" Jamii iliyostaarabika ni yenye kuheshimu Mawazo & Mitazamo ya wengine. Mchango wako katika kazi yoyote ulenge kujenga jamii yenye Kujitambua, Kujithamini na Kujiwajibisha "

 
Thursday, October 04, 2012

 CCM, kazi ya kupiga tantararira waachieni wapinzani

CCM, kazi ya kupiga ‘tantararira’ waachieni wapinzani


Hawra Shamte

WIKI iliyopita Dodoma palikuwa hapatoshi, palitaka kuchimbika bila jembe. Lakini mwishowe kilieleweka! Napenda kuchukua fursa hii kukipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa kufanya uchaguzi wake wa ndani.

Kilichonifurahisha zaidi ni pale Mwenyekiti alipoweka bayana kuwa ‘mtu mzima hatishiwi nyau! Wale wote waliokuwa wakitingisha kibiriti, walikuta kimejaa!

Mwenyekiti alisema anayetaka kuondoka CCM aondoke, kwani bila shaka atakuwa ameshajiandalia pakwenda. Kwa msisitizo zaidi alisema wanaotaka CCM ife, watakufa wao! Duh! Hilo nalo neno!

Lakini nilichojifunza ni kuwa kumbe yawezekana kufanya mabadiliko kama dhamira ikiwa ya dhati. Walisema kuwa wanataka kubadili safu ya uongozi, ikibidi vijana waingie kwa wingi zaidi na wazee waachie nafasi.

CCM hawakuwatoa wazee kwa fujo, bali wanawaengua taratibu kimkakati. Mlichofanya Dodoma tumekiona, lakini bila shaka haitoshi kubadilisha rangi ya chupa, mvinyo ikabaki ileile.

Ingawa ni Chama chenu, lakini nadhani kama kwamba Watanzania wengine pia wanayo haki ya kusema na kutoa ushauri kwa sababu hicho ni Chama Tawala. Serikali yetu inaongozwa na sera za Chama Cha Mapinduzi, hivyo wananchi wote kwa namna moja ama nyingine tunayo haki ndani ya chama tawala.

Kwa kuwa hatupati fursa ya kuingia ndani ya vikao vya Chama, lakini nafikiri kuwa sisi tunaruhusiwa kutoa mawazo yetu kwa kutumia majukwaa mengine na tunatarajia kuwa mawazo yetu yatatiliwa maanani.

CCM kubadilisha safu ya uongozi ni jambo moja, lakini jambo la pili ambalo lina umuhimu sawa na lile la kwanza nafikiri ni kubadilisha dira na mwelekeo.

CCM inachofanya ni kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa kupanga safu safi! Lakini haitoshi, kwani yapo mambo ambayo CCM inapaswa iige kutoka kwa vyama vingine, nayo ni ule mshawasha na moto wa mabadiliko.

Mabadiliko haya yasiwe ya nadharia, bali yawe ya vitendo. Kama CCM iliweza kudhibiti faulo katika uchaguzi wake wa ndani, tunatarajia itafanya hivyo hivyo katika Uchaguzi Mkuu wa vyama vingi. Mizengwe na rushwa iwe mwisho wake umefika! Kwa kuwa CCM ndiyo kinara, kinapaswa kiwe ndicho kiigizo chema kwa vyama vingine.

Ninachoweza kusema ni kuwa CCM ina kazi kubwa ya kujirudisha katika mioyo ya wakulima na wafanyakazi, katika mioyo ya walalahoi na wapenda haki, kinyume cha hivyo kitaendelea kurukishwa kichura na vyama vinavyofahamu kutumia mtaji wa walalahoi.

Tunatarajia kuiona CCM ikiyaona matatizo yake kama changamoto na iweke dhamira ya dhati ya kuzifanyia kazi changamoto hizo.

Athari ya mabadiliko ndani ya CCM inapaswa ionekane mpaka ndani ya Serikali, kwani Serikali iliyopo madarakani inaongozwa na CCM.

Kwa muda huu mchache wa miaka mitatu kasorobo, wananchi wangependa kuona mabadiliko ya dhati yakifanyika kwa watendaji wa Serikali. Dhamira za kutokomeza rushwa zitekelezwe, azma za kupambana na ubadhirifu wa mali za umma zitimizwe na shabaha na malengo ya kumpatia maisha bora kila Mtanzania yaelekezwe panapostahili, mwananchi angalau aone mwanga wa maisha yake, ajue anakoelekea, apate matumaini mapya, hiyo ndiyo dawa pekee ya kurudisha imani ya wananchi kwa CCM.

Dhamira ya dhati ya kumkomboa Mtanzania inapaswa itekelezwe kwa vitendo, kazi ya kupiga ‘tantararira’ (kupiga domo) waachiwe wengine kwa sababu hiyo ndiyo kazi yao, kwa kuwa hawana Serikali ya kuiendesha.

Ahadi za ajira zisiwe za kutiana hasira, kwa sababu tunaona jinsi vigogo wanavyopendeleana, jinsi nafasi za ajira zinavyokwenda kwa watoto wa wakubwa. Tunaona jinsi vijana wetu wanaomaliza vyuo na kuhangaika mitaani, wanavyoambiwa wajiajiri wakati hawajui hata wataanzaje.

Nafasi za kazi zinazotolewa zinaelezwa wazi kuwa anahitajika mtu mwenye uzoefu wa miaka isiyopungua mitatu; huyu kijana aliyemaliza chuo mwaka huu, uzoefu ataupata wapi na vipi? Hizi tulizonazo ni sera za kukwazana!

Wananchi wanaoumia kwa jasho, wanaotembea Azimio la Arusha kwa kukosa nauli za daladala, wanaoingia kwenye daladala na kubanana kama mishikaki, wanaoumiza vichwa kupanga bajeti ya siku, isiyopangika, ndio wanaoujua uhondo wa ngoma!

Kimsingi hawa hawahitaji kujazwa mapesa mifukoni, bali wanachohitaji ni kuboreshewa huduma zote muhimu, maji, afya, elimu na usafiri.

Kadhalika hata mazingira ya uwajibikaji nayo yaboreshwe, biashara zao wazifanye kwa wasaa na ikibidi wapunguziwe kodi na ushuru.

Kwenye sekta ya kilimo wakulima wapelekewe pembejeo na wapewe elimu ya kilimo cha kisasa, maafisa ugani waache kukaa ofisini, waende vijijini kuwahudumia wakulima.

Tunaona jitihada katika barabara, lakini bado tunahitaji mtandao mpana zaidi wa barabara hadi vijijini.

Miaka 50 baada ya Uhuru bado ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndio wanaopata umeme, hivyo jitihada zaidi za kuzalisha umeme na kuusambaza zinahitajika.

Tusitegemee tu chanzo cha aina moja cha kuzalisha umeme, inawezekana kutumia vyanzo vingine ambavyo tunavyo, Serikali sasa inapaswa ibadilike; badala ya kuchukua taarifa za kitaalamu na kuziweka kwenye makabrasha na kisha kuziweka kabatini, sasa ripoti hizo zifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.

Kupanga ni kuchagua, tukichagua vyema vipaumbele vyetu tutaweza kufikia malengo. Tuache kuweka vipaumbele saba katika mipango mikakati yetu ya maendeleo. Tuwe na vipaumbele vichache, tulivyovipanga vyema ambavyo tunaweza kuvitekeleza kutokana na rasilimali tulizonazo.

Dhamira peke yake bila vitendo haikidhi haja, tupunguze ahadi, tufanye kazi! Inawezekana, kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake!

0655 849694





3 Maoni ya Wasomaji:

Anonymous Kitoto anasema...

Lugha safi yenye ucheshi na utamu wa Kiswahili- maudhui changamoto...

8:24 PM  
Anonymous Anonymous anasema...

This does not make a lot of sense to some people given the fact that they
feel it might frustrate them more than help them.
Another notable person in the development was Dmitry
Pavlovsky who worked together with Alexey to make the game
on the Elektronika 60, a Russian computer. Companies are being set up
to come up with ideas for apps and produce them for the
growing market that the i - Phone has spawned. If you make more than one row at a time, you score more points.
Sweet and simple are two words that make Tetris so appealing to players initially.



Also visit my webpage; Pacman Advanced

6:14 PM  
Anonymous Vimax Asli anasema...

Nice blog and article, thanks for sharing

11:41 AM  

Post a Comment

<< Rudi mwanzo

KUHUSU MIMI

JINA:Hawra Shamte
MAKAZI:Dar es salaam
NCHI:Tanzania
KAZI:Mwandishi

KUELEKEA BUNGE LA BAJETI 2006

QuickTopic free message boards
Bonyeza hapa ili uweze kuelezea: NINI MTAZAMO WAKO JUU YA BAJETI IJAYO YA MWAKA 2006/07 NCHINI TANZANIA?

VYOMBO VYA HABARI MTANDAONI

  • The Citizen
  • Mwananchi
  • Mwanaspoti
  • Business Times
  • Majira
  • Daily News
  • Nipashe
  • The Guardian
  • The Express
  • Kiongozi
  • Uhuru/Mzalendo
  • Arusha Times
  • BLOGI ZA KISWAHILI

  • Bangaiza
  • Mwandani
  • Pambazuko
  • Damija
  • Mtafiti
  • Martha
  • Gaphiz
  • Swahili time
  • Miruko
  • Dira yangu
  • Msangimdogo
  • Jeff Msangi
  • Kasri la mwanazuoni
  • Kurunzi
  • Baragumu
  • Mawazohuru
  • Fikra Thabiti
  • Mtandaoni
  • Motowaka
  • Mkwinda
  • Ngurumo
  • Nyembo
  • Bwaya
  • Omega
  • Tafakari za Maisha
  • Nuru akilini
  • Mtandawazi
  • Mhujumu
  • Vijimamboz
  • Wakati wa Ukombozi
  • Kijiwe Joto
  • Watoto Wetu
  • Jungu kuu
  • Kisima cha Weledi
  • Jarida la Ughaibuni
  • Bhalezee
  • Sauti ya Baragumu
  • Kona yangu
  • Furahia Maisha
  • Bakanja
  • Terrie Swai
  • Fatma Karama
  • Kazonta
  • Binti Afrika
  • Blogu ya Kilimo
  • Ukombozi
  • Mwafrika
  • Digital Africa
  • Blogu ya lugha mseto
  • BLOGI ZA WAAFRIKA

  • BLOGAFRICA
  • BLOGU ZA WAAFRIKA
  • DIGITAL AFRICA
  • MAMA JUNKYARD'S
  • MSHAIRI
  • KENYAN PUNDIT
  • MONGI DREAMS
  • ISARIA MWENDE
  • CUNNING LINGUISTICA
  • ETHIOPUNDIT
  • MOCHALICIOUS
  • UNGANISHA
  • DEMOKRASIA KENYA
  • CHANUKA
  • BANKELE
  • MAARIFA/AKIEY
  • AFROMUSING
  • NEHANDA DREAMS
  • BLACK LOOKS
  • YUMMY WAKAME
  • AFRICAN OIL POLITICS
  • NUBIAN SOUL
  • SANAA
  • VIRTUAL INSANITY
  • MENTAL ACROBATICS
  • KENYA UNLIMITED
  • JIKUMBUSHE KAZI ZANGU ZA ZAMANI

    April 2006 May 2006 June 2006 October 2007 November 2007 December 2007 May 2008 July 2008 October 2008 July 2009 August 2012 October 2012

    Imetengenezwa na

    Ukibofya hapa utapelekwa katika Blogi ya msangimdogo

    na inawezeshwa na