengi. &lt;br /&gt;Tumeshuhudia katika nchi nyingi za Kiafrika viongozi wakiwa wanabadilisha katiba, za nchi ilimradi tu waendelee kubaki madarakani, hata kama wananchi wameshawachoka. Mara ngapi tunasikia kwamba Rais fulani anataka kufanya mabadiliko ya katiba ili kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani.  &lt;br /&gt;Ziko katiba zinazoweka vipindi vya urais, kwa mfano Tanzania kipindi cha Rais kukaa madarakani ni miaka mitano mara mbili, hii ina maana ya kwamba baada ya miaka kumi hata kama rais huyo anapendwa vipi ni lazima akabidhi uongozi kwa mwingine.&lt;br /&gt;Uamuzi wa aina hiyo una faida zake na hasara zake, faida ni kwamba unaepusha kujenga himaya ya kifalme na kidikteta.  Hasara yake ni kwamba mara nyingine inashindikana kumaliza ajenda na miradi ambayo Rais amejiwekea kwani miaka 10 si mingi na sera nyingi ni za muda mrefu.  &lt;br /&gt;Yawezekana mtu akajenga hoja kwamba uongozi ni mchakato, hivyo wengine watakaokuja badala ya aliyeondoka watauendeleza mchakato huo.  Hiyo ni kweli na ndivyo inavyopaswa iwe, lakini si lazima kwa kiongozi mpya kuendeleza sera na mikakati iliyowekwa na uongozi uliokuwapo madarakani.  Rais mpya ana uamuzi wa kupanga mipango na mikakati mipya endapo ataona kwamba iliyopo itamkwaza.&lt;br /&gt;Kubadilika katiba  kwa nchi za Afrika ni jambo la kawaida, kwani imeshatokea mara nyingi kwa baadhi ya nchi, rais wake kubadili katiba ilimradi tu abaki kuendelea madarakani.&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa Machiaveli, kiongozi ana haki na wajibu wa kuhakikisha kwamba anaendelea kulinda madaraka yake hata ukifika muda wa kustaafu anayo haki ya kuongeza muda, kwani kutafuta kiongozi mwingine ni kazi kubwa sana.&lt;br /&gt;Pengine Machiaveli alikuwa akizungumzia ufalme zaidi kuliko uongozi ambao msingi wake ni mkuonyesha njia na endapo kiongozi akishindwa kuonyesha njia anapaswa awapishe wengine nao wajaribu kuonyesha njia.  &lt;br /&gt;Lakini kwa mantiki ya Machiaveli, ni lazima uongozi uwe endelevu.  Endelevu aliyoiainisha ni ya kung’ang’ania madaraka, kwake yeye, uongozi ni mali ya mtu, pengine amepewa na Mungu hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kumnyang’anya aliyepewa na Mungu. &lt;br /&gt;Ipo dhana nyingine ya uongozi endelevu kwa mantiki ya ‘maliberali’ na siyo ya ‘marialisti.’  Katika falsafa za kiliberali uongozi ni mali ya umma si mali ya mtu na ni lazima uwe endelevu, yaani viongozi waliopo madarakani wanapaswa kutengeneza mfumo wa kupasiana kijiti, yaani wewe ongoza kwa miaka nane mathalan, wakati ukiwa madarakani hakikisha kwamba anapatikana mtu mwingine wa kushika pale utakapoachia na pengine kuendeleza yale uliyoyapanga na kukusudia kuyafanya lakini ukashindwa pengine kutokana na muda, na hili linafanyika duniani kote.&lt;br /&gt;Lakini lipo jingine linalotia mashaka katika uongozi wa Afrika;  hivi karibuni Rais wa Rwanda, Paul Kagame alipitisha sheria ya kinga ya Rais atakayeondoka madarakani kutoshtakiwa kwa kosa lolote lile alilolitenda wakati akiwa Rais.  Hii ni ngumu kwa sababu kinga hiyo yaweza kutumika vibaya, Rais aweza kuua, kuiba/kuhamisha na hata kuangamiza kwa kujiamini kwamba hakuna chochote kitakachomkuta.  Mfumo huu ni wa Alfa na Omega, kwamba Rais ndiyo mwisho.  Dhana hii inapingana na ile dhana ya kwamba hakuna aliye juu ya sheria.  Kagame hivi sasa yuko juu ya sheria, yeye ndiye mwanzo na ndiye mwisho!&lt;br /&gt;Binafsi naungana na wale wanaofikiri kwamba kuna haja ya kubadilisha mfumo wa uongozi wa Afrika, kwani uliopo hivi sasa ni ‘mkorogovyogo’!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa gazeti la Mwananchi.&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;br /&gt;0754 849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-1734287972874526624?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/1734287972874526624/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=1734287972874526624&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1734287972874526624'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1734287972874526624'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2008/07/mfumo-wa-uongozi-na-demokrasia-afrika.html' title='Mfumo wa uongozi na demokrasia Afrika, ni mkorogovyogo!'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-3396805410958076495</id><published>2008-07-31T07:42:00.000-07:00</published><updated>2008-07-31T07:47:05.744-07:00</updated><title type='text'>Prof. Masha:Watanzania walijibu swali lisilo kuhusu Shirikisho</title><content type='html'>Na Hawra Shamte&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MBUNGE wa Bunge la Afrika Mashariki, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha United Democratic na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha St. Augustine, Profesa Fortunatus Lwanyantika Masha anasema kwamba kwa bahati mbaya au kwa kutokutambua, Kamati iliyoongozwa na Profesa Samuel Wangwe haikuweza kuwaelekeza Watanzania swali halisi walilopaswa kulijibu ambalo ni je, tuharakishe Shirikisho la Afrika Mashariki?  Badala yake, wananchi wakajibu swali la je, mnataka Shirikisho?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akizungumza katika mjadala wa wazi katika Chuo Kikuu cha St. Augustine, tawi la Dar es Salaam, Prof. Masha alisema kamati ya Wangwe iliibua maoni na hisia nyingi kuhusu kazi ya kamati yenyewe; uamuzi wa kuundwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki; na wasiwasi wa kuunda Shirikisho la nchi zinazotofautiana kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiusalama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Masha anasema pengine mkanganyiko kuhusu Shirikisho unatokana na kuwapo kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo ili kulitambua Shrikisho la Afrika Mashariki ni muhimu kutofautisha baina ya Shirikisho na Jumuiya ya Afrika Mashariki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Watu wengi hawaoni tofauti baina ya jumuiya hizo mbili, na ndiyo maana kushindwa kwa EAC kunaunganishwa moja kwa moja na Shirikisho kwamba nalo laweza kushindwa kama ilivyoshindwa Jumuiya.  Wasichokifahamu wengi ni kwamba malengo na utashi wa kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki ni tofauti na yale yaliyokuwapo wakati wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika mwaka 1977,” anasema Prof. Masha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Prof. Masha anaendelea kueleza kuwa ingawa hivi sasa ipo Jumuiya ya Afrika Mashariki na ambayo kimfumo inaweza kuwa na Umoja wa Forodha, Soko Moja na Sarafu Moja bila ya kuwa na Shirikisho la kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Dhamira ya kuwa na Shirikisho ni kuunda Taifa Moja la watu wa Afrika Mashariki.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Prof. Masha anasema katika utangulizi wa Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, inaelezwa wazi kwamba: “Nchi za Tanzania, Kenya na Uganda zimedhamiria kuimarisha mahusiano yao ya uchumi, kijamii, kiutamaduni, kisiasa, kiteknolojia na mengine, kwa maendeleo ya haraka kwa nchi zote, kwa kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki; pamoja na umoja wa forodha na soko moja, baadaye sarafu moja na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkataba wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki ulishawasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na likauridhia mwaka 2000.  “Kwa maana nyingine ni kwamba; Bunge la Tanzania pamoja na Serikali ya Tanzania wameisharidhia kuundwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki.  Kinachobakia ni mchakato wa kulifikia Shirikisho,” anaeleza Prof. Masha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Agosti 28, 2004, wakuu wa Nchi wanachama wa EAC (Summit) waliunda kamati ya kuangalia namna ya kuharakisha mchakato wa Shirikisho ili kutimiza kwa haraka kusudio la Shirikisho la Kisiasa.  Ndipo ilipoanzishwa Kamati ya Amos Wako ambayo ripoti yake ilisema kwamba kimsingi kuundwa kwa Shirikisho la Kisiasa kumekwisha anza kwani tayari miundombinu yake imeshawekwa; kuna Mahakama ya Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki pamoja na maelewano ya mahusiano katika mambo ya majeshi, usalama na sera za nchi za nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ripoti ya Wako iliweza kuainisha majukumu sita ya Shirikisho ambayo ni Ulinzi na Usalama, mambo ya Nchi za Nje, Mamlaka ya Ziwa Viktoria, Haki, Polisi na Uhamiaji, fedha na Mipango na Miundombinu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Ingawa wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hawakuazimia moja kwa moja kukubaliana na mapendekezo ya kamati ya Wako, kwa matamshi yao walifurahishwa na kazi ya Kamati hiyo.  Kwa kuwa mengi ya yaliyomo katika mikakati ya maendeleo (EAC Development Strategy 2006 – 2010) yanatokana na mapendekezo ya kamati ya Wako; kimsingi walikubaliana na programu ya kufikia Shirikisho kama ilivyopendekezwa na Kamati ya wako.”&lt;br /&gt;Utata wa kazi ya kamati ya Wangwe&lt;br /&gt;Kamati ya Wangwe ilihusika na mchakato wa Mashauriano ya Kitaifa (National Consultative Process) kuhusu kuharakisha Shirikisho la Kisiasa.  Profesa Masha anasema nia ya kushirikisha wananchi wa Afrika Mashariki katika mchakato wa kuunda Shirikisho ni nzuri, ugumu ni namna ya kuwashirikisha na hasa baada ya maamuzi ya msingi yakiwa tayari yameisha chukuliwa.  Ni taratibu zipi zitumike katika kuwashirikisha?  Washirikishwe au waamue?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Prof. masha anasema pamoja na kuwa Kamati ya Wangwe ilikuwa inaratibu/inatafuta maoni ya wananchi kuhusu swali “je, Shiriksho liharakishwe au hapana?” lakini ilikuwa na utata wa aina mbili:  Kwanza; mkanganyiko wa swali lililotakiwa kujibiwa.  Pili; namna ya kupata maoni ambayo yanafanana na maoni ya Watanzania kwa ujumla.  Yote mawili yalikuwa matatizo ya kiufundi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waliohudhuria mikutano ya Kamati ya Wangwe na wengi waliotoa maoni katika vyombo vya habari, walijibu swali tofauti, yaani: Je, tuingie katika Shirikisho au hapana?  Kwanini? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Tofauti hii kubwa kati ya swali lililoulizwa na swali lililojibiwa, ilileta mkanganyiko mkubwa,   Waliokuwa wanaelewa vema Kazi ya kamati hiyo, waliliona zoezi lililoendeshwa na Kamati ya wangwe halikuwa na maana,”&lt;br /&gt;Prof. Masha anasema.&lt;br /&gt;Prof. Masha pia anabainisha tatizo jingine kubwa katika zoezi la Kamati ya Wangwe, kwamba lilikuwa namna walivyoratibu maoni ya wananchi.  “Kwa mfano; walikwenda katika Wilaya yenye watu zaidi ya 300,000; wakapata ukumbi katika makao makuu ya Wilaya; wakafanya mkutano mmoja au miwili na kupata jumla ya watu 200.  Maoni ya hawa 200 yana uhalali gani kuchukiliwa kwamba ni maoni ya wilaya nzima? Hawa 200 wamepatikanaje hata waweze kusemea Wilaya nzima?  Anahoji Prof. Masha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, Prof. Masha anakiri kwamba jambo zuri lililotokana na mizunguko ya Kamati ya Wangwe ni kutoa mjadala katika taifa, uliosisimua kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki hata kama wanaanchi walijibu swali lisilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho Prof. Masha anatoa usahuri kuwa suala la Shirikisho ni suala la kisiasa, lenye kuhitaji maamuzi ya kisiasa.  Wanasiasa hawawezi kukwepa wajibu wao wa kaumua mambo neyti kama Shirikisho, kwa kujificha nyuma ya kamati ambazo zina utata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-3396805410958076495?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/3396805410958076495/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=3396805410958076495&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/3396805410958076495'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/3396805410958076495'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2008/07/prof-mashawatanzania-walijibu-swali.html' title='Prof. Masha:Watanzania walijibu swali lisilo kuhusu Shirikisho'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-4742107332304788383</id><published>2008-05-01T23:22:00.000-07:00</published><updated>2008-05-01T23:27:06.699-07:00</updated><title type='text'>Haya ni mapambano ambayo wapenda demokrasia na amani lazima washinde!</title><content type='html'>Salaam&lt;br /&gt;Makala hii ilitoka katika gazeti la Mwananchi la April 16, nimeona niiweke mtandaoni tufaidike wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia makubaliano ya mwafaka wa kisiasa Zanzibar kugota, baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kuagiza kwamba suala la kuwapo kwa serikali shirikishi Zanzibar lirudishwe kwa wananchi kwa kupigiwa kura ya maoni, wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini wanaona kwamba, uamuzi huo unaweza kuzidisha utata wa kisiasa Zanzibar.  Katika makala hii, mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa na haki za binadamu ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa HAROUB OTHMAN ambaye pamoja na mambo mengine anashauri kuwa viongozi wanapaswa kuhakikisha kwamba ufumbuzi wa tatizo la kisiasa Zanzibar unapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010… &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Je, uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM kulirudisha suala la ‘Mwafaka’ kwa wananchi hasa kipengele cha serikali ya mseto, wewe unauonaje? Je, unaweza kuleta suluhisho la mgogoro?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Ni jambo la busara kwa serikali kutaka wananchi wake watoe maoni/mapendekezo juu ya mambo yoyote makubwa au madogo inayotaka kufanya. Kuna nchi kama Switzerland ambapo serikali zake za mikoa (cantons) huitisha kura za maoni hata katika mambo madogo madogo. Huo ndio utamaduni waliokua nao. Sisi hapa hatuna utamaduni huo. &lt;br /&gt;Kuna mambo mazito yamefanyika nchini bila ya kura ya maoni. Mifano ni kama Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964; kuletwa mfumo wa chama kimoja mwaka 1965; Azimio la Arusha la mwaka 1967 na sheria zilizofuatia za kutaifisha mali; kuja kwa mfumo wa vyama vingi wa 1992, na kadhalika. &lt;br /&gt;Ingekuwa kumepigwa kura ya maoni mwaka 1991 na wananchi asilimia 80 wakakataa mfumo wa vyama vingi, kama vile takwimu za Tume ya Nyalali zinavyoonyesha, kwa matokeo hayo si tungekataa mfumo wa vyama vingi? Athari zake tunazijuwa? Suala gani wataulizwa wananchi katika kura hiyo ya maoni; ikiwa wanataka au hawataki serikali ya mseto. Mimi nafikiri kwamba ‘Kamati ya Mwafaka’, baada ya kutafakari matatizo yote yaliyojitokeza tangu uchaguzi wa 1995, na zile chaguzi za 2000 na 2005, wakaonelea kwamba njia ya busara ni kuwa na serikali ya mseto. &lt;br /&gt;Kama alivyosema Rais Jakaya Kikwete na Profesa Ibrahim Lipumba, kila upande katika kamati hiyo imekuwa ikishauriana na wakuu wake. Hii ni kusema kwamba Rais Kikwete, Rais Amani Karume na Profesa Lipumba wote walijua nini kimezungumzwa katika kamati hiyo na nini kimekubaliwa. &lt;br /&gt;NEC ya CCM na Baraza Kuu la CUF vyote vilikuwa vikiarifiwa nini kinatokea. Mbona wakati wote huo wazo la kura ya maoni halikuletwa? Na baada ya Rais Karume kulileta suala hilo kwa Komredi Kingunge Ngombale Mwiru, Luteni Yusuf Makamba na Ali Ameir Mohamed, ambao ni wajumbe wa ‘Kamati ya Mwafaka’, si wangerejea kwa wenzao wa upande wa CUF kuwasikiliza wana maoni gani, kabla ya jambo hilo kupelekwa kwenye Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM? &lt;br /&gt;Tafsiri iliyojitokeza sasa hivi ni kwamba CCM haitaki hata hiyo dhana ya serikali ya mseto, na kusema kuwe na kura ya maoni ni njia tu ya kistaarabu ya kukataa jambo hilo. Kwani hata utekelezaji wake ambao unataka mabadiliko ya kikatiba, kuandaa daftari la wapiga kura na uendeshwaji wa hiyo kura ya maoni sioni vipi itawezekana kufanyika na halafu tuwe na uchaguzi wa mwaka 2010. Mimi sioni kwamba kutakuwa na kura ya maoni na wala kama kweli kutakuwa na jitihada za dhati za kuiangalia upya Katiba ya Zanzibar na kubadilisha sheria ya uchaguzi na kuifuma upya Tume ya Uchaguzi ili kuhakikisha kwamba kutakuwa kweli na uchaguzi huru na wa haki. Na ikiwa hayo hayakufanyika haraka, basi itakuwa tunaelekea pabaya huku tukijua na tukiwa macho wazi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;1. Je, unadhani CCM inayo dhamira ya kweli ya kuleta maelewano ya kisiasa Zanzibar?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Tunachoweza kusema juu ya CCM ni kutokana na dhamira zake za dhahiri, katiba yake na yale ambayo viongozi wake wanayazungumza hadharani. Na ikiwa chama hicho kinataka kubaki madarakani, Bara na Visiwani, na kuendelea kupata uhalali wa kuwa chama cha siasa, basi lazima kiende na wakati na kijifunze kutokana na historia ya nchi yetu lakini pia tujifunze kutokana na yanayotokea kwa wenzetu. Mizozo, uhasama, chuki, malumbano yasiyo na mwisho, uvunjwaji wa haki za binadamu, n.k., sio vitu vinavyowaunganisha watu bali vinaigawa jamii. Na jamii iliyogawanyika haipati maendeleo. La umuhimu pia ni urithi gani ambao Rais Jakaya Kikwete na Rais Amani Karume wanataka kuwaachia Watanzania baada ya uongozi wao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;2. Wachambuzi wanasema kuwa wahafidhina wa siasa za Zanzibar wanaogopeshwa na kipengele cha mgawanyiko wa madaraka. Je, hofu yao ina mashiko?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Kwa jinsi maelezo yanavyoonyesha juu ya nini kimetokea katika Kamati Kuu na NEC ya CCM, sio suala la wahafidhina au wapenda maendeleo kushinda, lakini ni ukosefu wa uongozi. Inaonyesha katika suala hili Kamati Kuu haikwenda kwenye NEC na msimamo mmoja na kujua nini wanataka. Wachunguzi wengi wanasema kuwa mgawanyiko uliotokea haukupata kuonekana tangu mkutano mkuu wa TANU wa mwaka 1958 kule Tabora kuhusu kura tatu. Uongozi ni kuonyesha njia; na ili kufanya hivyo uongozi lazima uwe unajua wapi unataka kuwapeleka watu na kuamini kwamba utaweza kuwafikisha huko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;3. Kwa maoni yako, unadhani nini kingeanza, kura ya maoni au mazungumzo? Na je, kwani makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo hayawezi kupewa uhalali wa kisheria mpaka wananchi washiriki katika kura za maoni? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Ninavyofahamu mimi ni kwamba ile Rasimu iliyotolewa na “Kamati ya Mwafaka’ na kupelekwa kwenye vyombo vya juu vya CUF na CCM ilimaanisha kwamba mazungumzo yamemalizika na kilichohitajika ni ridhaa ya vyombo hivyo na utekelezwaji wa mapendekezo hayo. Utekelezwaji ungeweza kufanyika kwa kulitumia Baraza la Wawakilishi, na hata pale ambapo ridhaa ya thuluthi mbili ya wajumbe ingehitajika, hilo lisingekuwa gumu kwa vile jambo hilo litakuwa limekubaliwa na vyama vyote viwili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;4. Hoja nyingine inayotolewa na wanasiasa wa vyama vingine (visivyo CUF na CCM) ni kuwa mazungumzo yangeshirikisha vyama vyote vya siasa na wala si CUF na CCM pekee, wewe unaonaje hoja hiyo?   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Ni hoja sahihi kabisa. Na si vyama vya kisiasa, bali pia asasi zisizokuwa za kiserikali, jumuiya za kidini, vyama vya kitaalamu, watu mashuhuri katika jamii, n.k. Kwani kinachotafutwa ni mustakabali wa taifa zima na kila mmoja ni mdau katika hilo. Lakini hili lingekuja katika awamu ya pili. Kuna mambo yaliyokubaliwa katika Mwafaka I na II ambayo hayakutekelezwa; kuna yale yaliyojitokeza katika uchaguzi wa mwaka 2005 ambapo ilipelekea CUF kusema hawamtambui Rais Amani Karume, na mengineyo. Sasa haya ni ya CUF na CCM. Matumaini yangu mimi ni kwamba ikiwa mwafaka utafikiwa, utatoa fursa ya kuwa na mjadala mpana zaidi na wa kitaifa kuhusu mustakabali wa taifa; na hapo kila chama, jumuiya, taaluma, n.k., ingebidi vishirikishwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;5. Je, uamuzi wa CUF kujitowa katika mazungumzo ya Mwafaka ni sahihi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Bila ya shaka CUF ina sababu zake za kufanya hivyo. Rasimu ile iliyokubaliwa na Kamati ya Mwafaka imejengeka kwenye msingi kwamba kurekebishwa kwa katiba, kufumwa upya kwa Tume ya Uchaguzi, kufanyiwa marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kutengeneza mazingira ya kuwapo kwa uchaguzi wa haki na huru, vitafanyika kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010; na chombo kitakachosimamia haya ni serikali ya mseto. Sasa kwa CCM kuleta jambo jipya la kura ya maoni na kutamka wazi kwamba kwa maoni yake serikali ya mseto itakuja baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 imekuwa kwamba ule msingi wa makubaliano yale haupo tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;6. Pamoja na kususia mazungumzo, unadhani CUF inaweza kuchukuwa hatua gani zaidi katika kukabiliana na usanii wa kisiasa wa CCM?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Huu sio usanii, ni mbinu za kisiasa. Utakumbuka katika taarifa iliyotolewa na Makamba, Ngombale na Ali Ameir kwenye Kamati Kuu ya CCM walizungumzia kwamba kuleta kura ya maoni ni njia ya ‘kuipiku’ CUF! Kutopatikana kwa suluhisho la kudumu sio kwamba inaiumiza Zanzibar tu lakini athari zake zinafika Bara pia. Tumeona vipi tatizo hili la Zanzibar lilivyochukuwa mjadala mkubwa na mrefu kwenye vikao vya CCM huko Butiama. Ikiwa tutafikia uchaguzi wa mwaka 2010 bila ya tatizo hili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu, nachelea kufikiri nini kitatokea. Hiki si kitisho bali ni baada ya kuangalia nini kinatokea nchini na kuona pia vipi mambo yanavyokwenda ulimwenguni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt; 8. Maalim Seif aliripotiwa kuwa alikwenda Uingereza na nchi za Scandinavia kuwashawishi waingilie kati suala la Mwafaka. Je, hatua hiyo aliyoichukuwa ni sahihi? Kama ni sahihi, je unadhani nchi hizo wahisani zinaweza kufanya nini katika kufikia hatima ya mgogoro wa kisiasa Zanzibar? &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;JIBU: Sijui Maalim Seif alikwenda wapi na kufanya nini. Lakini ninachojua ni kwamba jumuiya ya mabalozi wa kigeni hapa nchini imekuwa ikifuatilia kwa karibu mazungumzo yaliyokuwa yakifanyika baina ya CCM na CUF, na wengi wao wamesikitishwa na yaliyotokea. Nini watashauri serikali zao sijui, lakini matamshi aliyotoa Balozi wa Marekani hivi karibuni yanaashiria kwamba mambo hayatokuwa shwari si kwa Zanzibar tu bali kwa Tanzania kwa ujumla. Seif Shariff kokote atakakokwenda atasikilizwa lakini sidhani kwamba siasa za nchi hizo kwa Tanzania zitategemea nini Seif anataka bali hali halisi ilivyo nchini na maslahi ya nchi hizo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;9. Unazitathmini vipi jitihada za Rais Jakaya Kikwete katika kuondosha mpasuko wa kisiasa Zanzibar?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Rais Jakaya Kikwete alitamka azma yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar alipohutubia Bunge kwa mara ya kwanza kama Rais mwezi Desemba 2005. Viongozi wengi wa kiafrika hawana utamaduni wa kujali vipi historia itawasema na kuwahukumu katika kipindi cha utawala wao au wanataka kuwacha urithi upi ambao ukumbukwe wa utawala wao. Kuweza kulitanzuwa tatizo hili la Zanzibar sio tu kutampa Rais Kikwete na Rais Karume heshima zaidi nchini na kimataifa lakini pia itakuwa wamewacha urithi mzuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;10. Nini maoni yako kuhusu hisia za Wapemba kwamba wanataka waachiwe kisiwa chao na waunde serikali yao? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JIBU: Kwa upande mmoja naweza kufahamu kwanini hisia kama hizo zinaibuka sasa, lakini kwa kweli ni mawazo ya hatari kwa taifa letu. Ni kitu ambacho Mwalimu Nyerere alituonya kabla. Leo Wapemba wanaweza kujiona kuwa ni kitu kimoja dhidi ya Waunguja, lakini kesho itakuwa ni wale kutoka Ziwani, Kengeja, Wete au Kisiwa Panzi. Hoja sio kujitenga bali kujitahidi kujenga demokrasia ya kweli ambapo kila mmoja atakuwa na hisa katika upanuwaji wake, kuenziwa kwake na kudumishwa kwake. Haya ni mapambano ambayo wapenda demokrasia na amani lazima washinde!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-4742107332304788383?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/4742107332304788383/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=4742107332304788383&amp;isPopup=true' title='14 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/4742107332304788383'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/4742107332304788383'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2008/05/haya-ni-mapambano-ambayo-wapenda.html' title='Haya ni mapambano ambayo wapenda demokrasia na amani lazima washinde!'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>14</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-1664329151483150078</id><published>2007-12-05T04:11:00.000-08:00</published><updated>2007-12-05T04:18:57.052-08:00</updated><title type='text'>Rais anza kazi, nasi tutakusaidia kukomesha ufisadi huu</title><content type='html'>KUKEMEA au kukaripia kwa kawaida ni tabia ya wakubwa, wenye mamlaka, wawe katika ngazi ya kaya, tarafa, kijiji, wilaya, mkoa hadi taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais anapo kemea au anapo onya huwa anafanya wajibu wake, anafikiri kwamba kwa kufanya hivyo kuna watu watamsikiliza kwa sababu karipio la Rais ni amri ya katazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanaofuatilia historia ya nchi hii watagundua kuwa ni katika awamu ya kwanza tu ya serikali zote mbili (ile ya Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Karume), ndipo makemeo na makaripio yalipokuwa yakifanya kazi zake ipasavyo.  Linapotamkwa tu, hutekelezwa, hadi ikafikia watu kukamatwa na kuwekwa jela kwa kosa la uhujumu wa uchumi wakati hata hiyo sheria ya uhujumu wa uchumi ikiwa bado haijatungwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati ule Watanzania bado walikuwa waoga, walikuwa wanagenzi, ndio kwanza wanajifunza, walizoea kutawaliwa na kuamriwa.  Hizo zilikuwa ndio zama za ‘zidumu fikra za Mwenyekiti.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika zama hizi, mambo yamebadilika, watu hawashtushwi tena na makemeo, makaripio na maonyo.  Kauli za kisiasa kwao si tatizo, kwani si wamezoea kuzisikia?  Je kwani huo si sawa na wimbo wa taifa, hata mtu akiwa usingizini akili yake inauimba?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Jakaya Kikwete akiwa mkoani Pwani mwishoni mwa wiki iliyopita, alitoa tahadhari kwa viongozi wanaojigawia miradi ya wananchi maskini kuwa wasipoacha tabia hiyo watakiona cha mtema kuni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alipokuwa mkoani Tabora wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, Rais pia alitumia fursa hiyo kutoa onyo, aliwakemea wanaoeneza virusi vya ukimwi kwa makusudi kuwa watakiona cha moto.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais aliwahi kutoa tahadhari kwa wala rushwa na kuwaambia kuwa majina yao anayo ila anawapa muda wajirekebishe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kanuni za uongozi hasa wa nchi, mara nyingine si vizuri sana kufikiri kwamba unaweza kuibadilisha jamii kwa kutoa tahadhari, onyo, karipio au kemeo.  Mara nyingine uongozi unahitaji vitendo zaidi kuliko maneno. Kama Rais alivyowahi kusema kuwa kelele za wapinzani amezizoea, hivyo naye anapaswa ajihadhari ili ‘kelele’ zake nazo zisije zikazoeleka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mambo ambayo viongozi wanapaswa wayatende bila kusema, wanaweza kumuadhibu mtu kwa kosa la uhujumu uchumi au kuhujumu miradi, kimya kimya na ujumbe ukafika.  Binafsi naona si vema kwa Rais kupenda kutoa maonyo majukwaani kwani tunachoshindwa Watanzania ni kufanya kweli na kamwe si kusema.        &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna maonyo na maelekezo yaliyotolewa Ngurdoto kwa viongozi wa Serikali, kwa kiasi gani maonyo yale yameleta athari?  Je maelekezo yale waliyoyapata viongozi wetu katika semina elekezi hayakuweza kubadilisha muundo na mtindo wa uongozi serikalini?  Je ni kwa kiasi gani Serikali hii imekwenda kwa wananchi na imekuwa kweli Serikali ya watu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo alilolizungumza Rais ni dhahir, nami nachukua nafasi hii kumuunga mkono.  Si vibaya kutoa tahadhari na karipio lakini isiwe ndiyo mazoea. Hili la viongozi kujipendelea, angalau Rais ameligundua na nashukuru amelizungumzia.  Je ni miradi mingapi ambayo walengwa wake ni wananchi wa kipato cha chini ambayo huchukuliwa na wakubwa?  Rais amezungumzia mradi wa ugawaji wa miche ya miembe inayozaa kwa muda mfupi, lakini pia upo mradi wa usambazaji mbolea kwa wakulima, je ni wakulima wangapi wadogo wanaofaidika na mbolea hiyo?  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mradi wa upimaji viwanja katika maeneo mapya, je ni wananchi wangapi walalahoi wanaovipata viwanja hivyo?  Je hatuwaoni wakubwa jinsi wanavyojikatia eka kwa eka, eti ardhi ni mali hivyo wanaweka akiba?  Je hawa ‘pangupakavu’ wanawezeshwa vipi nao kujipatia angalau ekari moja moja ya akiba?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna nafasi za masomo zinazotolewa kwa ajili ya watoto wa wakulima na wafanyakazi, wavuja jasho wa nchi hii, je ni watoto wa wavuja jasho wangapi wanaopata fursa hizo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu iliyokusudiwa kwa ajili ya wanafunzi ambao wazazi wao hawana uwezo, je ni watoto wa vigogo na matajiri wangapi wanaopata mikopo hii ambayo hawastahili kuipata?  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ipo miradi ya Tasaf na Mkukuta, je viongozi wanajilinda vipi na ulafi na uchoyo ili miradi hiyo iwafikie walengwa? Ni vipi Tanzania itatimiza malengo ya millennia ya kupunguza umaskini uliokithiri wa asilimia 50 ya wananchi wake, ikiwa kumbe wapo viongozi walafi, waroho, wanaojilimbikizia na kupora miradi ya wananchi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna miradi ya usambazaji maji, katika hili nalo wako wahujumu wanaounganisha mabomba katikati ya bomba kubwa la usambazaji na kuyavuta kwa ‘pump’ hivyo kusababisha wengine kuyakosa, je hawa nao wanachukuliwa hatua gani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais unapaswa upange mikakati madhubuti ya kuwachukulia hatua kali hawa wasiopeleka miradi kwa walengwa na badala yake kujinufaisha wao binafsi kutokana na nafasi walizonazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukisikia ufisadi, huu wa kiongozi kuwa ‘mwamba ngoma, ngozi kuvutia kwake,’ ndio ufisadi mkubwa.  Rais anza kazi, nasi tuko nyuma yako, tutakusaidia kukomesha ufisadi huu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi ni Mhariri wa Siasa wa gazeti la Mwananchi.&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-1664329151483150078?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/1664329151483150078/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=1664329151483150078&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1664329151483150078'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/1664329151483150078'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2007/12/rais-anza-kazi-nasi-tutakusaidia.html' title='Rais anza kazi, nasi tutakusaidia kukomesha ufisadi huu'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-2044066180951625484</id><published>2007-11-28T00:58:00.000-08:00</published><updated>2007-11-28T01:00:12.679-08:00</updated><title type='text'>Adui yako muombee njaa, akikosea kidogo kandamiza!</title><content type='html'>WALIOSEMA siasa ni mchezo mchafu, leo nami naungana nao kuyaamini maneno yao.  Kweli siasa ni mchezo mchafu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa daima hubuni stratejia mpya za kujipatia maslahi ya kisiasa, mbinu, mikakati iliyopo katika siasa hasa za ushindani ni jinsi gani chama kimoja kitakavyokigaragaza kingine katika medani za kisiasa, iwe ni kwa majigambo, majibizano, kashfa na hata kubadilisha mwelekeo wa duru za siasa za wakati husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kawaida katika vyama huwa na idara na maofisa maalum wa propaganda, hawa ni makuhani wa propaganda, wamekubuhu, waweza kukushawishi kwamba hivi sasa ni usiku ilhali ni mchana, kisa kuna wingu limetanda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Propaganda ni utaalamu ambao kwa Tanzania, kinara wake ni Chama Cha Mapinduzi hawa wana ujuzi wa kutosha katika masuala ya propaganda na ujuzi huo si wa kubabaisha, una mashiko ya Urusi na Quba mabingwa wa propaganda za kijamaa duniani.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Chochote kinachotendeka katika medani za siasa hakishangazi, na ndiyo maana sikushangaa kumsikia Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Taifa, Jakaya Kikwete alipokuwa akifungua tawi la CCM litakalowahudumia wanachama takriban 700 ambao ni wanafunzi wa vyuo vikuu vya Kampala na Makerere, mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa, “hali ya kisiasa nchini ni shwari, hizo kelele kelele wanazozisikia ndio siasa, hivyo zisiwape shaka, adui yako muombee njaa, akikosea tu, kandamiza hapo hapo, si mnasikia tunavyokandamiza...”  Sehemu ya hafla hiyo kwa bahati ilionyeshwa na Televisheni ya Taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe, hivi vilio vinavyotolewa na wananchi na wanasiasa kuhusu Buzwagi, Richmond na vinginevyo ni ‘kelele kelele’ tu za kisiasa?  Kelele ambazo si hasha kutomzuia mwenye nyumba kulala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je ni vipi tutaidadavua kauli hii ya Mwenyekiti wa Chama Dola nchini?  Je anataka kutueleza nini hasa?  Kelele zinazopigwa siku za hivi karibuni ni suala la kuchunguzwa mikataba inayoingiwa na Serikali kama ile ya madini na ile ya nishati ya umeme.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbunge kijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliamsha hamasa mpya pale alipoliomba Bunge liunde kamati huru ya kuchunguza uingiaji wa mkataba wa machimbo ya madini katika mgodi wa Buzwagi.  Yaliyotokea kwa Zitto ni historia, lakini nini baadaye Rais alifanya?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alimteua Zitto kuwa mjumbe wa Kamati ya Madini.  Waswahili wana msemo usemao kuwa ‘mchawi mpe mtoto alee,’ msemo huo ukasadifu kwa Zitto kupewa kazi ya muda ya kulea mtoto, ni mjumbe wa Kamati ya Madini, alichotaka Zitto kukitoa kikoa, sasa hakitoleki tena, akijaribu tu ni yeye ndiye atakayepelekwa ‘msukule.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapigo ya CCM si ya kitoto, ni ya kisayansi, hawakurupuki bali hufanya hesabu na mara nyingi jawabu zake huwa sahihi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala ya watu kujadili jinsi mikataba ya madini isiyolinufaisha taifa inavyoingiwa, sasa wanamjadili Zitto, kwanini wee, kwanini.  Kwani vipi jamani?  Kwani wao wananchi wanataka iwe vipi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingelikuwa Rais hakuiteua kamati ile kwa jinsi alivyoiteua angelaumiwa, ameiteua walioteuliwa wanalaumiwa, kwani jamani Zitto kosa lake nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wako waliozikaanga mbuyu, sasa wanawaachia wenye meno watafune.  Huo ndio mchezo wa siasa, hautabiriki, haufahamiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya Rais huyu huyu, wiki tatu zilizopita alilikoroga togwa, alisema kuwa suala la Mahakama ya Kadhi si sera ya CCM wala msimamo wa Serikali yake, tena Rais kenda kuyazungumzia hayo kwenye jukwaa la Kanisa, wakati wa kumsimika Mkuu mpya wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Alex Malasusa.  Jambo hilo liliwakera Waislam, walikereka hasa kutokana na hadhira aliyoitumia Rais kuwasilisha ujumbe huo mzito, unaowahusu Waislam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi sidhani kama Rais aliyafanya hayo kibubusa, bila shaka alikuwa na sababu zake maridhawa.  Lakini nisichokitambua ni kuwa je ile nayo ni siasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuwa siasa ni uongo na mchezo mchafu, yawezekana ahadi ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi ni ahadi ya uongo wa kisiasa, tuliisikia ikitolewa katika majukwaa ya kisiasa wakati wa kampeni za mwaka 2005, ahadi hiyo hiyo ambayo leo twaambiwa kuwa si sera ya CCM ndiyo iliyotumika kumnadi mgombea wa Urais wa CCM mwaka 2005, tena ilikuwa ikisisitizwa sana katika maeneo yenye Waislam wengi.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vipi ahadi ile iliingia katika ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005, wananchi hawana shida ya kufahamu ila wanafahamu kwamba ipo na kama ilivyo kwa ahadi nyingine zote zilizotolewa wakati wa Kampeni ama zile zilizoingizwa katika ilani, wananchi wangependa ahadi hiyo itekelezwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama haiwezekani waelezwe mazingira yaliyosababisha kushindwa kuitekeleza ahadi hiyo, lakini kuwaambia wananchi kuwa hiyo si sera ya CCM wala ya Serikali ni kuwacheza shere Wapigakura.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mtindo huu wa Rais, nadhani hizo alizoziita kelele za kisiasa zitaendelea kupigwa kila uchao na kwa uchache wangu wa nadhari, nafikiri kelele hizi si nzuri, si za afya katika siasa na iko siku Rais zitamgharimu.&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-2044066180951625484?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/2044066180951625484/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=2044066180951625484&amp;isPopup=true' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2044066180951625484'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/2044066180951625484'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2007/11/adui-yako-muombee-njaa-akikosea-kidogo.html' title='Adui yako muombee njaa, akikosea kidogo kandamiza!'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-8552904709672774768</id><published>2007-11-27T23:33:00.000-08:00</published><updated>2007-11-28T00:58:11.496-08:00</updated><title type='text'>Hayawi hayawi, yamekua.</title><content type='html'>Comrades&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu n i uchambuzi uliotoka Nov 3 kwenye gazeti la Mwananchi, lakini kwa vile kuna wana blog walioniomba niupandishe wavuni, ndio kwanza leo napata nafasi ya kuupandisha, bcs nilikuwa na matatizo ya kifamilia kidogo.&lt;br /&gt;Nawatakia kila la heri na naomba muudadavue, si huu tu na mingine mingi ambayo nitajitahidi kuwaletea kila mara.&lt;br /&gt;Wasalaam&lt;br /&gt;Mnyongemnyongeni lakini haki yake mpeni&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila la heri CCM, tunatarajia mabadiliko ya kimaendeleo&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;HAYAWI hayawi, leo yanakuwa, ile siku waliyokuwa wakiisubiri kwa hamu leo imefika.  Si ya ndirimo na vifijo pekee, bali pia ya wasiwasi na huzuni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ifikapo kesho, mbivu na mbichi itakuwa imejulikana.  Wako watakaofurahi na wako watakaotamani ardhi ipasuke, wajifukie.  Lakini yote hayo ni maisha, kuna kupata na kukosa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Masikio ya Watanzania wote leo na kesho yameelekezwa Dodoma, yanataka kusikia kinachojiri.  Hayo yanatokea kwa sababu kubwa moja, Chama kinachofanya uchaguzi wake wa ngazi za juu za uongozi, ni Chama Dola, utake usitake kitakugusa kwa sababu Serikali inatekeleza sera za Chama Cha Mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuvunda kwa uongozi ndani ya CCM ni kuvunda kwa Serikali.  Tunatarajia kuwa wana-CCM watatuchagulia viongozi bora, makini na ambao kweli wanayo ari, nguvu na kasi ya kuwafikisha Watanzania kwenye nchi ya ahadi, watakakokwenda kula Manna na Sal-wa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamesema wasemao kuwa Chama fisadi, huzaa Serikali fisadi.  Kete za Watanzania zimelala kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, je ataweza kubadilisha mwelekeo wa Chama?  Je Kikwete ataweza kukinusuru Chama na ufisadi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote hayo yanategemea sana timu itakayochaguliwa na Mkutano huu mkuu, sambamba na uteuzi wa atakaowateua Mwenyekiti.  Tunawaomba watuletee watu safi!  Wenzetu, watakaojali maslahi yetu.  Chonde chonde, wajumbe msituangushe!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napenda kuungana na wale wasemao kuwa pengine tatizo lililopo katika utekelezaji wa sera za CCM ni timu iliyopo, si msaada kwa Mwenyekiti.  Mwenyekiti anahitaji kushauriwa na si kuogopwa.  Anapaswa apewe mrejesho-nyuma kuhusu maoni ya wananchi, huyu hastahili kudanganywa, anapodanganywa maana yake ni kuwa wanaodanganya, wanawadanganya wananchi.  Huyu ni mwakilishi wa wananchi, wamemkasimia madaraka yao, awasimamie mustakabali wao na wa nchi yao.  Mambo yakienda shaghala-baghala, wanaokomolewa ni wananchi na kamwe si Rais na Mwenyekiti wa Chama Dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara nyingine tena, wana-CCM tunawaomba mtuchagulie watu makini, wenye uchungu na nchi hii, tunaomba mtupe watu watakaomsaidia Mwenyekiti.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunafahamu kwamba kibarua kilichoko mbele yenu, si haba, lakini tunawasihi kwamba mnapotoa maamuzi yenu yasiwe ni yale yaliyoshawishiwa na ‘vipeperushwa.’  Vifanyieni kazi vipeperushi na mtuchagulie viongozi bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inashangaza kuona kwamba watu wanakimbilia mzigo wa dhamana, je hawauogopi?  Au kipo wanachonufaika nacho?  Ikiwa dhamana ina faida, tunaomba tugawane sote, sote tunufaike na rasilimali za nchi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadhalika tunawaomba wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, kusaidia kuweka mwelekeo wa Chama, kwani wako wanaosema kuwa CCM imepoteza mwelekeo.  Wako wanaosema kuwa slogani ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya si dira ya Chama, bali ni slogani tu kama ilivyo ile ya ‘Maisha Bora kwa kila Mtanzania.’  Hizo slogani zinafaa kuwekewa mikakati ili ziwe dira, kama ilivyokuwa wakati wa sera za ujamaa na kujitegemea.  Mwelekeo wa CCM ulikuwa ni kuwatetea wanyonge, wakulima na wafanyakazi.  Mweleko huo uko wapi sasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taswira ya CCM ya leo, haionyeshi mwelekeo huo adhimu, leo hii Chama kimejitoa kutoka cha kutetea haki za wanyonge na sasa kimekuwa ni cha kutetea hali za ‘kundi maslahi.’  Hoja yangu si kutokuchagua matajiri, bali ni kuwa na watu wanaothamini shabaha ya kuundwa kwa CCM.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sisi wananchi tumechoshwa na CCM ya ‘Chukua Chako Mapema,’ tunataka kuona Mapinduzi ya kimaendeleo, CCM isaidie kututoa kutoka katika hali duni na kutufikisha katika hali bora.  Tunatarajia CCM itufikishe katika nchi ya ahadi, yenye matunda na mafanikio tele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, si kweli kwamba hohehahe leo ni vigumu kupata uongozi ndani ya CCM?  Je yawezekana kweli kupata kura, bila ya wewe kutoa kula kwanza?  Takukuru mna kazi, kwani hongo hutolewa gizani!  Wapi mtawaona, wapi mtawakamata?  Wale mnaofanikiwa kuwakamata mnawakamata kama kafara tu, na nina wasiwasi kwamba mnahangaika kukamata vibua wakati mapapa yamejizamisha katika bahari kuu!  Kama wao wanapiga mbizi, nanyi mnapaswa mzamie mbizi na kama wao wanapiga kasia, nanyi tumieni kasia ili mwende kasi inayostahili, muwafikie na muwakamate.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho naomba nitoe kisa kimoja ambacho kina mazingatio, kisa hiki napenda kukitoa kama zawadi maalum kwa Mwenyekiti wa CCM.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Nabii Ibrahim siku moja aliamua kumtembelea mwanawe Ismail, kule jangwani alikomwacha na mama yake Haajirah.  Alipofika hakumkuta Ismail alikuwa kaenda kuwinda, safari hiyo kwa kawaida ilikuwa ikimchukua zaidi ya mwezi, lakini kwa bahati Nabii Ibrahim alimkuta mka-mwana wake, baada tu ya kumkaribisha bila ya hata kumtambua mgeni yule ni nani, mkewe Ismail akaanza kuelezea matatizo yanayowakumba katika kijiji kile, ooh!  Hapa tuna shida ya maji, kitoweo mpaka tuhangaike…  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nabii Ibrahim alikaa pale kwa mwanawe siku alizokaa, alipoondoka akaacha maagizo; ‘Akija mumeo, mwambie nyumba yake nzima, lakini kizingiti chake kibovu!’  Ismail alipopata ujumbe ule akamwambia mkewe kuwa, huyo ni baba yangu, amenipa maagizo kwamba mke niliyenaye hafai, hivyo nakuacha!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwako Mwenyekiti; Nyumba yako ni nzima, lakini kizingiti chako kibovu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa Gazeti la Mwananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;br /&gt;0754 849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-8552904709672774768?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/8552904709672774768/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=8552904709672774768&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/8552904709672774768'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/8552904709672774768'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2007/11/hayawi-hayawi-yamekua.html' title='Hayawi hayawi, yamekua.'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-3822512935073871919</id><published>2007-10-25T05:54:00.000-07:00</published><updated>2007-10-25T05:55:52.230-07:00</updated><title type='text'>Je taifa lisilo na miiko, sera wala dira ni taifa hai?</title><content type='html'>Na Hawra Shamte&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;KUNA watu ambao wamejaaliwa, wamejaaliwa vipawa na maono, au labda niseme wana fikra pevu, fikra zao hufanya kazi katika zama tofauti tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu hao wana uwezo mkubwa wa kufikiri, kutafakuri na hata kuyajadili mambo, wana uwezo wa kudadavua.  Hao ndio wanaoitwa ‘wanafalsafa’ hawa ni kama akina Machiavelli, John Stuart Mill, W. Rostow na wengineo wengi kutoka katika dunia iliyoendelea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kwa bahati hata katika ulimwengu wa tatu, wako watu ‘vichwa’ wenye uwezo mkubwa wa kufikiri na katika orodha ya watu hao, baba wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere ni mmoja wao.  Fikra zake bado ziko hai kama alivyosema Steven Bhiko, mwanaharakati wa kupigania haki za weusi wa Afrika Kusini katika miaka ya 60.  Bhiko alisema ni bora kuwa na fikra hai kuliko fikra mfu kwani ni bora kiwiliwili kinachokufa kuliko fikira iliyokufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Angalau twaweza kusema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi iliyojaaliwa kuwa na watu wenye fikra hai, mmoja wapo ni hayati Mwalimu Julius Nyerere.  Kilichokufa ni kiwiliwili tu, fikra na busara zake bado zipo na zitadumu milele kwani vitabu vya historia vitawakumbusha wanadamu zama hadi zama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania tukipata nafasi tuzichambue na tuzitafakari fikira mbalimbali za Mwalimu Nyerere.  Mwalimu Nyerere alikuwa muwazi na mkweli, alikemea rushwa na ufisadi kwa dhati na alisema kuwa kiongozi ni lazima aonyeshe kuichukia rushwa kwa dhati, kinyume cha hivyo huyo si kiongozi anayeifaa Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inasikitisha sana leo hii, kuona viongozi wakiwatetea wala rushwa, wakikemea rushwa midomoni wakati maneno yao hayaonyeshi taathira yake katika vitendo.  Zama za Mwalimu Nyerere na Edward Moringe Sokoine tuliwaona wahujumu uchumi jinsi walivyoadhirika.  Waliopenda kujilimbikizia mali walifanya hivyo kwa tahadhari kubwa, kwani wakigundulika, taadhira uwanjani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii viongozi wanaona fahari kuwa na mali isiyohesabika wala kutajika, wanaona raha kuambiwa kwamba wao ni matajiri/mabepari, na baya zaidi hakuna hata anayethubutu kuwanyooshea vidole au angalau kuwauliza mali hii mumeipata wapi.  Watu wanaishi raha mustarehe wala nadhari haziwasuti kwamba kuna wenzao wanaoshinda na kulalia kipande cha muhogo wa kuchemsha kwani hata kile kipande cha nguru cha hela tano hakipatikani tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Mwalimu alipoweka miiko na maadili ya uongozi aliona mbali, na hilo alilizungumza hadharani kwamba taifa lisilo na miiko na maadili ni taifa mfu.  Haiwezekani binadamu kumwachia uhuru usio na mipaka, awe na uhuru wa kuamua, awe na uhuru wa kuchukua na awe na uhuru wa kung’ang’ania na hata kuiba.  Ni lazima uhuru uwe na mipaka, kwamba tunakupa dhamana ya kuongoza lakini ni mwiko kumiliki mali, ni mwiko kuwa na nyumba za kupangisha, ni mwiko kuwa na mishahara miwili, ni mwiko…&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa yawezekana katika zama hizi za ujasiriamali miiko hiyo imepitwa na wakati, sasa viongozi wetu wanaruhusiwa kufanya biashara na kuwa na mitaji mikubwa mikubwa, lakini je ni wapi tunapiga mstari baina ya mali ya umma na mali ya kiongozi binafsi?  Ni vipi tunamzuia kuchota katika hazina ya taifa?  Au ni vipi tunamdhibiti asiingie mikataba inayonuka rushwa?  Hili ni vigumu kulidhibiti kama hakuna miiko inayoeleweka.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uongozi usiokuwa na miiko si uongozi wa kidemokrasia, huo ni utawala wa kifalme na ndiyo maana leo hii tunashuhudia familia zinaingia katika safu za uongozi.  Baba ni kiongozi wa ngazi fulani, mama ni kiongozi wa ngazi ya chini yake na hata watoto nao wanakimbilia kupanda ngazi za uongozi.  Hali hii tukiiruhusu kuna siku tutajikuta tumejenga himaya ya kifalme, badala ya kwenda mbele, tunarudi nyuma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna miiko, hakuna dira wala mwelekeo, mwenye nguvu mpishe.  Tuliambiwa ukimuona mtu anakimbilia madaraka muogope, kwani madaraka ni dhamana nzito isiyopaswa kukimbiliwa, kwani jamani ‘Ikulu’ kuna biashara gani?  Katika mantiki haya Ikulu yaweza tu kuwa ni nembo ya uongozi, lakini kukimbilia madaraka katika ngazi yoyote ya uongozi ni jambo lisiloingia akilini kwa mtu anayefahamu uzito wa madaraka, ni sawa na mzigo mzito anaotwisha mtu kichwani kwake ambao huchosha mabega yake na hata miguu yake, akiutua hushukuru, kwani huwa ametolewa mbali!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiongozi anapaswa akose amani watu wake wanapolala njaa, kichwa kimzunguke anaposikia mashakil yanayowakabili watu wake, akose usingizi kwa kufikiria jinsi ya kutatua matatizo ya watu wake?  Wakati wenzake wanakaa vitini, yeye kiti hakimuweki, lazima azunguke ofisi na kukuna kichwa.  Yote haya si mambo ya kuyakimbilia kwa mtu anayefahamu uzito wa dhamana ya uongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Angalia Tanzania yetu ya leo jinsi watu wanavyolilia kupata uongozi wa umma kwa njia yoyote ile, wako tayari kutoa vyao, ikibidi vyote kwa imani ya kuwa miaka mitano ya uongozi atavirudisha na ziada atapata.  Huo kwa kweli si uongozi wa umma, Watanzania tunapaswa twende tukaichote ile hazina ya busara aliyotuachia baba wa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukisema tunajiuliza wapi tunapokosea, tutajikuta hatujawahi kupatia kitu, sasa na tujiulize ni njia ipi sahihi ya kuifuata?  Je taifa lisilo na dira na mwelekeo ni taifa hai?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa Gazeti la Mwananchi.&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;br /&gt;0754 849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-3822512935073871919?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/3822512935073871919/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=3822512935073871919&amp;isPopup=true' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/3822512935073871919'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/3822512935073871919'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2007/10/je-taifa-lisilo-na-miiko-sera-wala-dira.html' title='Je taifa lisilo na miiko, sera wala dira ni taifa hai?'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-7975080133538013048</id><published>2007-10-09T23:41:00.000-07:00</published><updated>2007-10-09T23:47:49.284-07:00</updated><title type='text'>Kama Rais haelewi, nasi pia hatuelewi</title><content type='html'>Rais haelewi kwanini Tanzania bado ni masikini, nasi pia hatuelewi&lt;br /&gt;Na Hawra Shamte&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;RAIS Jakaya Kikwete wiki iliyopita alipokuwa nchini Ufaransa aliulizwa na waandishi wa habari kwanini Tanzania inashindwa kujinasua kutoka katika lindi la umasikini?  Rais alijibu kwa kweli hata yeye haelewi ni kwanini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais anayo haki ya kujibu hivyo alivyojibu kwa sababu ni vigumu kuidadavua sababu hasa inayopelekea Tanzania iendelee kuwa masikini.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania ni nchi iliyobarikiwa utajiri na rasilimali za kila aina, mito itiririshayo maji, maziwa yanayosaidia katika uzalishaji wa umeme, bahari yenye samaki an-wai, milima, mabonde yenye rutuba ya kilimo, ardhi yenye madini, almasi, dhahabu, uranium, tanzanite, ruby na kadhalika. Misitu yenye wanyama wa kila aina, pamoja na yote hayo Tanzania imejaaliwa kuwa na hali ya hewa nzuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania imebahatika si miongoni mwa nchi zinazopata majanga ya asili mara kwa mara.  Kwa kuwa Tanzania iko chini ya mstari wa Ikweta hivyo ni nchi yenye joto, lakini joto lake si la kutisha, kuna maeneo nchini ambayo katika kipindi kirefu hupata baridi lakini pia baridi yake si ya hatari.  Hivyo hali ya hewa ya Tanzania ni ya wastani.  Kwa kweli Tanzania imebarikiwa, sasa kwanini ni miongoni mwa nchi maskini sana duniani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema kuwa ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania ina watu zaidi ya milioni 36, hivyo haina tatizo la watu.  Tanzania ina ardhi yenye kilomita za mraba 945,000 hivyo haina uhaba wa ardhi, tena sehemu kubwa ya ardhi hiyo ina rutuba, katika hizo kilomita za mraba 62,000 ni maeneo yenye maji.  Hivyo katika orodha ya Mwalimu Nyerere kumesalia vitu viwili, ambayo ni siasa safi na uongozi bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je Tanzania tunayo siasa safi?  Wakati wa zama za Ujamaa na Kujitegemea, Tanzania ilieleweka itikadi yake, hivyo hata siasa zake zilikuwa zina mrengo unaoeleweka.  Katika zama hizi za utandawazi, Tanzania haina tena mwelekeo, haina dira, haina siasa inayoisimamia, haieleweki kama ni nchi ya kiliberali au ya kijamaa.  Tanzania imekuwa bendera inafuata mvumo.  Mvumo uliopo sasa ni soko huria, nayo ikafungua milango yake ya soko, lakini kwa bahati mbaya Tanzania haijaweza kuifungua milango ya masoko ya nchi tajiri ili nako iende ikapeleke bidhaa zake huko.  Kwa ufupi suala la ‘siasa safi’ ni suala linalohitaji tafakuri pana.  Je Tanzania inafuata siasa gani? Je hiyo siasa iliyopo ni safi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la uongozi bora ndilo linalotia kizunguzungu zaidi.  Hapa hatupaswi kuwajadili watu bali kuijadili dhana nzima ya ‘uongozi,’ twapaswa tudadavue sifa za uongozi, je uongozi bora ni upi au uwe vipi?  Bila shaka viko vigezo tunavyoweza kuvitumia ambavyo ni uwazi, ukweli, uwajibikaji, uadilifu, busara na demokrasia.  Pengine viko vingi zaidi ya hivyo nilivyovitaja, lakini je uongozi wetu umezingatia vigezo hivyo?  Hilo ni swali la kujiuliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pengine hayo kwa kiasi fulani yanaweza kujibu lile swali la kwanini Tanzania ni masikini. Lakini pia iko dhana nyingine inayoelezwa na wasomi, kwamba Tanzania ni masikini kwa sababu Watanzania ni wavivu wa kufikiri.  Hilo mimi siwezi kulipa udadavuzi wa kina, lakini akina Profesa Mwesiga Baregu, Issa Shivji na wengineo watakuwa wanao uchambuzi mzuri kuhusu hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini je, viongozi wetu wanapoingia mikataba mibovu huku dhamira zao zikiwa kwenye asilimia 10 (10%) bila kuzingatia maslahi ya taifa kwanza, je vipi tafakuri zao huwa kwa wakati huo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tunapowakaribisha wahamishaji na tunawaita wawekezaji, huwa tunafikiri nini?  Na wakati tunapofungua milango wazi ili mitandao ya wizi iingie, nini azma yetu inakuwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Rais alipoamua kuunda Baraza la Mawaziri lenye wajumbe 61, sijui kama alifikiria kama walipa kodi wa Tanzania wataumia kuubeba mzigo wa gharama kubwa za uendeshaji Serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati viongozi wanapokwenda ziarani nchi za nje kuomba msaada wa dola milioni 400 mathalan na kisha wakafuatana na ujumbe mkubwa ambao utatumia dola milioni 200 kuugharamia, je serikali huwa imefikiria nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanapojitokeza watu wakataka kuingia madarakani kwa udi na uvumba, hadi ikabidi wanunue Wapigakura, je dhamira yao hawa huwa ni nini?  Je fikra zao zinakuwa pevu au mbichi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati kiongozi anapotamka kuwa ni lazima ndege inunuliwe hata kama ni mbovu na hata ikibidi wananchi wale majani, je mawazoni mwake huwa anachora taswira gani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati fedha za walipa kodi zinapotumiwa kwa kuwapa posho viongozi kuzunguka mikoani na wilayani kuelezea umuhimu wa bajeti, wanataka kutueleza nini?  Je kama wao hawafikiri wanadhani wananchi wanaowaongoza hawana uwezo wa kufikiri pia?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati anaposimamishwa ubunge, mbunge wa upinzani kwa sababu tu ya kutaka iundwe kamati huru ya Bunge kuchunguza mkataba wenye utata na Spika akasema kwa furaha kuwa “sauti ya Kigoma Kaskazini sasa haitasikika,” alikuwa akifiria nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati tunapotoa maagizo ya kujenga shule bila kuongeza idadi ya walimu tunatarajia nini?  Na wakati tunapotaka kutimiza mahitaji hayo ya walimu tuliyonayo kwa kuanzisha kozi za ualimu za miezi mitatu, je, huwa tunafikiri matokeo yake ya baadaye?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania imeshindwa kuendelea kwa miaka zaidi ya 46 tokea ijitawale, labda tunapaswa kuangalia mbali zaidi, tuangalie vikwazo vinavyotukabili vya nje na vya ndani.  Je ni Watanzania tu ndio wavivu wa kufikiri au ni muundo wa mfumo wa dunia ulivyo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumkumbuke mtaalam wa siasa-uchumi W.W.Rostow na hatua zake za ukuaji wa uchumi sambamba na mzunguko wa umasikini (visual circle of poverty).  Walter Rodney naye aliandika ‘Vipi Ulaya imeifanya Afrika isiendelee’ labda tunapojiuliza kwanini bado tu masikini, Rostow na Rodney wanaweza kutupa jibu.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;hshamte@mwananchi.co.tz&lt;br /&gt;0754849694&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-7975080133538013048?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/7975080133538013048/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=7975080133538013048&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/7975080133538013048'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/7975080133538013048'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2007/10/kama-rais-haelewi-nasi-pia-hatuelewi.html' title='Kama Rais haelewi, nasi pia hatuelewi'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-114915511988533356</id><published>2006-06-01T02:39:00.000-07:00</published><updated>2006-06-01T02:45:21.010-07:00</updated><title type='text'>wananchi waujadili Muungano</title><content type='html'>NILIPIGWA na butwaa niliposoma habari kuu ya gazeti la mwananchi la Jumatatu, kuhusu kauli ya Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipigwa na butwaa kwa sababu mtu mmoja ametoa kauli mbili tofauti katika kipindi kisichozidi siku 8.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki iliyopita, Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Waziri Kiongozi Nahodha walikutana jijini Dar es Salaam kujadili kero za Muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kikao chao kilichoshirikisha mawaziri kutoka pande zote mbili za muungano, viongozi hao walikutana na waandishi wa habari na kuwaeleza yale waliyokubaliana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imani yetu ilikuwa kwamba makubaliano yoyote watakayoyafikia, msingi wake ni maoni ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini imeshangaza kwa upande wa Zanzibar, inaonyesha kama kwamba Waziri Kiongozi alikurupuka tu na kukubaliana na mengi ya yaliyojadiliwa bila kuzingatia maslahi ya Zanzibar na bila kutilia maanani matakwa ya Wazanzibari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wazanzibari wa kawaida wanasema mengi tu kuhusu Muungano, nilidhani maoni yao yangezingatiwa wakati wa majadiliano ya viongozi wa juu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kutokana na mambo kama haya ya kurukana na kuonekana kwamba upo upande umeemewa na umegubikwa na upande mwingine, ndio maana wananchi waliotoa maoni yao kuhusu Muungano walisema kwamba umefika wakati mjadala kuhusu Muungano usiwe wa Serikali pekee, uwekwe wazi, uratibiwe vizuri ili vyama vya siasa, asasi zisizo za kiserikali na vyama mbalimbali vya kijamii vishiriki kujadili suala hilo kwa sababu ni suala linaloihusu jamii nzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kufanya hivyo ingeonekana wazi kwamba kwa njia moja jamii imeshirikishwa katika kujadili mustakbali wa nchi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sio kama wananchi hawawaamini viongozi wao wa Serikali zote mbili katika kufikia maamuzi yanayogusa hisia za wananchi, lakini katika mfumo wa demokrasia ya uwakilishi, hakuna ubaya wowote kushirikishwa watu wengine katika kufikia maamuzi yaliyoazimiwa na Serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi nadhani njia muafaka ya kuratibu maoni ya wananchi ni kuwaruhusu wananchi watoe maoni yao kupitia kura ya maoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwa najiuliza swali, hivi ni kwa sababu gani kila mara kunapokuwa na msukumo kutoka kwa wananchi wakiwataka viongozi wao waitishe kura ya maoni ili wananchi wapate kutoa maoni yao moja kwa moja bila kupitia kwa wawakilishi wao, Serikali huwa inapata kigugumizi, kwani ina wasiwasi gani? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutoa kura za maoni kuhusu masuala mbalimbali katika jamii ni haki ya wananchi na nadhani Serikali haitaumia chochote kama itaruhusu kutumika kwa utaratibu huo katika suala la Muungano.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inatia wasiwasi kuona Serikali ikiogopa kusikiliza maoni ya wananchi wake, matokeo yake ndiyo kama haya ya Waziri Kiongozi Nahodha kujaribu kurudisha matamshi aliyoyatoa baada ya kupata shinikizo kubwa kutoka kwa Wazanzibari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya majadiliano yale Wazanzibari walimuuliza Nahodha ana dhamira gani kwao?  Kwani Wazanzibari hawawezi kumiliki mafuta yatakayozalishwa visiwani mwao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikiwa madini si suala la muungano, kwanini mafuta ya kutoka Zanzibar yawe ni suala la Muungano?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanzo alikubali kwamba mafuta ya Zanzibar yawe ya muungano na kwa pamoja waliamua shirika la Petroli nchini (TPDC) liwe la Muungano na wajumbe wake watoke pande zote mbili za Muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka zaidi ya 40 shirika hilo lilikuwa la Serikali ya Muungano pekee, ghafla maamuzi yamepitishwa liwe la Muungano vyereje?  Kwa sababu kumevumbuliwa dhahabu (mafuta) Zanzibar?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ndiyo Wazanzibari wa kawaida tu wanayojiuliza.  Wanasema walidhani kwamba kwa kuwa madini na maliasili si suala la Muungano, petroli nayo isingeingizwa katika masuala ya Muungano.&lt;br /&gt;  &lt;br /&gt;Binafsi nadhani ni makosa kufikiri kwamba mawazo yoyote kinzani ni mawazo ya vyama vya upinzani na kwamba mwanachama wa chama tawala hapaswi kuhoji lile analoona kuwa si sawa, kwa kuwa viongozi wake wameona kwamba hilo ndilo la sawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nadhani ifike wakati masuala ya Kitaifa yasipewe sura ya upinzani, waachiwe watu wawe huru kutoa mawazo yao, sidhani kama yupo Mtanzania mwenye akili timamu asiyetumiwa na mafisadi wasioitakia mema nchi hii, atatoa mawazo kwa shabaha ya kuvuruga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waachiwe watu watoe mawazo yao kuhusu mfumo wa muungao au makubaliano ya Muungano, bila kupigwa muhuri kwamba ni wapinzani, kwani nina wasiwasi itakuwa vigumu kupata mawazo ya kujenga (constructive ideas) ikiwa watoa mawazo watajengewa dhana ya kwamba mawazo ya watu Fulani, hayastahili kuchukuliwa kama mawazo ya kujenga, hata kama mawazo hayo yatakuwa mazuri kwa kiasi gani ama yatakuwa yana maslahi kwa Taifa kwa kiasi gani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la mafuta ni miongoni mwa masuala mengi tu ya kiuchumi ambayo Wazanzibari wanahisi kwamba wamenyang’anywa, basi kabla ya kuyatolea maamuzi masuala kama hayo, kwanini basi kwamba viongozi na wataalam wetu wasiende kujifunza katika mataifa yaliyoungana na kufanikiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenyewe walisema wanakusudia kwenda kujifunza katika nchi za Scotland, Norway na Canada, sasa imekuwaje wakaanza kutoa maamuzi hata kabla ya kupata hayo mafunzo waliyodhamiria kuyapata?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilidhani kikao kile cha mawaziri kilikuwa ni kikao cha kwanza tu cha kuangalia joto ya jiwe, sikufikiria hata kidogo kama kitakuwa ni kikao cha kutoa maamuzi, ingawa kisheria wanayo mamlaka hiyo ya kutoa maamuzi kwa niaba ya wananchi wa nchi hizi mbili zilizoungana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Masuala haya yanapaswa yaangaliwe kwa kina kwani kikao cha siku moja cha Mawaziri hakiwezi kutoa majibu ya maswali magumu waliyonayo wananchi, mojawapo likiwa ni yepi yaendelee kuwa mambo ya Muungano na yepi yasiwe mambo ya Muungano.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-114915511988533356?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/114915511988533356/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=114915511988533356&amp;isPopup=true' title='6 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114915511988533356'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114915511988533356'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2006/06/wananchi-waujadili-muungano.html' title='wananchi waujadili Muungano'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>6</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-114673654654093166</id><published>2006-05-04T02:51:00.000-07:00</published><updated>2006-05-04T02:55:46.770-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-114673654654093166?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/114673654654093166/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=114673654654093166&amp;isPopup=true' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114673654654093166'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114673654654093166'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2006/05/httpphotos1.html' title=''/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-114672893035957692</id><published>2006-05-04T00:46:00.000-07:00</published><updated>2006-05-04T00:48:50.496-07:00</updated><title type='text'>Adiy: Tunataka Serikali ya Z’baritamke Muungano huu ni batili</title><content type='html'>Hey comrades&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni makala iliyotoka kwenye gazeti la Mwananchi Mei 3, huu ni mwendelezo wa makala zangu kuhusu Muungano na matatizo yake.  Kwa wale ambao hawakubahatika kuisoma makala hii kwenye gazeti, i would like to share it with you here!  Welcome!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muungano wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na kudumu kwa miaka 42, hivi sasa wametokea watu wanaohoji uhalali wa kuwapo kwake. Katika makala hii Mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na Rashid Salum Adiy mmoja wa Wazanzibari 10 waliopeleka madai mahakamani wakitaka waonyeshwe hati ya asili ya makubaliano ya Muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rashid Salum Adiy na wenzake tisa walipeleka mahakamani ombi la kupatiwa taarifa yenye maelezo ya kisheria kuhusiana na kuwapo kwa itifaki ya Muungano kati ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adiy na wenzake walifungua madai namba 20/05 katika Mahakama Kuu Zanzibar dhidi ya Mwanasheria Mkuu. Kabla ya dai hilo kupelekwa mahakamani, Juni 20, 2005 Adiy na wenzake walimpelekea barua Mwanasheria Mkuu wakitaka wapatiwe nakala ya hati ya mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar barua ambayo Mwanasheria Mkuu aliijibu Juni 22 kwa kusema kuwa ofisi yake haikuweka kumbukumbu ya nakala ya Hati ya Mkataba wa Asili wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adiy anasema Mwanasheria Mkuu amethibitisha kwamba hakuna Mkataba wa Muungano kati ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar uliofikiwa kwa mujibu wa sheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo Adiy na wenzake wamefungua upya madai yao Mahakama Kuu wakiwashtaki watu watano.  Wa kwanza ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar wakimtaka atamke kwamba Muungano si halali kwa mujibu wa sheria za mikataba ya kimataifa.  Adiy anasema Mkataba wa Muungano haukufuata mkondo wa kisheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Ili mkataba wa kuunganisha nchi ufikiwe ni lazima kwanza vyombo halali vya kisheria vya nchi zinazotaka kuungana vijadili suala hilo, lakini kwa upande wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Bunge la Tanganyika tu ndilo lililoketi na kupitisha Mkataba wa Makubaliano (Memorandum of Understanding),” anaeleza Adiy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo Bunge la Tanganyika lilipitisha muswada wa makubaliano ya Muungano Aprili 25, 1964 wakati Rais wa Tanganyika Julius Nyerere na Rais wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar, Abeid Aman Karume waliweka saini makubaliano hayo ikiwa ni pamoja na vipengele 11 vya mambo ya Muungano, Aprili 22, 1964.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adiy anasema mkataba wa Muungano haukupaswa kufungwa kabla ya ‘Memorandum of Understanding,’ na hilo ni kosa kwa mujibu wa makubaliano ya kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo Adiy anasema ikiwa Bunge la Tanganyika liliketi na kuridhia makubaliano ya Muungano, Baraza la Mapinduzi Zanzibar halikuketi kuridhia makubaliano hayo.  “Ikiwa wanasema kuwa kwa wakati ule Zanzibar ilikuwa ikiendeshwa kwa ‘decree’ ya kijeshi, basi ielezwe bayana kwamba, Muungano uliopo uliundwa kwa amri za kijeshi chini ya Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Tanganyika na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na ikiwa hivyo ndivyo, basi Muungano uliopo hauna ridhaa ya wananchi ni muungano wa kijeshi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Unajua hakuna Muungano uliofanyika, bali uliofanyika ni uvamizi tu na hivi sasa Zanzibar ni koloni la Tanganyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sisi tunachotaka ni kuonyeshwa mkataba wa Muungano ambao uliwekwa saini na Nyerere na Karume na tumeambiwa kuwa haupo, na tumeambiwa hivyo kwa sababu hakuna kilichosainiwa,” anaeleza Adiy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Wa pili atakayeshtakiwa katika dai jipya ni Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi kwa sababu yeye kama Mtendaji Mkuu alipeleka indhari gani kwa serikali kuifahamisha kwamba kinachofanywa si halali?” Anahoji Adiy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wa tatu ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa huyu anatakiwa aeleze kwanini ameiondolea Zanzibar uanachama wake wa kudumu katika Umoja wa Mataifa?  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wa nne ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa ni chama kilichoweza kuweka sera na misingi ya kisiasa iliyoikandamiza na kuidhoofisha Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na wa mwisho atakayeburuzwa mahakamani ni Spika wa Baraza la Wawakilishi ambaye yeye atahojiwa kwanini amesimamia vikao vya Baraza bila kutaka kuthibitishiwa kwamba Zanzibar ni sehemu ya Muungano na anapaswa awe na maandishi ya makubaliano yaliyofikiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adiy anasema ikiwa Mwanasheria Mkuu atashindwa kutamka kuwa Muungano si halali kwa mujibu wa sheria, basi yeye na wenzake watawaeleza wananchi kuhusu jambo hilo na hatimaye ni nguvu ya umma ndiyo itakayoamua la kufanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sisi wasimamizi wa suala hili tuko 10 tu ambao ni mimi Adiy na wenzangu ni Rashid Ahmed Rashid, Rashid Yussuf Mchenga, Haji Sheha Hamadi,  Abdallah Hassan Mrisho, Mbaruk Sheha Simai, Khamis Ismail Makame , Ali Simai Mwadini, Nassor Hassan Nassor na Ali Omar Ali, lakini nyuma yetu wake Wazanzibar zaidi ya 10,000 wanaotuunga mkono, hivyo tutahakikisha kwamba dai letu hili ikikosa majibu ya kisheria ya kuridhisha, tutawahamasisha Wazanzibari wengi zaidi watuunge mkono na hatimaye iitishwe kura ya maoni, kinyume cha hivyo hatutapumzika mpaka tujue khatima ya Zanzibar chini ya uvamizi wa Tanganyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 inasema kuwa, Zanzibar ni sehemu ya Muungano wa Tanzania, ikiwa hivyo ndivyo Tanzania iko wapi ikiwa walioungana ni Tanganyika na Zanzibar?” Anahoji Adiy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adiy na wenzake, Aprili 26, 2006 wamefanikiwa kufungua kesi mpya ya madai katika mahakama kuu, kesi hiyo ya madai nambari 04/06 linaloiomba mahakama itoe amri ya ‘CERTIORARI NA MANDAMUS’ ili kumlazimisha Mwanasheria Mkuu atamke kwamba Muungano si halali kwa mujibu wa sheria za mikataba ya Kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwa mashtaka anayoshtakiwa Mwanasheria Mkuu Zanzibar ni kukataa kutoa tamko la ukweli la kisheria kwamba Muungano kati ya Jamhuri ya watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika sio halali na Zanzibar si sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadhalika Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi anashtakiwa kwa kushirikiana na Mwanasheria Mkuu Zanzibar kufanya kitendo kinyume cha sheria na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 toleo la mwaka 2003 kwa kuidanganya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na wananchi wa Zanzibar kuwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar imeungana na Jamhuri ya Tanganyika na kuwa Jamhuri moja huru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala jingine wameliita kuwa ni kufanyiwa udanganyifu na viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kushirikiana na dola ya kigeni ya Tanganyika na kuvunjwa kwa haki mbalimbali za Zanzibar kwa Wazanzibari kupotezewa uhuru wa kujiamulia mambo yao wenyenwe ndani na nje ya nchi yao kwa muda wa miaka 42.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-114672893035957692?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/114672893035957692/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=114672893035957692&amp;isPopup=true' title='13 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114672893035957692'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114672893035957692'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2006/05/adiy-tunataka-serikali-ya-zbaritamke.html' title='Adiy: Tunataka Serikali ya Z’baritamke Muungano huu ni batili'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>13</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-27184597.post-114621011953811094</id><published>2006-04-28T00:31:00.000-07:00</published><updated>2006-04-28T00:41:59.556-07:00</updated><title type='text'>Zanzibar haikukubali Muungano, ililazimishwa tu</title><content type='html'>Aprili 26, 2006 Watanzania wameadhimisha miaka 42 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wakiwa na mengi ya kujadili. Miongoni mwa mambo ambayo hivi sasa yako wazi kama ajenda zilizo huru kujadiliwa ni suala hilo la Muungano.  Katika makala hii, mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na Katibu wa Kwanza wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Salum Said Rashid ambaye anajulikana miongoni mwa wanaharakati wenzake kwa jina la Komredi Rashid. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Komredi unaweza kukumbuka namna nchi hizi mbili zilivyofikia hatua ya kuungana Aprili 26 mwaka 1964 na namna ninyi wa Baraza la Mapinduzi mlivyoshirikiana na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Abeid Amani Karume?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Zanzibar katika miaka ya 60 hadi mwanzoni mwa miaka ya 70 ilikuwa ikiendeshwa na Baraza la Mapinduzi na Baraza la Mawaziri na kulikuwa na ‘decree’ ya kirais (Presidential Decree) ambayo iliweka mfumo wa utawala. “Decree hii ilitaka Baraza la Mawaziri liwe linapeleka waraka wa Baraza (Cabinet Paper) kuhusu kila kitu kwa Baraza la Mapinduzi.  Kwa jambo kama la Muungano ilitakiwa iwepo sheria ya kirais (Presidential Decree). Hiyo haikuwapo na hiyo ilikuwa itiwe saini na Rais na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na baadae ichapishwe katika gazeti rasmi la serikali, mambo ambayo hayakufanyika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Sasa nini kilifanyika hata kuwezesha kuendelea kuwapo kwa muungano huo hadi hivi leo, wakati jambo hilo halikufanyika?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Muungano upo na utaendelea kuwapo kwa sababu Muungano huo umeweza kuendelea kutokana na mfumo wenyewe. Kuna serikali mbili, ya Muungano na ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kuna mambo ya Muungano na kuna mambo ya Serikali ya Zanzibar, usimamizi uliopo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ndio uliofanya Muungano huo uendelee kuwapo.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano wa ulinzi na usalama, utaona ya kwamba katika mambo 22 ya Muungano hakuna kitu kilichothaminiwa, kinachofanya kazi na kutiliwa nguvu kama suala la ulinzi kuliko la uchumi.  Ndio maana utaona kila pahala katika Zanzibar kuna vyombo vya dola vya Muungano, jeshi, polisi, usalama, hizi taasisi za vyombo vya dola ndivyo vilivyofanya Muungano ukasalilia mpaka hii leo, lakini sio kuwa umeleta faida kwa Wazanzibari au hata Watanganyika, faida gani waliyopata Tanganyika hadi leo?  Labda lawama!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pale mwanzo tuliulizana huu Muungano umemletea nani tija?  Umeleta tija kwa madola ya Magharibi kwa sababu wakati ule Zanzibar ilikuwa ina "strategic importance" na ilikuwa zaidi katika suala la Ukomunisti na Usoshalisti, na ule ulikuwa ni wakati wa vita baridi, na wao walikuwa na wasiwasi kuwa Serikali na Mapinduzi ya Zanzibar na Zanzibar yenyewe inaweza ikawa ndio ngome ya kupeleka Ukomunisti Tanganyika na hata Afrika nzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Usichukulie ukomunisti unavyoandikwa hivi leo na Magharibi kuwa umekufa, uchukulie katika mwaka 1964, kulikuwa hakuna ‘One Super Power’ kuna ‘two’ na ‘Super Power’ moja ilikuwa ikituunga mkono sisi, ya Kirusi na China na mataifa yote ya Kikomunisti.  Wakati ule tulipata silaha kutoka Urusi na masuala ya usalama tulikuwa tukijifunza kutoka Ujerumani ya Mashariki (GDR).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:   Komredi naomba turudi nyuma kidogo kuhusu lile suala la tija, kwa vipi Muungano haukuwaletea tija Watanganyika wala Wazanzibari?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Haukuwaletea tija Watanganyika wala Wazanzibari bali umewaletea migogoro. Tanganyika haikueleweka kimataifa kutokana na mikasa iliyotokea Zanzibar ambayo ilikuwa lazima iihami katika vyombo vya kimataifa, imeiletea migogoro kuwa mpaka leo inalaumiwa kuwa imeimeza Zanzibar, imeiletea mpaka leo migogoro kwa sababu kuna kero za Muungano, kama haziko hizo, Tanganyika isingepata tabu, isingepata lawama, kwa hiyo utaona kuwa hakuna tija kwa Watanganyika labda kwa watawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanganyika imepita katika misukosuko mingi ya kisiasa kama mataifa yote ya Afrika, lakini hata hivyo Zanzibar imepata misukosuko mingi zaidi kuliko Tanganyika na mpaka leo iko katika misukosuko kwa mfano hakuna agenda Zanzibar, leo kuna agenda ya CUF, kuna agenda ya CCM na haya ni madhara makubwa kwa Wazanzibari wote, kwa sababu kila nchi lazima iwe na agenda, wenyewe wanakubali kama Zanzibar nchi, katika fomu ya pasi ya kusafiria unaulizwa kama unataka kuandika nchi Tanzania ama Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Ikiwa hivyo ndivyo, unasemaje kuhusu ile kesi ya uhaini iliyomkabili Maalim Seif Sharif Hamad na wenzake na mahakama ikatoa maamuzi kuwa Zanzibar si dola?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Yule aliyetoa uamuzi ule hafahamu sheria za kimataifa. Zanzibar mpaka leo ni mwanachama wa United Nations kwa sababu haikufuta uanachama wake, kilichotokea ilifunga ofisi yake, ikachanganyisha na ofisi ya Tanganyika, hakuna utaratibu wa kujitoa katika Unietd Nations ukishakuwa umo katika 'charter' ya United Nations.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini matatizo ya Zanzibar ni ya ndani si ya nje, yapo yanayosababishwa na Muungano na yapo ambayo hayasababishwi.  Yanayosababishwa ni zaidi ya kiuchumi kwa sababu katika mambo 22 ya Muungano, mengi ni muhimu ya kiuchumi ambayo hayako katika madaraka ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.  Kwa miaka sasa hivi kuna tatizo la TRA, kuna tatizo la mafuta, SMZ ina gharama nyingi, haina mbinu za mapato, haina uwezo wa kuweka sera katika sekta ya uchumi kwa sababu mambo yote muhimu ya uchumi yako katika mambo ya Muungano, ukichukua mawasiliano, mafuta, sarafu…&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Wakati hayo yakiingizwa katika makubaliano ya Muungano, wanasiasa wa Zanzibar na wataalam walikuwa hawaoni kama mambo hayo yatakuja kuleta matatizo baadaye?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Wakati ule (1964) Wazanzibari kadhaa waliona kwamba kutakuwa na matatizo, mimi mmoja wao niliona na nikaasa sana na kukataa na nanukuliwa katika vitabu  kwamba nimesema ‘inachukuliwa mamlaka na madaraka kamili ya Zanzibar na hatupati kitu chochote kile, lakini ujue yale mazingira ya wakati ule yalilazimisha hayo.  Kwa sababu kwanza shauri la Muungano halikutoka Zanzibar lilitoka Tanganyika kwa sababu ilishinikizwa na Amerika na Uingereza, vitabu na magazeti yote viliandika kwamba Muungano ilikuwa project ya (Mradi wa) CIA (Shirika la Ujasusi la Marekani), kwa hiyo Muungano si project ya Tanganyika, ilikuwa project ya nje, na kwa wakati ule kwa Tanganyika, Zanzibar ni mambo ya nje na mpaka siku za hivi karibuni mambo ya Muungano yalikuwa yakiendeshwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar hakuna agenda ya ndani wala ya nje. Ndio maana Wazanzibari tunaumia, na nchi yoyote ile ambayo haina agenda haiwezi kufanikiwa, mathalan chukua uchumi, Zanzibar inanuka njaa!  Je kuna mipango yoyote ya kuondoa njaa hii?  Haiwezi ikawepo kwa sababu mipango hiyo lazima iwe ya kimuungano, kwa sababu mambo yote muhimu ya uchumi yako katika mambo ya Muungano. Serikali ya Zanzibar haiwezi ikasema inapunguza ushuru ili iimarishe biashara, itaambiwa si mambo yako hayo!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Unasema kwamba mlitoa ushauri, sasa ilikuwaje ikawa ule ushauri wenu haukusikilizwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Mazingira hayakuruhusu, siasa ya nje ya Muingereza na Mmarekani haikuturuhusu kufanya hivyo, walitung’ang’aniza kuwa lazima tuungane.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Je unataka kusema kuwa hata Karume mwenyewe hakuwa na uamuzi juu ya hilo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Karume alitishwa! Hata sisi tulitishwa. Siyo Karume tu, tuliambiwa ya kwamba hapa patavamiwa, na sisi tutakamatwa na Serikali ya Mapinduzi itafutwa, na Magharibi haikubali hata siku moja kuwa Zanzibar iwe ya kikomunisti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya hayakufanyika hapa tu katika ulimwengu, yalifanyika katika mataifa mengi sana, yamefanyika British Guyana, yamefanyika katika Domican Republic na nchi nyingi nyingine, siyo Zanzibar tu, katika miaka ya 50 na 60 mpaka kumalizika ukomunisti, mataifa madogo ya ulimwengu wa tatu na hata mataifa madogo ya Ulaya yalikuwa yakiishi katika hali ya hatari, hali ya wasiwasi, hayawezi yakawa na sera zao wenyewe kama leo unavyoona, lazima watu wafuate IMF, lazima wafuate World Bank na wakati ule ilikuwa lazima wafuate ubepari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Sasa ikiwa walikataa Zanzibar isiwe nchi ya Kikomunisti, lakini baada ya miaka michache tu baada ya muungano, 1967, Mwalimu Nyerere akaifanya Tanzania ikawa nchi ya Kisoshalisti?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Walimpinga. Walilipinga Azimio la Arusha. Nyerere alitoka mrengo wa kulia akaingia wa kushoto kwa sababu wakati ule marafiki wa Afrika walikuwa Wakomunisti na maadui wa Afrika walikuwa Wakepitalisti, ukichukua suala la ukoloni, hakukuwa na koloni la Mashariki katika Afrika, kulikuwa na makoloni ya Magharibi, halafu katika vita vya kumuondoa mkoloni waliounga mkono ni mataifa ya Mashariki, siku zile vita vilikuwa vikipiganwa kwa silaha katika Afrika, waliokuwa wakitoa silaha ni mataifa ya Mashariki, waliokuwa wakifundisha watu kupigana ni mataifa ya Mashariki, kwa hivyo Mwalimu hakufanya makosa aliposema kwamba marafiki zake wa kweli ni mataifa ya Mashariki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Unasema kwamba walimpinga Mwalimu Nyerere, kwanini wasimtishie kama walivyoitishia Zanzibar?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Kwa sababu yeye hakuwahi kusema ni Mkomunisti, alisema yeye ni mjamaa, tena Ujamaa wa Kiafrika kama wa Leopard Sengo ambaye ndiye aliyeanzisha ‘African Socialism.’&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walimpinga kwa sababu alifilisi mali yao, mabenki yao, viwanda vyao, mashirika yao ya bima, madini yao, mali yote ya Magharibi yalifilisiwa, lakini leo si yamerudi palepale?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Tumeshaona historia na sababu za kuwapo kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, sasa tufanye nini ili kuimarisha huu Muungano ambao pamoja na kuwapo kwake kwa utatanishi lakini kila mtu anaona kwamba umeleta faida zaidi kuliko hasara?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Sisi  tulivyokuwa tunagombania Uhuru, lengo letu lilikuwa umoja wa Afrika na tulifahamu umuhimu wa kuungana na ushahidi wa umuhimu wa kuungana unaonekana dhahiri hivi sasa, kwa sababu Afrika haikuungana. Kuna matatizo Afrika nzima na haya hayataondoka mpaka Afrika iungane, kwa hiyo huu Muungano, ukiuchukulia kama chanzo cha Umoja wa Afrika, ni kitu cha maana sana, kama kuna haja au hakuna haja ya Muungano kama ulivyo mfumo wake hivi sasa hilo ni suala jingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umeuliza kifanywe nini. Cha kufanya sasa hivi wakati tuna miaka 42 ya Muungano, kila Mtanganyika, Mzanzibari afanye tathmini, amepata faida gani yeye binafsi katika Muungano huu katika hii miaka 42?  Acha lile tabaka tawala, la Tanganyika na la Zanzibar, wananchi wa kawaida wamepata faida gani?  Watanganyika wamepata faida gani, Wazanzibari wamepata faida gani?  Vipi wanaweza kupata faida katika Muungano?  Kwa mfumo upi?  Hili ni suala la watu wote, lakini kwa fikra zangu mimi, kunatakiwa tathmini ya haraka sana ambayo ifanywe kwa uwazi na watu wote washirikishwe hasa hapa Zanzibar kwa sababu Tanganyika haikumezwa, iliyomezwa ni Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hivyo hili suala ni muhimu zaidi hapa Zanzibar kuliko Tanganyika, halafu usisahau kwamba kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Muungano ndiyo Serikali ya Tanganyika, kwa hivyo Tanganyika imeongezewa madaraka na Zanzibar imepunguziwa madaraka katika huu mfumo wa Muungano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa watu wanailaumu SMZ katika sekta ya uchumi lakini haina nguvu, watafanya nini?  Hawawezi wakakaa wakaita wataalam wa mambo ya uchumi, kuwapangia mipango ya kuendesha uchumi wa Zanzibar kwa sababu mambo yote ya uchumi ni mambo ya Muungano, hilo ndilo tatizo kubwa lililomo katika Muungano.  Ikiwa mambo haya hayatarekebishwa matatizo hayatakwisha, tatizo kubwa ni kuwa hakuna agenda Zanzibar na hiyo ndiyo sumu inayowaua taratibu Wazanzibari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Swali:  Unasema kwamba Tanganyika haikumezwa iliyomezwa ni Zanzibar, lakini kuna maneno yanayosemwa kwamba Zanzibar wamenufaika zaidi na Muungano kuliko inavyonufaika Tanganyika kwa sababu Wazanzibari wanapata fursa zaidi ya kufaidi matunda ya Muungano kuliko wanavyopata Watanganyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Hiyo inaeleweka, kwa sababu Nyerere, mwenyewe aliliona hilo lakini kwa kuwa Tanganyika ni kubwa sana kuliko Zanzibar ni lazima aliye mdogo apate ‘prevelages’ fulani ambazo hawezi kupata mkubwa, ili ile dhana ya samaki mkubwa kummeza mdogo isije ikashika mashika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mfumo wa Muungano wa wakati ule tofauti na wa leo, wakati ule Karume alikuwa na madaraka, alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, halafu kulikuwa na vyama viwili, Zanzibar chake na Tanganyika chake (TANU na ASP), ulipokuja utaratibu wa chama kimoja tena ndicho chenye madaraka ya mwisho, utaratibu huo ulitumika vibaya sana kuondosha madaraka kutoka Zanzibar kuyapeleka katika Jamhuri ya Muungano na mambo mengi yalipitishwa wakati huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata ile Katiba ya Muungao ilipokuja haikuja katika utaratibu uliowekwa katika hati iliyotiwa saini na marais wawili kwa sababu ilitakikana liitwe Bunge la Katiba, halikuitwa Bunge la Katiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Sasa Bunge hilo la Katiba lingeitishwa vipi kwa pande zote mbili wakati Zanzibar hakukuwa na Bunge?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Kwa mujibu wa ‘Presidential Decree’ namba 3 iliyotiwa saini na Karume na mimi kama Katibu wa Baraza la mapinduzi, ilikuwa lazima uitwe uchaguzi mwaka mmoja baada ya Mapinduzi na ile hati ya Muungano ilikubaliwa liitishwe Bunge la Katiba mwaka mmoja baadaye ili kutathmini na kupasisha Katiba ya Kudumu ya Muungano na uchaguzi Zanzibar ulikuwa ufanyike Januari 1965, lakini yote hayo hayakufanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa pana mambo mawili, kuna sheria na kuna hali halisia ya mambo yalivyo, tukubali, tusikubali, Muungano upo, umeendelea miaka 42 na hakuna ishara ya kuonyesha ya kwamba utatoweka!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Sasa tufanye nini ili kuondosha hizo zinazoitwa kero za Muungano?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Vipi Wazanzibari washirikishwe katika kuondosha kero hizi. Kwanza SMZ lazima izishughulikie, hasa Rais wa Zanzibar kwa sababu huu Muungano ulikuwa kati ya Rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar, pahala pazuri sana ni rais wa Muungano na Rais wa Zanzibar kuzishughulikia kero za Muungano.  Kwa upande wa Tanganyika kuna utaratibu, kwa upande wa Zanzibar utaratibu unaofaa ni kuwashirikisha Wazanzibari wote na kufahamishwa, kuelezewa ili sote tuwe na agenda ya Zanzibar, nikisema hivyo namaanisha kwamba chama kilicho katika madaraka na chama cha Upinzani, juu ya suala hili wasiwe na mgogoro na uhasama na uadui kwa sababu linawahusu watu wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Lakini lipo tatizo jingine la kuwa hali ya Zanzibar kuwa ni dola ama si dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Zanzibar unaweza kusema ni ‘sovereign’ na si ‘sovereign’.  Kisheria Zanzibar ‘sovereign’ na inaweza leo ikadai ile ‘sovereignty’ yake. Mwalimu Nyerere aliwahi kumwambia Colen Legarb wa ‘London Observer’ (1965) kwamba ikiwa Wazanzibari watataka kuuvunja Muungano, sitawapelekea majeshi ‘I will not bomb them’ (anamnukuu alivyosema Nyerere), Mwalimu kama mwasisi wa Muungano alijua kwamba Karume alikuwa akiliwakilisha taifa iliyo huru, wala Zanzibar haikutekwa kijeshi na Tanganyika, wala kihistoria Zanziabr katika karne 4 zilizopita haijapata kuwa sehemu ya Tanganyika, ingawa Tanganyika ilipata kuwa sehemu ya Zanzibar lakini Zanzibar haijapata kuwa sehemu ya Tanganyika.  Ufalme wa Zanzibar ulikuwa ukitawala takriban katika ufukwe wote wa Afrika Mashariki ikiwemo Dar es Salaam, Kilwa na kwengineko halafu Mjerumani akainunua Tanganyika kutoka Zanzibar na akaitawala, lakini nawaomba Watanganyika wasiwe na chuki na Zanzibar kwa mambo yaliyopita.  Haina haja ya chuki, sisi ni mataifa pacha, Tanganyika na Zanzibar, sisi tunapenda Muungano uendelee na haiwezekani Zanzibar ikakaa katika uhasama au ikaihatarisha Tanganyika, itakuwa tunajihatarisha wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maamuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Rufaa Tanzania ninavyoitafsiri mimi ni kuwa ikiwa ukitaka kupindua ni lazima upindue Serikali ya Muungano, huwezi ukapindua Serikali ya Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Kwanini isiwezekane kupindua Serikali ya Zanzibar wakati ina Rais wake na chombo vyake vya kutunga sheria, kwanini isipinduliwe?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Kwa sababu mpaka leo haina utambulisho wa kimataifa.  Ikiwa tutakubaliana kwamba kuna faida kubwa ya kuwa na viti viwili kuliko kimoja katika Umoja wa Mataifa kwa upande wa Tanzania, kesho Zanzibar itampeleka mtu kama Balozi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Ilikuwaje Zanzibar ikakubali kunyimwa haki zote hizo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Hii nakurudisha tena pale kutokana na mazingira ya wakati ule.  Kwa nini Zanzibar ilikubali kutawaliwa na Mwingereza mwaka 1890, Kwa nini katika mwaka 1808 ilikubali kutawaliwa na Ujerumani? Kwanini Afrika ilikubali kugawanywa na kutawaliwa na wakoloni?  Huwezi kusema kuwa ilikubali, ililazimishwa kukubali mipango ile.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete alisema kwamba muundo wa Muungano hauna matatizo, bali wenye matatizo ni viongozi, je wewe unasemaje juu ya hilo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Mimi naona hili suala la viongozi muhimu sana, lakini itakuwa makosa kama viongozi watakaa kwenye vikao vya siri kuyatatua matatizo haya, hayataondoka, haya matatizo yanawahusu wananchi, hayawahusu viongozi.  Vilevile Rais Kikwete ameagiza Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi wakutane hata kama hakuna matatizo.  Ikiwa Jaji Nyalali na Jaji Kisanga wameona kama kuna matatizo.  Walizungumza na watu wengi na walichukua muda mrefu na kuona kuwa una matatizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nadhani iko tofauti kubwa kati ya awamu ya Kikwete na zile zilizopita, angalau yeye anazungumzia kuwa kuna kero, pia amesema kuwa suala la Zanzibar linategemea Wazanzibari wenyewe.  Suala la Zanzibar liko namna mbili; Huwezi ukatatua migogoro ya kisiasa ndani ya nchi ukapata maendeleo peke yake bila kutatua kero za Muungano, haiwezekani, hayo mambo mawili yanakwenda sambamba.  Suala siyo Serikali mbili au tatu, suala ni madaraka na mamlaka ya Serikali, leo yakipunguzwa mambo ya Muungano yakarudishwa kwenye SMZ, mambo katika sera za sekta za uchumi na pakawepo Zanzibar suluhu ya kisiasa kati ya watu wanaogombana, wenye uhasama na uadui hali inayosikitisha hasa ukizingatia kwamba hawa ni ndugu.  Ikiwa Zanzibar kuna agenda na kuna mipango ya kiuchumi katika miezi 18 tu hali ya maisha Zanzibar yanaweza yakabadilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Kwa hiyo unasema kuwa tatizo kubwa la Wazanzibari katika Muungano ni uchumi zaidi kuliko siasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Unajua sisi ni nchi ndogo, na hatuna ‘ambitious’ zile za kutawala na ‘ku-influence’ hatuwezi, hata kama tukitaka.  Zaidi kitu ambacho kingetushughulisha sasa hivi ni kula yetu, ajira kwanza, halafu tukishakuwa katika hali nzuri na tunaendelea ndio masuala hayo ya Serikali ngapi yafuate.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mambo mengi Zanzibar imenyang’anywa. Ziko ‘economic and financial consequenses’ za Muungano.  Kwa mfano mpaka leo suala la ‘currency board’ ya Afrika Mashariki halijamalizika.  Kuna fedha za Zanzibar ambazo mpaka leo haijazipata kutoka Serikali ya Muungano, itabidi zifanyiwe hesabu za miaka 42 ili tujue nani kapata faida na nani hakupata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wapo wanaosema kuwa matatizo ya nchi masikini zinazoendelea ni ulafi wa viongozi tu, je dhana hiyo ina ukweli kiasi gani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Mimi nafikiri matatizo yanatokana na mifumo ya kiutawala si ulafi wa viongozi, ile mifumo ambayo inawafanya watu kama hao wakawa viongozi, watu walafi, wala rushwa na wasio na uzalendo, watu wanaojipigania maslahi yao kwa kurundika mali na kujibeparisha na wasiojali maslahi ya umma. Ikiwa katiba inampa nafasi Rais kusema ‘serikali yangu’ huoni kama hiyo ni hatari! Ikiwa itatokea nafasi ya kubadilisha katiba hapa Zanzibar, tunapaswa tuwe makini sana ili taasisi zisiweze kutengeneza madikteta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini nchi yoyote ile ambayo watu wamegawanyika kama tulivyogawanyika sisi hapa Zanzibar, ikawa kuna uadui na uhasama kati ya pande mbili zinazoleta mtafaruku wa kisiasa, maslahi yake hupotea, nchi ambayo haina umoja wa kitaifa haiwezi ikasimamia maslahi yake.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/27184597-114621011953811094?l=mnyongemnyongeni.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/feeds/114621011953811094/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=27184597&amp;postID=114621011953811094&amp;isPopup=true' title='9 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114621011953811094'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/27184597/posts/default/114621011953811094'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyongemnyongeni.blogspot.com/2006/04/zanzibar-haikukubali-muungano_28.html' title='Zanzibar haikukubali Muungano, ililazimishwa tu'/><author><name>Hawra Shamte</name><uri>http://www.blogger.com/profile/02739017252907078272</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='27' height='32' src='http://photos1.blogger.com/blogger/1437/2856/1600/DSCF0074.jpg'/></author><thr:total>9</thr:total></entry></feed>
