" Jamii iliyostaarabika ni yenye kuheshimu Mawazo & Mitazamo ya wengine. Mchango wako katika kazi yoyote ulenge kujenga jamii yenye Kujitambua, Kujithamini na Kujiwajibisha "

 
Thursday, October 04, 2012

 CCM, kazi ya kupiga tantararira waachieni wapinzani

CCM, kazi ya kupiga ‘tantararira’ waachieni wapinzani


Hawra Shamte

WIKI iliyopita Dodoma palikuwa hapatoshi, palitaka kuchimbika bila jembe. Lakini mwishowe kilieleweka! Napenda kuchukua fursa hii kukipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa kufanya uchaguzi wake wa ndani.

Kilichonifurahisha zaidi ni pale Mwenyekiti alipoweka bayana kuwa ‘mtu mzima hatishiwi nyau! Wale wote waliokuwa wakitingisha kibiriti, walikuta kimejaa!

Mwenyekiti alisema anayetaka kuondoka CCM aondoke, kwani bila shaka atakuwa ameshajiandalia pakwenda. Kwa msisitizo zaidi alisema wanaotaka CCM ife, watakufa wao! Duh! Hilo nalo neno!

Lakini nilichojifunza ni kuwa kumbe yawezekana kufanya mabadiliko kama dhamira ikiwa ya dhati. Walisema kuwa wanataka kubadili safu ya uongozi, ikibidi vijana waingie kwa wingi zaidi na wazee waachie nafasi.

CCM hawakuwatoa wazee kwa fujo, bali wanawaengua taratibu kimkakati. Mlichofanya Dodoma tumekiona, lakini bila shaka haitoshi kubadilisha rangi ya chupa, mvinyo ikabaki ileile.

Ingawa ni Chama chenu, lakini nadhani kama kwamba Watanzania wengine pia wanayo haki ya kusema na kutoa ushauri kwa sababu hicho ni Chama Tawala. Serikali yetu inaongozwa na sera za Chama Cha Mapinduzi, hivyo wananchi wote kwa namna moja ama nyingine tunayo haki ndani ya chama tawala.

Kwa kuwa hatupati fursa ya kuingia ndani ya vikao vya Chama, lakini nafikiri kuwa sisi tunaruhusiwa kutoa mawazo yetu kwa kutumia majukwaa mengine na tunatarajia kuwa mawazo yetu yatatiliwa maanani.

CCM kubadilisha safu ya uongozi ni jambo moja, lakini jambo la pili ambalo lina umuhimu sawa na lile la kwanza nafikiri ni kubadilisha dira na mwelekeo.

CCM inachofanya ni kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa kupanga safu safi! Lakini haitoshi, kwani yapo mambo ambayo CCM inapaswa iige kutoka kwa vyama vingine, nayo ni ule mshawasha na moto wa mabadiliko.

Mabadiliko haya yasiwe ya nadharia, bali yawe ya vitendo. Kama CCM iliweza kudhibiti faulo katika uchaguzi wake wa ndani, tunatarajia itafanya hivyo hivyo katika Uchaguzi Mkuu wa vyama vingi. Mizengwe na rushwa iwe mwisho wake umefika! Kwa kuwa CCM ndiyo kinara, kinapaswa kiwe ndicho kiigizo chema kwa vyama vingine.

Ninachoweza kusema ni kuwa CCM ina kazi kubwa ya kujirudisha katika mioyo ya wakulima na wafanyakazi, katika mioyo ya walalahoi na wapenda haki, kinyume cha hivyo kitaendelea kurukishwa kichura na vyama vinavyofahamu kutumia mtaji wa walalahoi.

Tunatarajia kuiona CCM ikiyaona matatizo yake kama changamoto na iweke dhamira ya dhati ya kuzifanyia kazi changamoto hizo.

Athari ya mabadiliko ndani ya CCM inapaswa ionekane mpaka ndani ya Serikali, kwani Serikali iliyopo madarakani inaongozwa na CCM.

Kwa muda huu mchache wa miaka mitatu kasorobo, wananchi wangependa kuona mabadiliko ya dhati yakifanyika kwa watendaji wa Serikali. Dhamira za kutokomeza rushwa zitekelezwe, azma za kupambana na ubadhirifu wa mali za umma zitimizwe na shabaha na malengo ya kumpatia maisha bora kila Mtanzania yaelekezwe panapostahili, mwananchi angalau aone mwanga wa maisha yake, ajue anakoelekea, apate matumaini mapya, hiyo ndiyo dawa pekee ya kurudisha imani ya wananchi kwa CCM.

Dhamira ya dhati ya kumkomboa Mtanzania inapaswa itekelezwe kwa vitendo, kazi ya kupiga ‘tantararira’ (kupiga domo) waachiwe wengine kwa sababu hiyo ndiyo kazi yao, kwa kuwa hawana Serikali ya kuiendesha.

Ahadi za ajira zisiwe za kutiana hasira, kwa sababu tunaona jinsi vigogo wanavyopendeleana, jinsi nafasi za ajira zinavyokwenda kwa watoto wa wakubwa. Tunaona jinsi vijana wetu wanaomaliza vyuo na kuhangaika mitaani, wanavyoambiwa wajiajiri wakati hawajui hata wataanzaje.

Nafasi za kazi zinazotolewa zinaelezwa wazi kuwa anahitajika mtu mwenye uzoefu wa miaka isiyopungua mitatu; huyu kijana aliyemaliza chuo mwaka huu, uzoefu ataupata wapi na vipi? Hizi tulizonazo ni sera za kukwazana!

Wananchi wanaoumia kwa jasho, wanaotembea Azimio la Arusha kwa kukosa nauli za daladala, wanaoingia kwenye daladala na kubanana kama mishikaki, wanaoumiza vichwa kupanga bajeti ya siku, isiyopangika, ndio wanaoujua uhondo wa ngoma!

Kimsingi hawa hawahitaji kujazwa mapesa mifukoni, bali wanachohitaji ni kuboreshewa huduma zote muhimu, maji, afya, elimu na usafiri.

Kadhalika hata mazingira ya uwajibikaji nayo yaboreshwe, biashara zao wazifanye kwa wasaa na ikibidi wapunguziwe kodi na ushuru.

Kwenye sekta ya kilimo wakulima wapelekewe pembejeo na wapewe elimu ya kilimo cha kisasa, maafisa ugani waache kukaa ofisini, waende vijijini kuwahudumia wakulima.

Tunaona jitihada katika barabara, lakini bado tunahitaji mtandao mpana zaidi wa barabara hadi vijijini.

Miaka 50 baada ya Uhuru bado ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndio wanaopata umeme, hivyo jitihada zaidi za kuzalisha umeme na kuusambaza zinahitajika.

Tusitegemee tu chanzo cha aina moja cha kuzalisha umeme, inawezekana kutumia vyanzo vingine ambavyo tunavyo, Serikali sasa inapaswa ibadilike; badala ya kuchukua taarifa za kitaalamu na kuziweka kwenye makabrasha na kisha kuziweka kabatini, sasa ripoti hizo zifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.

Kupanga ni kuchagua, tukichagua vyema vipaumbele vyetu tutaweza kufikia malengo. Tuache kuweka vipaumbele saba katika mipango mikakati yetu ya maendeleo. Tuwe na vipaumbele vichache, tulivyovipanga vyema ambavyo tunaweza kuvitekeleza kutokana na rasilimali tulizonazo.

Dhamira peke yake bila vitendo haikidhi haja, tupunguze ahadi, tufanye kazi! Inawezekana, kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake!

0655 849694





 CCM, kazi ya kupiga tantararira waachieni wapinzani

CCM, kazi ya kupiga ‘tantararira’ waachieni wapinzani


Hawra Shamte

WIKI iliyopita Dodoma palikuwa hapatoshi, palitaka kuchimbika bila jembe. Lakini mwishowe kilieleweka! Napenda kuchukua fursa hii kukipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa kufanya uchaguzi wake wa ndani.

Kilichonifurahisha zaidi ni pale Mwenyekiti alipoweka bayana kuwa ‘mtu mzima hatishiwi nyau! Wale wote waliokuwa wakitingisha kibiriti, walikuta kimejaa!

Mwenyekiti alisema anayetaka kuondoka CCM aondoke, kwani bila shaka atakuwa ameshajiandalia pakwenda. Kwa msisitizo zaidi alisema wanaotaka CCM ife, watakufa wao! Duh! Hilo nalo neno!

Lakini nilichojifunza ni kuwa kumbe yawezekana kufanya mabadiliko kama dhamira ikiwa ya dhati. Walisema kuwa wanataka kubadili safu ya uongozi, ikibidi vijana waingie kwa wingi zaidi na wazee waachie nafasi.

CCM hawakuwatoa wazee kwa fujo, bali wanawaengua taratibu kimkakati. Mlichofanya Dodoma tumekiona, lakini bila shaka haitoshi kubadilisha rangi ya chupa, mvinyo ikabaki ileile.

Ingawa ni Chama chenu, lakini nadhani kama kwamba Watanzania wengine pia wanayo haki ya kusema na kutoa ushauri kwa sababu hicho ni Chama Tawala. Serikali yetu inaongozwa na sera za Chama Cha Mapinduzi, hivyo wananchi wote kwa namna moja ama nyingine tunayo haki ndani ya chama tawala.

Kwa kuwa hatupati fursa ya kuingia ndani ya vikao vya Chama, lakini nafikiri kuwa sisi tunaruhusiwa kutoa mawazo yetu kwa kutumia majukwaa mengine na tunatarajia kuwa mawazo yetu yatatiliwa maanani.

CCM kubadilisha safu ya uongozi ni jambo moja, lakini jambo la pili ambalo lina umuhimu sawa na lile la kwanza nafikiri ni kubadilisha dira na mwelekeo.

CCM inachofanya ni kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa kupanga safu safi! Lakini haitoshi, kwani yapo mambo ambayo CCM inapaswa iige kutoka kwa vyama vingine, nayo ni ule mshawasha na moto wa mabadiliko.

Mabadiliko haya yasiwe ya nadharia, bali yawe ya vitendo. Kama CCM iliweza kudhibiti faulo katika uchaguzi wake wa ndani, tunatarajia itafanya hivyo hivyo katika Uchaguzi Mkuu wa vyama vingi. Mizengwe na rushwa iwe mwisho wake umefika! Kwa kuwa CCM ndiyo kinara, kinapaswa kiwe ndicho kiigizo chema kwa vyama vingine.

Ninachoweza kusema ni kuwa CCM ina kazi kubwa ya kujirudisha katika mioyo ya wakulima na wafanyakazi, katika mioyo ya walalahoi na wapenda haki, kinyume cha hivyo kitaendelea kurukishwa kichura na vyama vinavyofahamu kutumia mtaji wa walalahoi.

Tunatarajia kuiona CCM ikiyaona matatizo yake kama changamoto na iweke dhamira ya dhati ya kuzifanyia kazi changamoto hizo.

Athari ya mabadiliko ndani ya CCM inapaswa ionekane mpaka ndani ya Serikali, kwani Serikali iliyopo madarakani inaongozwa na CCM.

Kwa muda huu mchache wa miaka mitatu kasorobo, wananchi wangependa kuona mabadiliko ya dhati yakifanyika kwa watendaji wa Serikali. Dhamira za kutokomeza rushwa zitekelezwe, azma za kupambana na ubadhirifu wa mali za umma zitimizwe na shabaha na malengo ya kumpatia maisha bora kila Mtanzania yaelekezwe panapostahili, mwananchi angalau aone mwanga wa maisha yake, ajue anakoelekea, apate matumaini mapya, hiyo ndiyo dawa pekee ya kurudisha imani ya wananchi kwa CCM.

Dhamira ya dhati ya kumkomboa Mtanzania inapaswa itekelezwe kwa vitendo, kazi ya kupiga ‘tantararira’ (kupiga domo) waachiwe wengine kwa sababu hiyo ndiyo kazi yao, kwa kuwa hawana Serikali ya kuiendesha.

Ahadi za ajira zisiwe za kutiana hasira, kwa sababu tunaona jinsi vigogo wanavyopendeleana, jinsi nafasi za ajira zinavyokwenda kwa watoto wa wakubwa. Tunaona jinsi vijana wetu wanaomaliza vyuo na kuhangaika mitaani, wanavyoambiwa wajiajiri wakati hawajui hata wataanzaje.

Nafasi za kazi zinazotolewa zinaelezwa wazi kuwa anahitajika mtu mwenye uzoefu wa miaka isiyopungua mitatu; huyu kijana aliyemaliza chuo mwaka huu, uzoefu ataupata wapi na vipi? Hizi tulizonazo ni sera za kukwazana!

Wananchi wanaoumia kwa jasho, wanaotembea Azimio la Arusha kwa kukosa nauli za daladala, wanaoingia kwenye daladala na kubanana kama mishikaki, wanaoumiza vichwa kupanga bajeti ya siku, isiyopangika, ndio wanaoujua uhondo wa ngoma!

Kimsingi hawa hawahitaji kujazwa mapesa mifukoni, bali wanachohitaji ni kuboreshewa huduma zote muhimu, maji, afya, elimu na usafiri.

Kadhalika hata mazingira ya uwajibikaji nayo yaboreshwe, biashara zao wazifanye kwa wasaa na ikibidi wapunguziwe kodi na ushuru.

Kwenye sekta ya kilimo wakulima wapelekewe pembejeo na wapewe elimu ya kilimo cha kisasa, maafisa ugani waache kukaa ofisini, waende vijijini kuwahudumia wakulima.

Tunaona jitihada katika barabara, lakini bado tunahitaji mtandao mpana zaidi wa barabara hadi vijijini.

Miaka 50 baada ya Uhuru bado ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndio wanaopata umeme, hivyo jitihada zaidi za kuzalisha umeme na kuusambaza zinahitajika.

Tusitegemee tu chanzo cha aina moja cha kuzalisha umeme, inawezekana kutumia vyanzo vingine ambavyo tunavyo, Serikali sasa inapaswa ibadilike; badala ya kuchukua taarifa za kitaalamu na kuziweka kwenye makabrasha na kisha kuziweka kabatini, sasa ripoti hizo zifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.

Kupanga ni kuchagua, tukichagua vyema vipaumbele vyetu tutaweza kufikia malengo. Tuache kuweka vipaumbele saba katika mipango mikakati yetu ya maendeleo. Tuwe na vipaumbele vichache, tulivyovipanga vyema ambavyo tunaweza kuvitekeleza kutokana na rasilimali tulizonazo.

Dhamira peke yake bila vitendo haikidhi haja, tupunguze ahadi, tufanye kazi! Inawezekana, kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake!

0655 849694





Wednesday, August 22, 2012


Na watajwe ili wakome kutufisidi na kutufilisi


Hawra Shamte

NAKUBALIANA kwa asilimia 100 na ushauri wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kwamba waliohusika na kuhamisha fedha nchini na kuzipeleka nje ya nchi kuzificha watajwe. Nami naungana naye kushangaa kwa nini hawatajwi?

Nashangaa kwa sababu hii si silika ya Watanzania kunyamazia uovu au kutishika kuusema uovu au kuogopa kuwaadhiri waovu.

Kwanini waovu hawatajwi? Kwanini tumekuwa tukitishia tu kuwataja watu ambao tunasema tunao ushahidi wa kutosha kuwa wanaifisidi nchi, wanahawilisha rasilimali za nchi.

Wanaohamisha fedha nchini na kuzipeleka kuzihifadhi katika benki za nje, hata kama ni fedha zao na tujaalie kuwa wamezipata kihalali, lakini kimsingi hawa ni wahujumu wa uchumi wa nchi.

Ikiwa uchumi wa taifa masikini kama Tanzania unategemea mzunguko wa dola ya Marekani, inakuwaje mtu mmoja anachukua mamilioni ya dola (anayodai kuwa ni yake) na kwenda kuyaweka katika benki ya Uswisi au kwengineko kokote kulikovunjwa shoka mpini ukabaki?

Anachofanya ni kukandamiza mzunguko wa fedha nchini kwake na kwenda kuimarisha mzunguko wa fedha wa nchi zilizoendelea.

Hii ni tabia ya uchoyo na ulafi, ikiwa mtu umepata inakuwaje hutaki na mwenzako apate? Huyu angeweka mabilioni yake ya fedha nchini, si yangetusaidia wengi kama yalivyotusaidia mabilioni ya Kikwete?

Kwa sababu kinachofanyika ni kuongeza uwezo wa benki wa kukopesha wateja wake, kwa kuwa benki inakuwa na wateja wakubwa wanaoingiza fedha nyingi zinazokaa kwa muda mrefu bila kazi.

Pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa sheria ya uhujumu uchumi, pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa kuulizwa wamepata wapi hivyo ‘vijisenti.’ Lakini kama wamezipata fedha hizo kwa njia halali kwanini waogope?

Nadhani umefika wakati Watanzania tukatae kugawana umasikini, kama baadhi yetu wanao utajiri walioupata kwa nguvu zao, kwanini waogope kujidhihirisha kama wao wana fedha na kisha fedha zao waziweke pahali panapotambulika kisheria.

Hawa akili zao na roho zao ni mbaya kuliko wale waliokuwa wakifukia magunia ya fedha chini ya ardhi wakati wa uhujumu uchumi. Wanaofanya hivi bila shaka ni wezi, wanaogopa kugundulika kama wana mabilioni ya fedha wasiyoweza kuyaelezea jinsi walivyoyapata.

Lakini hii tabia ya kuficha ukweli haikuanza leo, wala si wabunge tu wanaohofia kuuweka wazi ukweli, kwani hata viongozi wetu kadhaa serikalini katika kadhia tofauti tumeshawasikia wakisema kuwa wahalifu wanawafahamu lakini wanawapa muda wajirekebishe.

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema kuwa amepelekewa orodha ya wauza unga, lakini anawapa muda mpaka Krismasi, ikimalizika atawashughulikia...

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema anawajua waliojichukulia na kujihodhia fedha za Madeni ya Nje za Benki Kuu (EPA) lakini akawapa muda wazirejeshe...

Hii imekuwa ndiyo tabia, yamekuwa ndiyo mazoea, umekuwa ndio utamaduni mpya tulioamua kuufuata; utamaduni wa kuwahifadhi waovu, utamaduni wa kutowataja wezi, utamaduni wa kuwaonea haya wahalifu, utamaduni wa kuwapa muda wajirekebishe.

Wengine wamejifunza utamaduni wa kuwavumilia wanaowachafua, lakini hili la kutowataja wanaofisidi mali ya umma, wanaohawilisha rasilimali za taifa, hapa tumekithiri ada!

Wanahamisha nyara za taifa, wanasafirisha mpaka wanyama tunawavumilia, tunawaangalia tu. Wanachimba madini yetu, wanatuachia mashimo yasiyozibika, sisi tupo tunawaangalia tu, eti tunajivunia amani na utulivu.

Ni amani gani aliyonayo mtu anayeishi kwa mlo mmoja kwa siku? Ni amani gani anayoipata mtu anayetafuta maji kuanzia saa nane za usiku mpaka saa 6 mchana, anasubiri chemchem ifumuke, achote kwa kata, tena kwa utulivu ili asiyachafue? Haya ndiyo maji anayotarajia kwenda kunywa yeye na familia yake. Anafanya hivyo kwa sababu ahadi ya kupelekewa maji hadi kwenye kaya yake bado haijatekelezwa kwa sababu Serikali haina fedha, lakini Serikali hiyohiyo inawaangalia baadhi ya wananchi wake na hata wawekezaji iliyowaalika waje nchini kuwekeza, wakihamisha rasilimali za taifa.

Ni utulivu gani anaoupata mama mjamzito ambaye katika zama hizi zenye maradhi ya kuambukiza ya kila aina, anapokwenda hospitalini kujifungua anakuta wanalazwa watatu katika kitanda kimoja?

Ni utulivu gani anaokuwa nao mwanafunzi wetu wa shule ya msingi pale anapoketi sakafuni na kuandika kwenye daftari lake hali ya kuwa amepinda mgongo na kukunja miguu?

Kwa hali hii ya kutodhibiti mali ya umma, hali ya kuwaacha wachache wakifaidi keki ya taifa, hali ya kuwaacha walafi wakikomba mboga yote na kuwaacha watoto wetu wakiwa na utapiamlo; kiasi kiongozi wetu aseme Tanzania ina rasilimali nyingi, lakini hajui kwanini bado ni masikini.

Atajuaje? Wakati wanayoyafanya hayo wanafanya kwa kificho? Wakati wanahamisha mamilioni ya fedha kwenda kuyaficha nje ya nchi kama wezi? Wakati watu hawako wazi na wala si wa kweli?

Masikini Tanzania imegeuzwa shamba la bibi, tena bibi mwenyewe keshafariki, shamba halina msimamizi, wajukuu wanajichumia hata vilivyo vichanga, visivyopea wanavipepea kwa moto, wanahamisha badala ya kula wao au hata kuwaruhusu wenzao kujichumia na kukidhi njaa, hamu na kuondosha ghamu zao. Hii ni hatari!


0655 849694






Na watajwe ili wakome kutufisidi na kutufilisi


Hawra Shamte

NAKUBALIANA kwa asilimia 100 na ushauri wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kwamba waliohusika na kuhamisha fedha nchini na kuzipeleka nje ya nchi kuzificha watajwe. Nami naungana naye kushangaa kwa nini hawatajwi?

Nashangaa kwa sababu hii si silika ya Watanzania kunyamazia uovu au kutishika kuusema uovu au kuogopa kuwaadhiri waovu.

Kwanini waovu hawatajwi? Kwanini tumekuwa tukitishia tu kuwataja watu ambao tunasema tunao ushahidi wa kutosha kuwa wanaifisidi nchi, wanahawilisha rasilimali za nchi.

Wanaohamisha fedha nchini na kuzipeleka kuzihifadhi katika benki za nje, hata kama ni fedha zao na tujaalie kuwa wamezipata kihalali, lakini kimsingi hawa ni wahujumu wa uchumi wa nchi.

Ikiwa uchumi wa taifa masikini kama Tanzania unategemea mzunguko wa dola ya Marekani, inakuwaje mtu mmoja anachukua mamilioni ya dola (anayodai kuwa ni yake) na kwenda kuyaweka katika benki ya Uswisi au kwengineko kokote kulikovunjwa shoka mpini ukabaki?

Anachofanya ni kukandamiza mzunguko wa fedha nchini kwake na kwenda kuimarisha mzunguko wa fedha wa nchi zilizoendelea.

Hii ni tabia ya uchoyo na ulafi, ikiwa mtu umepata inakuwaje hutaki na mwenzako apate? Huyu angeweka mabilioni yake ya fedha nchini, si yangetusaidia wengi kama yalivyotusaidia mabilioni ya Kikwete?

Kwa sababu kinachofanyika ni kuongeza uwezo wa benki wa kukopesha wateja wake, kwa kuwa benki inakuwa na wateja wakubwa wanaoingiza fedha nyingi zinazokaa kwa muda mrefu bila kazi.

Pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa sheria ya uhujumu uchumi, pengine wanafanya hivyo kwa kuogopa kuulizwa wamepata wapi hivyo ‘vijisenti.’ Lakini kama wamezipata fedha hizo kwa njia halali kwanini waogope?

Nadhani umefika wakati Watanzania tukatae kugawana umasikini, kama baadhi yetu wanao utajiri walioupata kwa nguvu zao, kwanini waogope kujidhihirisha kama wao wana fedha na kisha fedha zao waziweke pahali panapotambulika kisheria.

Hawa akili zao na roho zao ni mbaya kuliko wale waliokuwa wakifukia magunia ya fedha chini ya ardhi wakati wa uhujumu uchumi. Wanaofanya hivi bila shaka ni wezi, wanaogopa kugundulika kama wana mabilioni ya fedha wasiyoweza kuyaelezea jinsi walivyoyapata.

Lakini hii tabia ya kuficha ukweli haikuanza leo, wala si wabunge tu wanaohofia kuuweka wazi ukweli, kwani hata viongozi wetu kadhaa serikalini katika kadhia tofauti tumeshawasikia wakisema kuwa wahalifu wanawafahamu lakini wanawapa muda wajirekebishe.

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema kuwa amepelekewa orodha ya wauza unga, lakini anawapa muda mpaka Krismasi, ikimalizika atawashughulikia...

Tumeshawahi kumsikia kiongozi akisema anawajua waliojichukulia na kujihodhia fedha za Madeni ya Nje za Benki Kuu (EPA) lakini akawapa muda wazirejeshe...

Hii imekuwa ndiyo tabia, yamekuwa ndiyo mazoea, umekuwa ndio utamaduni mpya tulioamua kuufuata; utamaduni wa kuwahifadhi waovu, utamaduni wa kutowataja wezi, utamaduni wa kuwaonea haya wahalifu, utamaduni wa kuwapa muda wajirekebishe.

Wengine wamejifunza utamaduni wa kuwavumilia wanaowachafua, lakini hili la kutowataja wanaofisidi mali ya umma, wanaohawilisha rasilimali za taifa, hapa tumekithiri ada!

Wanahamisha nyara za taifa, wanasafirisha mpaka wanyama tunawavumilia, tunawaangalia tu. Wanachimba madini yetu, wanatuachia mashimo yasiyozibika, sisi tupo tunawaangalia tu, eti tunajivunia amani na utulivu.

Ni amani gani aliyonayo mtu anayeishi kwa mlo mmoja kwa siku? Ni amani gani anayoipata mtu anayetafuta maji kuanzia saa nane za usiku mpaka saa 6 mchana, anasubiri chemchem ifumuke, achote kwa kata, tena kwa utulivu ili asiyachafue? Haya ndiyo maji anayotarajia kwenda kunywa yeye na familia yake. Anafanya hivyo kwa sababu ahadi ya kupelekewa maji hadi kwenye kaya yake bado haijatekelezwa kwa sababu Serikali haina fedha, lakini Serikali hiyohiyo inawaangalia baadhi ya wananchi wake na hata wawekezaji iliyowaalika waje nchini kuwekeza, wakihamisha rasilimali za taifa.

Ni utulivu gani anaoupata mama mjamzito ambaye katika zama hizi zenye maradhi ya kuambukiza ya kila aina, anapokwenda hospitalini kujifungua anakuta wanalazwa watatu katika kitanda kimoja?

Ni utulivu gani anaokuwa nao mwanafunzi wetu wa shule ya msingi pale anapoketi sakafuni na kuandika kwenye daftari lake hali ya kuwa amepinda mgongo na kukunja miguu?

Kwa hali hii ya kutodhibiti mali ya umma, hali ya kuwaacha wachache wakifaidi keki ya taifa, hali ya kuwaacha walafi wakikomba mboga yote na kuwaacha watoto wetu wakiwa na utapiamlo; kiasi kiongozi wetu aseme Tanzania ina rasilimali nyingi, lakini hajui kwanini bado ni masikini.

Atajuaje? Wakati wanayoyafanya hayo wanafanya kwa kificho? Wakati wanahamisha mamilioni ya fedha kwenda kuyaficha nje ya nchi kama wezi? Wakati watu hawako wazi na wala si wa kweli?

Masikini Tanzania imegeuzwa shamba la bibi, tena bibi mwenyewe keshafariki, shamba halina msimamizi, wajukuu wanajichumia hata vilivyo vichanga, visivyopea wanavipepea kwa moto, wanahamisha badala ya kula wao au hata kuwaruhusu wenzao kujichumia na kukidhi njaa, hamu na kuondosha ghamu zao. Hii ni hatari!


0655 849694





Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

Ajali ya Skagit: Haya ni matokeo ya taifa linalopenda mitumba


Hawra Shamte

Ilikuwa Septemba 10, 2011 ilipotokea ajali ya meli katika bahari ya Hindi, eneo la Nungwi Zanzibar.
Kumbukumbu na taswira bado hazijaondoka vichwani mwa Watanzania. Maumivu ya mioyo kila wanapowakumbuka vipenzi vyao, ndugu, jamaa na rafiki zao na hata Watanzania wenzao waliopoteza maisha katika ile ajali ya MV Spice Islander iliyoua zaidi ya watu 200.

Ajali ile ilituduwaza. Mengi yalisemwa, tafakuri nyingi zilidadavuliwa. Ingawa ajali haina kinga, lakini Waswahili wanasema tahadhari kabla ya athari.Tulidhani tumejifunza, au tumejirekebisha, lakini afanalek, ajali nyingine kama ile imetokea, Julai 18, 2012, tofauti ni aina ya meli na eneo meli ilipozama.

Kwa kawaida akipoteza maisha hata mtu mmoja kwa ajali zinazoweza kuzuilika, watu wenye akili murua lazima waingie simanzi, wajilaumu na waazimie kujikinga na ajali.

Tulidhani ajali ya Mv Spice Islander ilitupa fundisho, tuache kujaza abiria kwenye vipando. Tulidhani ajali ile ilitufunza kuchukua hatua za tahadhari zote zinazopaswa kuchukuliwa na vyombo vya majini. Tulidhani mamlaka husika zimetanabahi na kubaini makosa yanayotendeka katika sekta ya usafiri wa majini.

Tulidhani ripoti ya Tume iliyoundwa mara baada ya ajali ya Mv Spice Islander ingefanyiwa kazi badala ya kuwekwa kwenye majalada na juu ya mashubaka na kuziacha ziote vumbi, au kubaki kuwa historia isiyozingatiwa.

Tulidhani kwa kuwa tuliambiwa lililopita si ndwele, tungeganga yajayo, tatizo hili hata kama lingejirudia, lisingejirudia mapema hivi, angalau tungekuwa tumeliganga kidogo hata kama ikiwa hatukuliponya.

Mara hii ajali imetokea upande wa pili wa mkondo, imetokea katika mkondo wa Chumbe eneo la Pungume, kilomita 48 kutoka bandari ya Zanzibar.

Boti iliyozama mara hii ni Skagit inayomilikiwa na kampuni ya Seagull. Yenyewe pia ilibeba zaidi ya uwezo wake, yasemekana kuwa uwezo wake ni kubeba abiria 200. Yenyewe ilibeba watu 291 mbali na mizigo. Hadi jana Alhamisi taarifa zilisema kuwa waliookolewa walikuwa 142, waliopotea 113, waliopatikana wakiwa wamefariki ni 36. Kwa hesabu za harakaharaka ni kuwa watu takriba 150 wamejongomea.

Pamoja na maafa yote hayo, itakachofanya Serikali ni kuunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali, je, inasaidia nini? Wakati tulipaswa kuunda Tume za kupanga mikakati ya jinsi ya kukinga ajali, lakini sisi tunaunda tume baada ya madhara kutokea.

Kwa kuwa sisi wanadamu ni wenye mazingatio, tulidhani Mv Spice Islander ingekuwa imetupa mazingatio, lakini masikini kwa vile sisi ni ‘zumbukuku,’ maisha yetu, taratibu zetu na mienendo yetu mibovu tuliendelea nayo kama kwamba hakuna kilichotokea, lililopita limepita.

Vyombo vyetu vingi vya uysafirishaji viko chini ya kiwango, kwa sababu kama ambavyo wengi wetu hatununui magari mapya, vilevile hatununui meli mpya wala ndege mpya, zaidi pia hatununui hata nguo mpya, tumeligeuza taifa letu kuwa taifa la mitumba, hizi tunazoziona sasa ndiyo athari zake.

Sisemi kama kipya hakizami (kwani Mv Titanic) ilizama ikiwa mpya wakati wa safari yake ya kwanza baharini. Lakini sote tunajua madhara ya vikuukuu, vijembe vilivyokongoka mpini, sisi tunavichukua na kuviweka vibanio.

Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka hata ukiona unyasi utauogopa, lakini sisi hatuogopi nyoka wa aina yoyote yule, maisha kwetu kila siku yanakwenda kama kawaida, kwetu maisha ni mazoea si mabadiliko wala maendeleo.

Mwanzoni mwa miaka ya 70 wakati serikali zilipokuwa zikitoa huduma, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa ikitoa huduma za usafirishaji. Ilirithi meli za Mv Afrika na Mv Jamhuri, zilipochakaa ilinunua meli ya Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo. Aliyepanda Mv Mapinduzi na Mv Maendeleo atakuwa anafahamu jinsi zilivyokuwa. Zilikuwa meli kubwa, nzuri na madhubuti, hivyo usafiri wa baharini ulikuwa wa uhakika zaidi.

Baada ya serikali kuacha jukumu lake la kutoa huduma za usafiri, hivi sasa usafiri wa baharini kama ulivyo usafiri wa nchi kavu umekuwa shaghala baghala, kila mwenye mkweche wake anauingiza baharini au barabarani bila kujali kwamba anacheza na roho za watu.

Serikali zetu zipo, zimenyamaza kimya kama kwamba zinaridhika na hali inayoendelea. Kazi ya serikali sasa imekuwa ni kuboresha miundombinu ya barabara tu, haina habari ya vipando.

Waliopewa mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nao kama wamelala usingizi, na hata kama wameamka, bila shaka wakiminyiwa mkono kwa makosa ya wasafirishaji, wao wanaufumbata. Hivyo makosa ya usafirishaji ni vigumu kumalizika nchini, kwa sababu Watanzania tumejifunza tabia ya kufumbia macho maovu.

Kama wameshtushwa kutoka usingizini, ati Sumatra jana (Alhamisi) ilikataza boti za asubuhi zisisafiri hadi zikaguliwe. Tahadhari inachukuliwa baada ya hatari, na hilo litafanyika kwa muda mchache tu, halafu Watanzania watazoea na watasahau, maisha yataendelea kama kawaida.

Tunaikumbuka hekaheka ya vidhibiti mwendo kwenye magari ya abiria, je, iliishia wapi? Baada ya hashuo kumalizika, kila msafirishaji akaendelea na mazoea, ajali zinatokea kama kawaida kwa sababu tunaamini kuwa ajali hazina kinga, lakini wakati huo huo tunatambua kuwa ziko tahadhari za kuchukua kabla ya ajali lakini sisi tunazipuuzia.

Taifa lina kilio, kwa bahati mbaya hakuna anayetuthibitishia kuwa Watanzania karibu tutapata maliwazo, karibu tutahaniwa vilio vyetu, kwani kama hazijaua 100 barabarani zinaua 200 baharini au 1000 majini. Ajali ya Mv Bukoba bado iko mawazoni mwetu, lakini tunaendelea kujipumbaza kama kwamba roho zilizopotea zilistahili kupotea.

Ajali zitokanazo na uzembe hazistahili kuwekewa maneno ya kuliwazwa, hizi ni lazima tuzipige vita kwa nguvu zetu zote, na hii haiko kwa wasafirishaji tu, hata kwa wasafiri; nao wanapaswa wachukue hatua za tahadhari, kama mtu ameliona basi limejaa, hata kama ana haraka, hana sababu ya kung’ang’ania kuingia katika basi hilo; hivyo hivyo kwa wapandaji boti na meli, kama abiria ametambua kuwa tiketi zimekwisha, hana sababu ya kung’ang’ania magendo kwani anapaswa atambue kuwa anaiweka roho yake rehani.

Tunayo mipango na mikakati mingi ya maendeleo, lakini kwa bahati mbaya mipango yetu karibu yote iko mbioni, hivi sasa hizi mbio zinapaswa zifike ukingoni. Tunataka kuona miumbombinu iliyo bora na nyenzo za usafiri zilizo imara, kinyume cha hivyo ni muhali kwa Watanzania kufuta machozi mashavuni mwao, mwaka nenda, mwaka rudi ajali zitatuliza!

0655 849694.

Wednesday, July 22, 2009

 Waislam, jukumu la kuanzisha Mahakama ya Kadhi ni lenu

WIKI iliyopita wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa papo bungeni alisema kwamba serikali haijalitupa suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi, lakini imependekeza kuwa kutokana na suala hilo kuwa la imani, liundiwe mfumo wake ambao hautasimamiwa na dola ili chombo hicho kiendelee kuwa nguzo muhimu ya dini ya Kiislamu.

Pinda amesema kwa kuwa Mahakama ya Kadhi ni suala la imani, hivyo Waislam waiunde katika mfumo wao na serikali itatoa msaada kwa chombo hicho hadi kitakaposimama.

Amesema chombo hicho kikiundwa na kusimamiwa na dola serikali itakuwa inakiona kama chombo chake cha dola tu hivyo haitakuwa imetenda haki kwa Waislam na hata Watanzania kwa ujumla wao.

Waziri Mkuu amesema kwa kuwa inasemwa kwamba Mahakama ya Kadhi, au ofisi ya Kadhi msingi wake ni imani ya dini, hivyo anadhani si busara chombo hicho kikawekwa katika mfumo unaotakiwa kusimamiwa na dola.

Kwa kauli hiyo ya Waziri Mkuu ni wazi kwamba Waislam sasa wanapaswa kukianzisha chombo hicho wao wenyewe na kutafuta utaratibu mwafaka wa kuzifanya sheria na maamuzi yake yakubalike na jamii ya Waislam nchini Tanzania.

Binafsi nakubaliana kwa asilimia 100 na tamko hilo la Waziri Mkuu Pinda, kwani ni wazi kwamba serikali itakapoianzisha mahakama hiyo itabidi iwe ni miongoni mwa vyombo vya serikali na itakayosimamiwa na serikali yenyewe na wala si Waislam.

Serikali mwaka 1968 iliivunja Jumuiya ya Kiislam iliyoitwa East African Muslim African Society (EAMWS) jumuiya iliyoanzishwa na Agakhan na ambayo viongozi wake wengi walikuwa ni wenye asili ya Kiasia. EAMWS kama jina lilivyo ilikuwa ni jumuiya ya Waislam ya Afrika Mashariki.

Baada ya kuona kuwa Waislam wa Tanzania kwa ujumla wao hawawakilishwi vema na EAMWS na kutoa malalamiko kadhaa wa kadhaa, ndipo serikali ilipoifuta jumuiya hiyo na kuwahamasisha viongozi Waislam waliokuwa Serikalini kusimamia kuanzishwa kwa jumuiya nyengine ya Waislam wa Tanzania. Kwa msaada wa Sheikh Abeid Karume na Sheikh Rashid Kawawa waliwakutanisha masheikh wa Kiislam pale Iringa mwaka huo huo 68 na kuanzisha Baraza Kuu la Waislam Tanzania, na kwa kuwa EAMWS ilivunjwa kisheria, mali zote zilizokuwa za EAMWS zilimilikishwa BAKWATA.

Kutokana na insafu hiyo, BAKWATA kwa Waislam ikawa inaonekana kuwa ni chombo cha serikali japokuwa serikali haiwachagulii kiongozi wala haiwalipi mishahara isipokuwa hutoa msaada pale inapoombwa kufanya hivyo.

Kutokana na iktisadi hiyo na pengine matendo yasiyoridhisha au yasiyoisaidia jamii ya Kiislam kwa ujumla wake nchini, ndipo mara baada ya kufunguliwa milango ya mfumo wa kiliberali na ruhusa ya kuanzishwa kwa vyama vya kijamii katika miaka ya 1980, ndipo jumuiya nyingi za Kiislam zikaibuka kama uyoga. Nia ikiwa kuziba mapengo pale ambapo Bakwata imeshindwa na pengine kuwafanya Waislam wawe wamoja zaidi.

Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislam mathalan, lililoanzishwa kwa jitihada za wasomi na masheikh mbalimbali wasiokubaliana na mawazo na matendo ya Bakwata, ilidhaniwa kuwa hilo lingeweza kujenga jumuiya yenye nguvu na kuwaunganisha Waislam wawe na sauti moja. Hadi leo Baraza hilo lina umri wa miaka 15 na bado halijapiga hatua, ndio kwanza linasimama dede na wala jitihada zake za kuunganisha jumuiya na taasisi za kiislam hazijafanikiwa kihivyo.

Jitihada nyingine za Waislam za kuwanyang’anya Bakwata mamlaka yao kwa Waislam nchini, walianzisha Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA). Baraza hilo hadi sasa limebakia Kisarawe tu. Waislam wanapaswa kujiuliza kwanini jitihada zao zinasuasua, watafute mbinu za kujikwamua na waache kuwanyooshea wengine vidole?

Hoja iliyopo ni kwamba ikiwa Waislam hawaipendi Bakwata kwa madai kuwa ni kibaraka wa serikali, itakuwaje kwa Mahakama ya Kadhi endapo itaundwa na kuingizwa katika mfumo wa Serikali? Je, itakuwa ni chombo cha Waislam au chombo cha Serikali?

Binafsi nadhani Waislam walikokotwa na ahadi za kisiasa zilizoanza kutolewa na Augustine Mrema wakati akiwa NCCR Mageuzi na baadaye hoja hiyo kupokwa na CCM. Ukiiangalia kwa undani wake utaona kuwa ni hoja ya kisiasa tu ambayo hujengwa kwa maslahi ya wakati fulani.

Kadhalika kuna madai ya kwamba zipo nchi zenye ofisi ya Kadhi Mkuu na Mahakama ya Kadhi ambazo zinasimamiwa na Serikali, hiyo ni kweli lakini ukiangalia utakuta kwamba idadi ya Waislam katika nchi hizo ni ndogo, hivyo serikali inachofanya ni kulinda haki za wachache (minority rights) lakini katika nchi kama Tanzania ambayo takribani idadi ya Waislam na wasio Waislam inakaribiana, kuunda chombo cha kisheria kitakachosimamiwa na dola kwa maslahi ya dini moja pengine ni hoja yenye ukakasi kidogo.

Ni kweli iko haja ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na ofisi ya Kadhi Mkuu nchini Tanzania lakini si haki kuishinikiza serikali kuanzisha mamlaka hizo, Waislam wenyewe wanapaswa wazianzishe na kuzisimamia, wanachopaswa kuitaka serikali kufanya ni kuzitambua tu kisheria na kutoa msaada pale inapohitajika.

Hata hivyo swali linalojitokeza ni kuwa ni nani atakayemfunga paka kengele? Swali hilo linakuja kwa sababu nchini Tanzania Waislam hawana mamlaka moja wanayoiamini na kuitegemea kusimamia mambo yao, Waislam wamegawanyika si kwa madhehebu tu bali kwa makundi na kwa taasisi mbalimbali ambazo kimsingi nyingi hazikubaliani kimtazamo.

Hawra Shamte ni mhariri wa siasa wa gazeti la Mwananchi.
hshamte@mwananchi.co.tz
0754 849694

Tuesday, July 14, 2009

 Mzimu wa Muungano tusipoutuliza utatukosesha amani

MAFAHALI wawili wakipigana ziumiazo nyasi. Huo ni msemo maarufu wa Kiswahili ambao bila shaka una maana pana. Hivi sasa hapa kwetu kuna mafahali wawili wapiganao, yeyote yule atakayebwagwa au hata ikiwa kila mmoja mwisho wa siku atashika njia yake, lakini ni wazi kwamba nyasi zitakuwa zimegaragazwa. Suala la mafuta ambayo yanadaiwa kuwapo Zanzibar limegeuka mzimu unaokuja na kuondoka, lakini hivi sasa unaonyesha kana kwamba umeamua kubaki kwetu, unatukokoteza, unaturudisha nyuma, unatutia wahka. Kwa kawaida mzimu wowote hutulizwa, hivyo ili na huu usiendelee kutuandama tunapaswa kutafuta njia za kuutuliza, kinyume cha hivyo utatukosesha amani. Suala hili limekuwa likiibuka mara kwa mara kwa sababu tu kwa muda wote limekuwa likishughulikiwa kwa udanganyifu, inaonyesha kana kwamba katika kamati ya kushughulikia kero za Muungano inayoongozwa na Makamu wa Rais wajimbe wakiwemo, Waziri Mkuu kwa upande wa Bara na Waziri Kiongozi kwa upande wa Zanzibar, kuna watu ambao wanaogopana, au labda kuna upande unaouogopa mwingine na kushindwa kuambizana ukweli na kinachobaki ni kutoa ahadi za kisiasa tu zisizo na mwisho, “suala hili tunalishughulikia,” siku zinakwenda, miezi inapita, miaka inakatika, awamu zinabadilika, ahadi hiyo bado ingalipo. Mara hii Wazanzibari wameamua kumtafuna jongoo kwa meno. Kasimama Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Yusuf Himid mbele ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Mkuu wa Shughuli za Serikali ndani ya Baraza, Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha akiwapo na akiwa kimya kumsikiliza. Kwa sauti kubwa na ya hamasa, Himid akasema ‘Wazanzibari tumechoka kuburuzwa katika suala hili, sasa huu ni uamuzi wa Baraza la Mapinduzi kwamba mafuta tunayatoa rasmi katika mambo ya Muungano…” Kiongozi wa mambo ya Serikali Barazani yuko pembeni kaketi, kimya kanyamaza, anang’aa ng’aa macho tu. Hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba Himid kapata baraka zote kutoka kwa wakuu wake kulisema jambo hilo, maana yake ni kwamba sasa watu wanataka kupimana nguvu. “Hii ni serikali ya Mapinduzi ati! Ikiwa hawa wenzetu hawataki kuelewa hivyo, itabidi sasa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itumie uamuzi wa nchi za kimapinduzi katika kuliondoa suala la mafuta na gesi asilia kwenye orodha ya mambo ya Muungano…” Bara nako wakubwa wanasema yao, eti Wazanzibari wanajifurahisha, eti mwenye mamlaka ya kutoa jambo katika Katiba ya Muungano ni Bunge tu. Hee! Kasheshe!Mara hii hapatoshi! Huenda pakachimbika bila sululu. Wazanzibari sasa wameamua kulishughulikia suala la mafuta na pengine mambo mengineyo yaliyoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano kutoka kumi na moja hadi 22, ilikuwaje yakaongezwa? Kwa idhini ya nani? Katika vikao vipi? Hayo ni maswali yanayoulizwa na bado hayajapata majibu labda kwa sababu hakuna mjibuji au hayajibiki. Wazanzibari sasa wanasema katika hili watatumia ukaidi, na kwa ukaidi hawajambo! Kwa ubishi kama wenyeji wa Kigoma, ubishi wao hawishi, wako tayari kukata kole la mnazi ili kuhesabu nazi zilizomo kwa sababu walishindana idadi yake wakati kole likining’inia mnazini, sasa kupata uhakika ni lazima liangushwe ili nazi zihesabiwe watu wote wakiona, huo ndio ukaidi wanaotaka kuuanzisha Wazanzibari na kwa hili husahau tofauti zao za kisiasa, hivi sasa itikadi yao moja tu, Uzanzibari na haki yao katika Muungano, likimalizika hili wataurudia ubishi wao wa zamani ule wa CCM na CUF waliouweka pembeni. Hali hiyo inaonyesha kwamba viongozi wetu wameshindwa kulishughulikia suala hili, lakini kwa kuliacha hivi lilivyo kwa kila mwenye kinywa, sauti na nafasi kusema atakavyo, huenda lisitufikishe popote na badala yake kuzua mgogoro mkubwa au pengine tuseme kwamba sasa mgogoro wa kikatiba utaibuka na hautazimika mpaka zijulikane mbichi na mbivu. Mara kwa mara wataalamu wa masuala ya siasa wamekuwa wakipendekeza kwamba tatizo hilo lianze kutatuliwa katika chanzo chake na si katika matawi, tatizo ni Katiba na Mkataba wa Muungano au pengine tatizo ni Muungano wenyewe. Inashangaza kuona kwamba watawala hawataki na wala hawapendi mambo haya yaguswe, lakini ni vyema yakaguswa na kuzungumzwa leo kuliko kusubiri mpaka ukaidi na mabavu yatumike kwani kwa kuruhusu hayo kutokea, huenda tukagawana mbao! Hiyo ni kuonyesha kwamba subira ya wananchi wa Zanzibar sasa inakaribia kufikia kikomo na hiyo inadhihirishwa kutoka vinywani mwa wawakilishi wao, haya mambo si ya kuyafanyia mzaha kwani Waswahili wanasema; ‘Mzaha mzaha, hutumbuka usaha.’ Binafsi nadhani mpira huu wa masuala ya Muungano sasa unapaswa kuchezwa na wakuu wa nchi husika, wasiachiwe Mansour Himid na Adam Malima kurushiana pasi kali na kuziumiza nyasi, kwani hawa ni vijumbe tu, tunawaomba wahusika waingie uwanjani walisakate kandanda! Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa Gazeti la Mwananchi. hshamte@mwananchi.co.tz 0754 849694

Labels:

 Fikra pevu kamwe haitakufa

NI vigumu kuamini, lakini ni kweli, wakati wake ulifika, aliitwa naye akaitika. Atakumbukwa kwa mengi mazuri, hasa kwa mchango wake kwa jamii. Mpiganaji wa haki za binadamu na msema kweli.

Profesa Haroub Othman Miraji (68) ni vigumu kwa anayemtambua kuamini kuwa ametutoka, amekwenda kwenye pumziko la milele. Ingawa binadamu hapendi kuamini linapomtokea linalomuhuzunisha, au kwa vile ana tabia ya kupenda kusikia yale yanayompendeza tu, kifo cha Profesa Haroub kilitufanya wengi kutoziruhusu akili zetu kukubali ukweli, lakini bado ukweli unabaki pale pale, kwamba pamoja na kuwa tulimhitaji lakini Mungu alimhitaji zaidi, wakati wake ulifika, aliitwa na akaitika.

Kama mpigania haki mashuhuri wa Afrika Kusini Steven Biko alivyowahi kusema kwamba ‘fikra njema ni ile isiyokufa na ni vema kufa kimwili kuliko kufa kifikra,’ fikra na mawazo ya Profesa Haroub yatadumu milele, ulioondoka kwetu ni mwili tu lakini fikra zake zitabaki kuwa hai kwa wanamapinduzi na wapigania haki za wanyonge.

Profesa Haroub ni alama ya fikra pevu, mahiri na yenye busara. Pamoja na wadhifa aliokuwa nao na heshima katika jamii lakini alikuwa mtu wa watu, tayari kuzungumza na kila aliyemkabili, hakubagua mdogo wala mkubwa, kwake yeye mwenye elimu na asiyekuwa na elimu hakuwa na tofauti katika misingi ya kibinadamu.

Aliamini kwa dhati kwamba binadamu wote ni sawa, hakujikweza wala hakutakabari. Binafsi Profesa Haroub alikuwa ni chanzo changu cha habari (source). Kila ninapotingwa na jambo hasa katika masuala ya siasa, mitafuruku na migogoro yake, Profesa Haroub ndiye aliyekuwa kimbilio langu, simu moja tu ilitosha kupanga naye miadi ya kufanya mahojiano na kama hayupo nchini atakwambia ‘niandikie maswali unitumie mtandaoni.’ Ukimwambia muda wa mwisho wa kuwasilisha, hakikisha kwamba majibu yako utayapata ndani ya muda mulioahidiana. Ukimwambia nitakuja ofisini kwako saa tatu asubuhi, saa tatu kasoro robo yeye atakuwa ameshafika.

Profesa Haroub alikuwa mahiri katika kudadavua suala la kisiasa Zanzibar na pia alikuwa rejea muhimu katika masuala ya katiba na sheria. Bila kigugumizi Profesa Haroub siku moja aliniambia kwamba ‘Katiba ya Tanzania imejaa viraka,’ nami nikaandika hivyo katika makala. Hata hivyo hakuishia hapo ila alivieleza viraka vingi vilivyomo katika katiba na kisha kutoa ushauri. Alisema kwamba kama nguo imejaa viraka kweli yaweza kuvalika? Uking’ang’ania kuivaa bila shaka siku moja itakuadhiri. Akaendelea kusema kwamba nguo yenye viraka vingi inapoteza uhalisia wake, inapoteza taswira yake ya awali, hivyo kama uliupenda mshono wake ni vema ununue kitambaa kingine ushone mpya. Huo ndio mfano unaoakisi katiba ya Tanzania ambayo kimsingi haikidhi haja ya mfumo wa vyama vingi vya siasa kwa sababu yenyewe asili yake ni katiba ya chama kimoja.

Pamoja na kupigania mabadiliko ya katiba, Profesa Haroub alikuwa mstari wa mbele kupigania kuwapo kwa Tume huru za uchaguzi ili kufanyika kwa chaguzi huru na haki hapa Tanzania. Kwa maneno mepesi ni kwamba alikuwa mwanademokrasia mtetezi wa wanyonge na mpiganaji wa haki za binadamu.

Kwa kuwa alikuwa muwazi na msema kweli, wapo viongozi ambao hawakumpenda na wako wengine walimnasibisha na chama cha siasa hasa cha upinzani, lakini kimsingi Profesa Haroub hakujifunga na chama chochote cha siasa na ndiyo maana akawa anaweza kukosoa na kusema kweli. Alichokuwa akikikosoa si chama bali ni mfumo wa siasa uliopo nchini na kwamba mfumo huo kubadilishika kwake ni lazima uanzie katika katiba.

Pamoja na usomi wote aliokuwa nao, Profesa Haroub hakujitenga na watu wa kawaida, alishiriki katika shughuli na hafla mbalimbali alizotaarifiwa. Mimi alinifanya kama mtani wake, alikuwa akiweza kunipigia simu na kunambia; “hivi sasa niko kwenu Pemba, vipi nikuletee mashelisheli?”
Profesa Haroub pamoja na usomi wake, alijichanganya!

Kitu kimoja muhimu nilichokigundua kwake ni kwamba pamoja na kuwa alikuwa tayari kushirikiana na vyombo vya habari kwa wakati wowote ule lakini alikuwa makini. Neno lake kila siku lilikuwa ‘nisikilize kwa makini, usininukuu vibaya.’

Pamoja na kwamba alikuwa na kazi nyingi, midahalo mingi na mihadhara mingi lakini utashangaa jinsi alivyokuwa na shauku ya kusoma. Ofisini kwake hakuingiliki, vitabu kila pembe, vimefurika mpaka vimepitiliza, lakini hakuwa akisahau alipoweka kitabu. Unapokwenda kufanya mahojiano naye na ukawa unataka kumrikodi ni lazima usogeze kidogo vitabu na makabrasha yatakayokuwapo mezani kwake au ukiweke kitonge (tape recorder) chako juu ya vitabu.

Siku moja nilibahatika kufika nyumbani kwake pale Chuo Kikuu, nako mambo hayakuwa tofauti sana na ofisini kwani mashubaka yote yalijaa vitabu, meza za ukumbini nazo zilikuwa na vitabu vilivyofunuliwa kuonyesha kuwa wapo watu waliokuwa wakifanya kazi ya kusoma na kuongeza ujuzi. Kwa bahati nzuri mke aliyemuoa ni sawa na yeye, Profesa Saida Yahya Othman, naye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, hivyo wote walikuwa ni wapenzi wa kusoma, wakawa wamefanana sawasawa kama sahani na kawa.

Kimaumbile Profesa Haroub alikuwa ni mpole lakini makini, hakuwa msemaji ovyo na alikuwa ni msikilizaji mzuri, na hiyo ndiyo sifa ya mtu anayependa kujifunza, hakuwa mtu mwenye dharau hata kidogo, hata kama ulichomuuliza sicho, atakujibu kwa hekima kubwa huku akikuelekeza kilicho ndicho, kwamba ‘tatizo si hilo bali ni kitu fulani na ambacho nadhani kimesababishwa na kitu fulani.’


Mwaka 1992 Profesa Haroub akishirikiana na wenzake, Fatma Maghimbi na Hassan Said walianzisha Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Zanzibar baada ya kuona kwamba jamii ya Kizanzibari inahitaji kufahamu haki zao na kuwa na taasisi ambayo angalau itasimamia kutendeka kwa haki.

Azma ya kituo hicho ambacho hadi umauti ulipomkuta, Profesa Haroub alikuwa mwenyekiti wake, ni kuhakikisha kuwa kila mkazi wa Zanzibar hususan masikini, wanawake, watoto, walemavu na makundi mengine yenye nafasi finyu katika jamii wanaelewa kuhusu haki zao za msingi na wanazifanyia kazi ili kujenga jamii inayofuata misingi ya sheria na inayoongozwa na utawala bora.

Siku moja nilizungumza na Profesa Haroub kuhusu uwepo wa kituo hicho na suala zima la utawala bora Zanzibar naye akasema; “ni vigumu kuwa na utawala bora ikiwa watu wanaoongozwa hawajui hata maana yake, hawaelewi umuhimu wa sheria na kwa ufupi hawajui haki zao. Hivyo dhamira kuu ya kuanzisha kituo hicho ni kuwashajiisha Wazanzibari kujua haki zao kwa kuwapa mafunzo kwa njia tofauti na pia kuwasaidia kutetea haki zao.

Nilipozungumza naye alinambia kuwa kituo hicho kimedhamiria kuinua upeo wa wananchi juu ya masuala ya sheria, haki na wajibu wa mwananchi kwa nchi yake kwa kuendesha semina, warsha, mikutano pamoja na kutoa ushauri wa kisheria.

Profesa Haroub hakuishia hapo bali alieleza pia uzoefu wake kwa watu wenye madaraka na alisema “kuna tabia ya watu hasa wenye mamlaka kuchezea sheria, wanahisi kama kwamba sheria haiwahusu au hata kama inamuhusu anaweza kuipinda, ikiwa watu kama hao wataendelea kupewa mwanya katika jamii, suala la utawala bora litakuwa ni la hadithini tu.

“Haitoshi kutamka kwamba unafuata utawala bora, au hata kuwa na Wizara inayoshughulikia masuala ya utawala bora, halafu wanaovunja haki za binadamu ni maafisa wa vyombo vya dola,” alisema Profesa Haroub.

Hayo ni baadhi tu ya matamshi yaliyotoka kwenye kinywa cha mwanadiplomasia, mwana demokrasia na mpiganaji wa haki za binadamu, Hayati Profesa Haroub Othman. Kifo chake kimeacha pengo kwa Watanzania wote, wanazuoni na wanajamii aliojitolea muda wake na uwezo wake kuwatetea, kuwafumbua macho, kuwazibua masikio na kuwaonyesha njia ya kuelekea kwenye utawala wa sheria na unaoheshimu haki za binadamu. Mchango wake kwa jamii ni mkubwa na bila shaka jitihada zake iko siku zitazaa matunda. Uliokufa ni mwili tu, fikra na mawazo yake bado yataendelea kuwapo. Profesa Haroub aliiaga dunia Juni 28, mjini Zanzibar na kuzikwa Juni 29, 2009.

Labels:

Wednesday, October 15, 2008

 Tumejifunza nini kutokana na uchaguzi mdogo Tarime?

KAMPENI rasmi za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime zilianza Septemba 21. Kampeni hizo zilizofanyika kwa wiki tatu mfululizo hadi kukoma siku moja tu kabla ya uchaguzi uliofanyika Jumapili iliyopita, Oktoba 12 kwa hakika ziliwasimamisha dede Watanzania.

Kila kukicha habari za kutoka Tarime zilipamba vichwa vya habari vya magazeti, nyingi hazikuwa za kufurahisha, zaidi ni vitisho na wasiwasi kwamba Tarime hapatoshi!

Vijembe na kejeli mara hii havikufua dafu kwani vilizidiwa na mapanga na mawe. Wengi walijeruhiwa na wengine kupoteza maisha yao. Kama vile haitoshi hata kiumbe asiyejua kitu kuhusu uchaguzi, mbwa aliyevishwa sare ya CCM, alikatishwa maisha yake kutokana na ushabiki usio wa kistaarabu. Tuliouona Tarime haukuwa ushabiki wa kisiasa bali wa kihuni. Tulisahau kauli mbiu ya kushindana bila kupigana.

Katika hali ya kawaida hiyo haikuwa demokrasia na pengine ni vigumu kuuita uchaguzi ule kuwa ulikuwa huru, pengine ulikuwa wa haki lakini haukuwa wa amani. Yaliyotokea Tarime yanaakisi hali ya kutokuwapo kwa demokrasia halisi Tanzania. Demokrasia yetu bado ni ya ‘magubegube’ (ya kubabaisha). Bado tunadhani kwamba ushindi ni lazima, wanasiasa wanajaribu kila mbinu kuhakikisha ushindi bila ya kuheshimu utashi wa wananchi. Bado wako wanaodhani kwamba wana haki ya kutawala au kuchukua viti vyote vya uwakilishi. Bado demokrasia haijatuingia akilini mwetu kwamba ni uhuru wa kuchagua kiongozi unayemtaka.

Bado tunadhani tunaweza kushinda kwa njia za wizi na ulaghai. Bado tunafikiria kuwa kinachotakiwa ni ‘ushindi wa kishindo’ kumbe vile wananchi wanachotaka ni mwakilishi wao atakayetetea maslahi yao.

Napenda kuungana na wale wenye maoni ya kwamba demokrasia ya vyama vingi kwa Afrika ni demokrasia ngeni, pengine tunahitaji muda zaidi wa kujifunza au pengine si demokrasia stahiki kwa watu wa Bara hili wenye miundo yao ya asili ya utawala.

Inaonyesha kana kwamba demokrasia hii tuliyonayo ni demokrasia ya kupandikizwa na kulazimishwa kwetu, wenyewe hatujawa tayari. Hata hivyo, bado hatujachelewa, kama kweli tunaipenda na tunataka iingie katika mizizi ya mifumo yetu ya uongozi wa umma, basi tuwe tayari kujifunza na katika kujifunza tujitahidi kujiepusha na mabaya, kwa mfano kutumia nguvu wakati wa kampeni na wakati wa uchaguzi, kutumia nguvu za dola za ziada na hata kufanya mbinu za kupata ushindi usio halali. Hayo ni mambo ambayo kama kweli tunayo dhamira ya kufuata mfumo huu wa demokrasia uliopandikizwa kwetu, mambo hayo yamo ndani ya uwezo wetu.

Demokrasia hii tunayoiga haitaki mizengwe, ina misingi yake iliyo bayana, demokrasia hii haihitaji risasi wala mabomu. Lakini ni demokrasia inayopaswa kufuatwa na watu wote katika jamii, wapiga kura, wanasiasa na hata Serikali. Kama tutaizingatia misingi hiyo ya demokrasia ni wazi kwamba tutajiepusha kwa kiasi kikubwa na tafrani zinazotokea wakati wa uchaguzi.

Binafsi nadhani hatuhitaji Jumuiya ya Ulaya ituambie la kufanya, hatuhitaji wakaguzi wa nje waje watwambie kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki. Hatuhitaji kufundishwa hayo, kwani hayo yamo ndani ya uwezo wetu, ni utashi na matakwa yetu na ni ustaarabu tunaoweza kuujenga tukitaka.

Lakini kuna jingine, ambalo pengine ni funzo kwa Chama tawala, kwamba wananchi wanaposema ‘hapana’ maana yake ni ‘hapana.’ Tarime wametupa fundisho, wananchi wa Tarime pengine ukali ni khulka yao, ni watu wasiokubali kunyanyaswa wala kuonewa, ni watu walio tayari kusimamia haki zao hata kama ikibidi wengine kupoteza maisha yao, hiyo ndiyo gharama ya demokrasia, lakini gharama hii ni kubwa mno na ambayo tunapaswa kuhakikisha kwamba hatuingii katika gharama za aina hiyo katika chaguzi zozote zile ziwazo hapa nchini.

Lakini twapaswa kufahamu kwamba Watanzania kuna kitu wamejifunza kutoka Tarime na kama wataamua kutumia mbinu kama za wakazi wa Tarime katika kuhakikisha kwamba wanalinda haki yao ya kuchagua, basi bila shaka Tanzania patakuwa hapakaliki, patachimbika bila jembe!

Watawala na viongozi wa vyama vya siasa wanapaswa waheshimu matakwa ya wananchi na wawape uhuru wao wa kuchagua. Hakuna ubishi kwamba kila anayeingia katika ushindani anaingia kwa dhamira ya kushinda, lakini kushinda huko hakupaswa kuwe ‘kwa kucha na meno!’ Mwageni sera zenu wananchi watazisikia. Kwanini hatuchukui mfano wa biashara? Wafanyabiashara kama 10 wanakuwa wamejipanga katika mstari mmoja na pengine wote wanauza bidhaa za aina moja, lakini wakati huo huo wanaheshimu utashi wa wateja wao. Mteja anaweza kumruka mfanyabiashara wa kwanza na akaenda kwa mfanyabiashara wa katikati au wa mwisho. Na hiyo ndiyo dhana ya biashara huria na pia inapaswa iwe dhana ya siasa huria.

Lakini pia kama ambavyo kwenye biashara zipo za ‘kimachinga’ ambazo mmachinga utakapomuuliza bei ya kitu ni lazima ukinunue, usipokinunua utavurumishiwa gunia la matusi mpaka utamani ardhi ipasuke ujifukie. Na siasa nazo ziko za namna hiyo pia, zile za Tarime ukiwa ni mfano mmoja wapo.

Tunakumbuka jinsi Mwenyekiti wa DP, mchungaji Christopher Mtikila alivyovurumishiwa mawe, kisa eti alitamka yasiyowaridhi wana-Tarime. Hizo ni siasa za ‘kimachinga’ lazima ukubaliane na wanayoyataka wachuuzi. Lakini hiyo ni ilani iliyo kiambazani inapaswa kuzingatiwa, tayari moshi umeshaanza kufuka, tutahadhari nyika zisishike moto!

0754 849694
hshamte@mwananchi.co.tz

Thursday, July 31, 2008

 Mfumo wa uongozi na demokrasia Afrika, ni mkorogovyogo!

Na Hawra Shamte

UKIANGALIA mlolongo wa matukio, visa na mikasa ya viongozi wa Bara la Afrika, moja kwa moja utabaini kuwa mengi wafanyayo ni yale yaliyoainishwa katika falsafa za Niccolo Machiaveli, mwanafalsafa wa karne ya 15 aliyezaliwa Roma Italia.
Katika masuala ya uongozi wa umma, Machiaveli aliweka mkazo kwa kiongozi kung’ang’ania kuendelea kubaki madarakani, alisisitiza kwamba ‘ufalme’ au uongozi ni lazima ulindwe kwa nguvu zote, hata ikibidi kutumia jeshi ama kuua.
Kama ni utashi wao, viongozi wengi hasa wa Bara la Afrika wangependa waendelee kukaa madarakani daima dawama, kwao wao ukishakamata madaraka ni sawa na pingu za maisha, hadi ufe uzikwe.
Mifano tunayo mingi, Wapo akina Yoweri Museveni, Robert Mugabe, Omar Al Bashir, Husni Mubarak na wengineo. Sidhani kwamba ni lazima wajitangaze kuwa ni maraisi wa maisha, bali vitendo vyao vinatosha kuthibitisha hayo. Je, demokrasia ya uchaguzi na kupishana madarakani inatumikaje Afrika?
Pengine demokrasia ya aina hiyo si demokrasia ya waafrika, uongozi wa jadi ungetosha kujenga misingi ya uongozi na demokrasia, kwani hivyo ndivyo inavyoonyesha kihalisia. Kila anayeshika madaraka ikiwa atalazimika kuondoka madarakani ataweka mazingira ambayo kama ataondoka basi nafasi yake ishikwe na angalau na mtoto wake, mifano ya hao tunayo mengi.
Tumeshuhudia katika nchi nyingi za Kiafrika viongozi wakiwa wanabadilisha katiba, za nchi ilimradi tu waendelee kubaki madarakani, hata kama wananchi wameshawachoka. Mara ngapi tunasikia kwamba Rais fulani anataka kufanya mabadiliko ya katiba ili kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani.
Ziko katiba zinazoweka vipindi vya urais, kwa mfano Tanzania kipindi cha Rais kukaa madarakani ni miaka mitano mara mbili, hii ina maana ya kwamba baada ya miaka kumi hata kama rais huyo anapendwa vipi ni lazima akabidhi uongozi kwa mwingine.
Uamuzi wa aina hiyo una faida zake na hasara zake, faida ni kwamba unaepusha kujenga himaya ya kifalme na kidikteta. Hasara yake ni kwamba mara nyingine inashindikana kumaliza ajenda na miradi ambayo Rais amejiwekea kwani miaka 10 si mingi na sera nyingi ni za muda mrefu.
Yawezekana mtu akajenga hoja kwamba uongozi ni mchakato, hivyo wengine watakaokuja badala ya aliyeondoka watauendeleza mchakato huo. Hiyo ni kweli na ndivyo inavyopaswa iwe, lakini si lazima kwa kiongozi mpya kuendeleza sera na mikakati iliyowekwa na uongozi uliokuwapo madarakani. Rais mpya ana uamuzi wa kupanga mipango na mikakati mipya endapo ataona kwamba iliyopo itamkwaza.
Kubadilika katiba kwa nchi za Afrika ni jambo la kawaida, kwani imeshatokea mara nyingi kwa baadhi ya nchi, rais wake kubadili katiba ilimradi tu abaki kuendelea madarakani.
Kwa mujibu wa Machiaveli, kiongozi ana haki na wajibu wa kuhakikisha kwamba anaendelea kulinda madaraka yake hata ukifika muda wa kustaafu anayo haki ya kuongeza muda, kwani kutafuta kiongozi mwingine ni kazi kubwa sana.
Pengine Machiaveli alikuwa akizungumzia ufalme zaidi kuliko uongozi ambao msingi wake ni mkuonyesha njia na endapo kiongozi akishindwa kuonyesha njia anapaswa awapishe wengine nao wajaribu kuonyesha njia.
Lakini kwa mantiki ya Machiaveli, ni lazima uongozi uwe endelevu. Endelevu aliyoiainisha ni ya kung’ang’ania madaraka, kwake yeye, uongozi ni mali ya mtu, pengine amepewa na Mungu hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kumnyang’anya aliyepewa na Mungu.
Ipo dhana nyingine ya uongozi endelevu kwa mantiki ya ‘maliberali’ na siyo ya ‘marialisti.’ Katika falsafa za kiliberali uongozi ni mali ya umma si mali ya mtu na ni lazima uwe endelevu, yaani viongozi waliopo madarakani wanapaswa kutengeneza mfumo wa kupasiana kijiti, yaani wewe ongoza kwa miaka nane mathalan, wakati ukiwa madarakani hakikisha kwamba anapatikana mtu mwingine wa kushika pale utakapoachia na pengine kuendeleza yale uliyoyapanga na kukusudia kuyafanya lakini ukashindwa pengine kutokana na muda, na hili linafanyika duniani kote.
Lakini lipo jingine linalotia mashaka katika uongozi wa Afrika; hivi karibuni Rais wa Rwanda, Paul Kagame alipitisha sheria ya kinga ya Rais atakayeondoka madarakani kutoshtakiwa kwa kosa lolote lile alilolitenda wakati akiwa Rais. Hii ni ngumu kwa sababu kinga hiyo yaweza kutumika vibaya, Rais aweza kuua, kuiba/kuhamisha na hata kuangamiza kwa kujiamini kwamba hakuna chochote kitakachomkuta. Mfumo huu ni wa Alfa na Omega, kwamba Rais ndiyo mwisho. Dhana hii inapingana na ile dhana ya kwamba hakuna aliye juu ya sheria. Kagame hivi sasa yuko juu ya sheria, yeye ndiye mwanzo na ndiye mwisho!
Binafsi naungana na wale wanaofikiri kwamba kuna haja ya kubadilisha mfumo wa uongozi wa Afrika, kwani uliopo hivi sasa ni ‘mkorogovyogo’!

Hawra Shamte ni Mhariri wa Siasa wa gazeti la Mwananchi.
hshamte@mwananchi.co.tz
0754 849694

 Prof. Masha:Watanzania walijibu swali lisilo kuhusu Shirikisho

Na Hawra Shamte

MBUNGE wa Bunge la Afrika Mashariki, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha United Democratic na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha St. Augustine, Profesa Fortunatus Lwanyantika Masha anasema kwamba kwa bahati mbaya au kwa kutokutambua, Kamati iliyoongozwa na Profesa Samuel Wangwe haikuweza kuwaelekeza Watanzania swali halisi walilopaswa kulijibu ambalo ni je, tuharakishe Shirikisho la Afrika Mashariki? Badala yake, wananchi wakajibu swali la je, mnataka Shirikisho?

Akizungumza katika mjadala wa wazi katika Chuo Kikuu cha St. Augustine, tawi la Dar es Salaam, Prof. Masha alisema kamati ya Wangwe iliibua maoni na hisia nyingi kuhusu kazi ya kamati yenyewe; uamuzi wa kuundwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki; na wasiwasi wa kuunda Shirikisho la nchi zinazotofautiana kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiusalama.

Profesa Masha anasema pengine mkanganyiko kuhusu Shirikisho unatokana na kuwapo kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo ili kulitambua Shrikisho la Afrika Mashariki ni muhimu kutofautisha baina ya Shirikisho na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Watu wengi hawaoni tofauti baina ya jumuiya hizo mbili, na ndiyo maana kushindwa kwa EAC kunaunganishwa moja kwa moja na Shirikisho kwamba nalo laweza kushindwa kama ilivyoshindwa Jumuiya. Wasichokifahamu wengi ni kwamba malengo na utashi wa kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki ni tofauti na yale yaliyokuwapo wakati wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika mwaka 1977,” anasema Prof. Masha.

Prof. Masha anaendelea kueleza kuwa ingawa hivi sasa ipo Jumuiya ya Afrika Mashariki na ambayo kimfumo inaweza kuwa na Umoja wa Forodha, Soko Moja na Sarafu Moja bila ya kuwa na Shirikisho la kisiasa.

“Dhamira ya kuwa na Shirikisho ni kuunda Taifa Moja la watu wa Afrika Mashariki.”

Prof. Masha anasema katika utangulizi wa Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, inaelezwa wazi kwamba: “Nchi za Tanzania, Kenya na Uganda zimedhamiria kuimarisha mahusiano yao ya uchumi, kijamii, kiutamaduni, kisiasa, kiteknolojia na mengine, kwa maendeleo ya haraka kwa nchi zote, kwa kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki; pamoja na umoja wa forodha na soko moja, baadaye sarafu moja na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.”

Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulishawasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na likauridhia mwaka 2000. “Kwa maana nyingine ni kwamba; Bunge la Tanzania pamoja na Serikali ya Tanzania wameisharidhia kuundwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki. Kinachobakia ni mchakato wa kulifikia Shirikisho,” anaeleza Prof. Masha.

Agosti 28, 2004, wakuu wa Nchi wanachama wa EAC (Summit) waliunda kamati ya kuangalia namna ya kuharakisha mchakato wa Shirikisho ili kutimiza kwa haraka kusudio la Shirikisho la Kisiasa. Ndipo ilipoanzishwa Kamati ya Amos Wako ambayo ripoti yake ilisema kwamba kimsingi kuundwa kwa Shirikisho la Kisiasa kumekwisha anza kwani tayari miundombinu yake imeshawekwa; kuna Mahakama ya Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki pamoja na maelewano ya mahusiano katika mambo ya majeshi, usalama na sera za nchi za nje.

Ripoti ya Wako iliweza kuainisha majukumu sita ya Shirikisho ambayo ni Ulinzi na Usalama, mambo ya Nchi za Nje, Mamlaka ya Ziwa Viktoria, Haki, Polisi na Uhamiaji, fedha na Mipango na Miundombinu.

“Ingawa wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hawakuazimia moja kwa moja kukubaliana na mapendekezo ya kamati ya Wako, kwa matamshi yao walifurahishwa na kazi ya Kamati hiyo. Kwa kuwa mengi ya yaliyomo katika mikakati ya maendeleo (EAC Development Strategy 2006 – 2010) yanatokana na mapendekezo ya kamati ya Wako; kimsingi walikubaliana na programu ya kufikia Shirikisho kama ilivyopendekezwa na Kamati ya wako.”
Utata wa kazi ya kamati ya Wangwe
Kamati ya Wangwe ilihusika na mchakato wa Mashauriano ya Kitaifa (National Consultative Process) kuhusu kuharakisha Shirikisho la Kisiasa. Profesa Masha anasema nia ya kushirikisha wananchi wa Afrika Mashariki katika mchakato wa kuunda Shirikisho ni nzuri, ugumu ni namna ya kuwashirikisha na hasa baada ya maamuzi ya msingi yakiwa tayari yameisha chukuliwa. Ni taratibu zipi zitumike katika kuwashirikisha? Washirikishwe au waamue?

Prof. masha anasema pamoja na kuwa Kamati ya Wangwe ilikuwa inaratibu/inatafuta maoni ya wananchi kuhusu swali “je, Shiriksho liharakishwe au hapana?” lakini ilikuwa na utata wa aina mbili: Kwanza; mkanganyiko wa swali lililotakiwa kujibiwa. Pili; namna ya kupata maoni ambayo yanafanana na maoni ya Watanzania kwa ujumla. Yote mawili yalikuwa matatizo ya kiufundi.

Waliohudhuria mikutano ya Kamati ya Wangwe na wengi waliotoa maoni katika vyombo vya habari, walijibu swali tofauti, yaani: Je, tuingie katika Shirikisho au hapana? Kwanini?

“Tofauti hii kubwa kati ya swali lililoulizwa na swali lililojibiwa, ilileta mkanganyiko mkubwa, Waliokuwa wanaelewa vema Kazi ya kamati hiyo, waliliona zoezi lililoendeshwa na Kamati ya wangwe halikuwa na maana,”
Prof. Masha anasema.
Prof. Masha pia anabainisha tatizo jingine kubwa katika zoezi la Kamati ya Wangwe, kwamba lilikuwa namna walivyoratibu maoni ya wananchi. “Kwa mfano; walikwenda katika Wilaya yenye watu zaidi ya 300,000; wakapata ukumbi katika makao makuu ya Wilaya; wakafanya mkutano mmoja au miwili na kupata jumla ya watu 200. Maoni ya hawa 200 yana uhalali gani kuchukiliwa kwamba ni maoni ya wilaya nzima? Hawa 200 wamepatikanaje hata waweze kusemea Wilaya nzima? Anahoji Prof. Masha.

Hata hivyo, Prof. Masha anakiri kwamba jambo zuri lililotokana na mizunguko ya Kamati ya Wangwe ni kutoa mjadala katika taifa, uliosisimua kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki hata kama wanaanchi walijibu swali lisilo.

Mwisho Prof. Masha anatoa usahuri kuwa suala la Shirikisho ni suala la kisiasa, lenye kuhitaji maamuzi ya kisiasa. Wanasiasa hawawezi kukwepa wajibu wao wa kaumua mambo neyti kama Shirikisho, kwa kujificha nyuma ya kamati ambazo zina utata.

Mwisho.

Thursday, May 01, 2008

 Haya ni mapambano ambayo wapenda demokrasia na amani lazima washinde!

Salaam
Makala hii ilitoka katika gazeti la Mwananchi la April 16, nimeona niiweke mtandaoni tufaidike wengi.

Kufuatia makubaliano ya mwafaka wa kisiasa Zanzibar kugota, baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kuagiza kwamba suala la kuwapo kwa serikali shirikishi Zanzibar lirudishwe kwa wananchi kwa kupigiwa kura ya maoni, wachambuzi wa masuala ya kisiasa nchini wanaona kwamba, uamuzi huo unaweza kuzidisha utata wa kisiasa Zanzibar. Katika makala hii, mwandishi HAWRA SHAMTE anazungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa na haki za binadamu ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa HAROUB OTHMAN ambaye pamoja na mambo mengine anashauri kuwa viongozi wanapaswa kuhakikisha kwamba ufumbuzi wa tatizo la kisiasa Zanzibar unapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010…

Swali: Je, uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM kulirudisha suala la ‘Mwafaka’ kwa wananchi hasa kipengele cha serikali ya mseto, wewe unauonaje? Je, unaweza kuleta suluhisho la mgogoro?

JIBU: Ni jambo la busara kwa serikali kutaka wananchi wake watoe maoni/mapendekezo juu ya mambo yoyote makubwa au madogo inayotaka kufanya. Kuna nchi kama Switzerland ambapo serikali zake za mikoa (cantons) huitisha kura za maoni hata katika mambo madogo madogo. Huo ndio utamaduni waliokua nao. Sisi hapa hatuna utamaduni huo.
Kuna mambo mazito yamefanyika nchini bila ya kura ya maoni. Mifano ni kama Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964; kuletwa mfumo wa chama kimoja mwaka 1965; Azimio la Arusha la mwaka 1967 na sheria zilizofuatia za kutaifisha mali; kuja kwa mfumo wa vyama vingi wa 1992, na kadhalika.
Ingekuwa kumepigwa kura ya maoni mwaka 1991 na wananchi asilimia 80 wakakataa mfumo wa vyama vingi, kama vile takwimu za Tume ya Nyalali zinavyoonyesha, kwa matokeo hayo si tungekataa mfumo wa vyama vingi? Athari zake tunazijuwa? Suala gani wataulizwa wananchi katika kura hiyo ya maoni; ikiwa wanataka au hawataki serikali ya mseto. Mimi nafikiri kwamba ‘Kamati ya Mwafaka’, baada ya kutafakari matatizo yote yaliyojitokeza tangu uchaguzi wa 1995, na zile chaguzi za 2000 na 2005, wakaonelea kwamba njia ya busara ni kuwa na serikali ya mseto.
Kama alivyosema Rais Jakaya Kikwete na Profesa Ibrahim Lipumba, kila upande katika kamati hiyo imekuwa ikishauriana na wakuu wake. Hii ni kusema kwamba Rais Kikwete, Rais Amani Karume na Profesa Lipumba wote walijua nini kimezungumzwa katika kamati hiyo na nini kimekubaliwa.
NEC ya CCM na Baraza Kuu la CUF vyote vilikuwa vikiarifiwa nini kinatokea. Mbona wakati wote huo wazo la kura ya maoni halikuletwa? Na baada ya Rais Karume kulileta suala hilo kwa Komredi Kingunge Ngombale Mwiru, Luteni Yusuf Makamba na Ali Ameir Mohamed, ambao ni wajumbe wa ‘Kamati ya Mwafaka’, si wangerejea kwa wenzao wa upande wa CUF kuwasikiliza wana maoni gani, kabla ya jambo hilo kupelekwa kwenye Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM?
Tafsiri iliyojitokeza sasa hivi ni kwamba CCM haitaki hata hiyo dhana ya serikali ya mseto, na kusema kuwe na kura ya maoni ni njia tu ya kistaarabu ya kukataa jambo hilo. Kwani hata utekelezaji wake ambao unataka mabadiliko ya kikatiba, kuandaa daftari la wapiga kura na uendeshwaji wa hiyo kura ya maoni sioni vipi itawezekana kufanyika na halafu tuwe na uchaguzi wa mwaka 2010. Mimi sioni kwamba kutakuwa na kura ya maoni na wala kama kweli kutakuwa na jitihada za dhati za kuiangalia upya Katiba ya Zanzibar na kubadilisha sheria ya uchaguzi na kuifuma upya Tume ya Uchaguzi ili kuhakikisha kwamba kutakuwa kweli na uchaguzi huru na wa haki. Na ikiwa hayo hayakufanyika haraka, basi itakuwa tunaelekea pabaya huku tukijua na tukiwa macho wazi!

1. Je, unadhani CCM inayo dhamira ya kweli ya kuleta maelewano ya kisiasa Zanzibar?

JIBU: Tunachoweza kusema juu ya CCM ni kutokana na dhamira zake za dhahiri, katiba yake na yale ambayo viongozi wake wanayazungumza hadharani. Na ikiwa chama hicho kinataka kubaki madarakani, Bara na Visiwani, na kuendelea kupata uhalali wa kuwa chama cha siasa, basi lazima kiende na wakati na kijifunze kutokana na historia ya nchi yetu lakini pia tujifunze kutokana na yanayotokea kwa wenzetu. Mizozo, uhasama, chuki, malumbano yasiyo na mwisho, uvunjwaji wa haki za binadamu, n.k., sio vitu vinavyowaunganisha watu bali vinaigawa jamii. Na jamii iliyogawanyika haipati maendeleo. La umuhimu pia ni urithi gani ambao Rais Jakaya Kikwete na Rais Amani Karume wanataka kuwaachia Watanzania baada ya uongozi wao?

2. Wachambuzi wanasema kuwa wahafidhina wa siasa za Zanzibar wanaogopeshwa na kipengele cha mgawanyiko wa madaraka. Je, hofu yao ina mashiko?

JIBU: Kwa jinsi maelezo yanavyoonyesha juu ya nini kimetokea katika Kamati Kuu na NEC ya CCM, sio suala la wahafidhina au wapenda maendeleo kushinda, lakini ni ukosefu wa uongozi. Inaonyesha katika suala hili Kamati Kuu haikwenda kwenye NEC na msimamo mmoja na kujua nini wanataka. Wachunguzi wengi wanasema kuwa mgawanyiko uliotokea haukupata kuonekana tangu mkutano mkuu wa TANU wa mwaka 1958 kule Tabora kuhusu kura tatu. Uongozi ni kuonyesha njia; na ili kufanya hivyo uongozi lazima uwe unajua wapi unataka kuwapeleka watu na kuamini kwamba utaweza kuwafikisha huko.

3. Kwa maoni yako, unadhani nini kingeanza, kura ya maoni au mazungumzo? Na je, kwani makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo hayawezi kupewa uhalali wa kisheria mpaka wananchi washiriki katika kura za maoni?

JIBU: Ninavyofahamu mimi ni kwamba ile Rasimu iliyotolewa na “Kamati ya Mwafaka’ na kupelekwa kwenye vyombo vya juu vya CUF na CCM ilimaanisha kwamba mazungumzo yamemalizika na kilichohitajika ni ridhaa ya vyombo hivyo na utekelezwaji wa mapendekezo hayo. Utekelezwaji ungeweza kufanyika kwa kulitumia Baraza la Wawakilishi, na hata pale ambapo ridhaa ya thuluthi mbili ya wajumbe ingehitajika, hilo lisingekuwa gumu kwa vile jambo hilo litakuwa limekubaliwa na vyama vyote viwili.

4. Hoja nyingine inayotolewa na wanasiasa wa vyama vingine (visivyo CUF na CCM) ni kuwa mazungumzo yangeshirikisha vyama vyote vya siasa na wala si CUF na CCM pekee, wewe unaonaje hoja hiyo?

JIBU: Ni hoja sahihi kabisa. Na si vyama vya kisiasa, bali pia asasi zisizokuwa za kiserikali, jumuiya za kidini, vyama vya kitaalamu, watu mashuhuri katika jamii, n.k. Kwani kinachotafutwa ni mustakabali wa taifa zima na kila mmoja ni mdau katika hilo. Lakini hili lingekuja katika awamu ya pili. Kuna mambo yaliyokubaliwa katika Mwafaka I na II ambayo hayakutekelezwa; kuna yale yaliyojitokeza katika uchaguzi wa mwaka 2005 ambapo ilipelekea CUF kusema hawamtambui Rais Amani Karume, na mengineyo. Sasa haya ni ya CUF na CCM. Matumaini yangu mimi ni kwamba ikiwa mwafaka utafikiwa, utatoa fursa ya kuwa na mjadala mpana zaidi na wa kitaifa kuhusu mustakabali wa taifa; na hapo kila chama, jumuiya, taaluma, n.k., ingebidi vishirikishwe.

5. Je, uamuzi wa CUF kujitowa katika mazungumzo ya Mwafaka ni sahihi?

JIBU: Bila ya shaka CUF ina sababu zake za kufanya hivyo. Rasimu ile iliyokubaliwa na Kamati ya Mwafaka imejengeka kwenye msingi kwamba kurekebishwa kwa katiba, kufumwa upya kwa Tume ya Uchaguzi, kufanyiwa marekebisho ya sheria ya uchaguzi na kutengeneza mazingira ya kuwapo kwa uchaguzi wa haki na huru, vitafanyika kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010; na chombo kitakachosimamia haya ni serikali ya mseto. Sasa kwa CCM kuleta jambo jipya la kura ya maoni na kutamka wazi kwamba kwa maoni yake serikali ya mseto itakuja baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 imekuwa kwamba ule msingi wa makubaliano yale haupo tena.

6. Pamoja na kususia mazungumzo, unadhani CUF inaweza kuchukuwa hatua gani zaidi katika kukabiliana na usanii wa kisiasa wa CCM?

JIBU: Huu sio usanii, ni mbinu za kisiasa. Utakumbuka katika taarifa iliyotolewa na Makamba, Ngombale na Ali Ameir kwenye Kamati Kuu ya CCM walizungumzia kwamba kuleta kura ya maoni ni njia ya ‘kuipiku’ CUF! Kutopatikana kwa suluhisho la kudumu sio kwamba inaiumiza Zanzibar tu lakini athari zake zinafika Bara pia. Tumeona vipi tatizo hili la Zanzibar lilivyochukuwa mjadala mkubwa na mrefu kwenye vikao vya CCM huko Butiama. Ikiwa tutafikia uchaguzi wa mwaka 2010 bila ya tatizo hili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu, nachelea kufikiri nini kitatokea. Hiki si kitisho bali ni baada ya kuangalia nini kinatokea nchini na kuona pia vipi mambo yanavyokwenda ulimwenguni.

8. Maalim Seif aliripotiwa kuwa alikwenda Uingereza na nchi za Scandinavia kuwashawishi waingilie kati suala la Mwafaka. Je, hatua hiyo aliyoichukuwa ni sahihi? Kama ni sahihi, je unadhani nchi hizo wahisani zinaweza kufanya nini katika kufikia hatima ya mgogoro wa kisiasa Zanzibar?

JIBU: Sijui Maalim Seif alikwenda wapi na kufanya nini. Lakini ninachojua ni kwamba jumuiya ya mabalozi wa kigeni hapa nchini imekuwa ikifuatilia kwa karibu mazungumzo yaliyokuwa yakifanyika baina ya CCM na CUF, na wengi wao wamesikitishwa na yaliyotokea. Nini watashauri serikali zao sijui, lakini matamshi aliyotoa Balozi wa Marekani hivi karibuni yanaashiria kwamba mambo hayatokuwa shwari si kwa Zanzibar tu bali kwa Tanzania kwa ujumla. Seif Shariff kokote atakakokwenda atasikilizwa lakini sidhani kwamba siasa za nchi hizo kwa Tanzania zitategemea nini Seif anataka bali hali halisi ilivyo nchini na maslahi ya nchi hizo.

9. Unazitathmini vipi jitihada za Rais Jakaya Kikwete katika kuondosha mpasuko wa kisiasa Zanzibar?

JIBU: Rais Jakaya Kikwete alitamka azma yake ya kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar alipohutubia Bunge kwa mara ya kwanza kama Rais mwezi Desemba 2005. Viongozi wengi wa kiafrika hawana utamaduni wa kujali vipi historia itawasema na kuwahukumu katika kipindi cha utawala wao au wanataka kuwacha urithi upi ambao ukumbukwe wa utawala wao. Kuweza kulitanzuwa tatizo hili la Zanzibar sio tu kutampa Rais Kikwete na Rais Karume heshima zaidi nchini na kimataifa lakini pia itakuwa wamewacha urithi mzuri.

10. Nini maoni yako kuhusu hisia za Wapemba kwamba wanataka waachiwe kisiwa chao na waunde serikali yao?

JIBU: Kwa upande mmoja naweza kufahamu kwanini hisia kama hizo zinaibuka sasa, lakini kwa kweli ni mawazo ya hatari kwa taifa letu. Ni kitu ambacho Mwalimu Nyerere alituonya kabla. Leo Wapemba wanaweza kujiona kuwa ni kitu kimoja dhidi ya Waunguja, lakini kesho itakuwa ni wale kutoka Ziwani, Kengeja, Wete au Kisiwa Panzi. Hoja sio kujitenga bali kujitahidi kujenga demokrasia ya kweli ambapo kila mmoja atakuwa na hisa katika upanuwaji wake, kuenziwa kwake na kudumishwa kwake. Haya ni mapambano ambayo wapenda demokrasia na amani lazima washinde!

KUHUSU MIMI

JINA:Hawra Shamte
MAKAZI:Dar es salaam
NCHI:Tanzania
KAZI:Mwandishi

KUELEKEA BUNGE LA BAJETI 2006

QuickTopic free message boards
Bonyeza hapa ili uweze kuelezea: NINI MTAZAMO WAKO JUU YA BAJETI IJAYO YA MWAKA 2006/07 NCHINI TANZANIA?

VYOMBO VYA HABARI MTANDAONI

  • The Citizen
  • Mwananchi
  • Mwanaspoti
  • Business Times
  • Majira
  • Daily News
  • Nipashe
  • The Guardian
  • The Express
  • Kiongozi
  • Uhuru/Mzalendo
  • Arusha Times
  • BLOGI ZA KISWAHILI

  • Bangaiza
  • Mwandani
  • Pambazuko
  • Damija
  • Mtafiti
  • Martha
  • Gaphiz
  • Swahili time
  • Miruko
  • Dira yangu
  • Msangimdogo
  • Jeff Msangi
  • Kasri la mwanazuoni
  • Kurunzi
  • Baragumu
  • Mawazohuru
  • Fikra Thabiti
  • Mtandaoni
  • Motowaka
  • Mkwinda
  • Ngurumo
  • Nyembo
  • Bwaya
  • Omega
  • Tafakari za Maisha
  • Nuru akilini
  • Mtandawazi
  • Mhujumu
  • Vijimamboz
  • Wakati wa Ukombozi
  • Kijiwe Joto
  • Watoto Wetu
  • Jungu kuu
  • Kisima cha Weledi
  • Jarida la Ughaibuni
  • Bhalezee
  • Sauti ya Baragumu
  • Kona yangu
  • Furahia Maisha
  • Bakanja
  • Terrie Swai
  • Fatma Karama
  • Kazonta
  • Binti Afrika
  • Blogu ya Kilimo
  • Ukombozi
  • Mwafrika
  • Digital Africa
  • Blogu ya lugha mseto
  • BLOGI ZA WAAFRIKA

  • BLOGAFRICA
  • BLOGU ZA WAAFRIKA
  • DIGITAL AFRICA
  • MAMA JUNKYARD'S
  • MSHAIRI
  • KENYAN PUNDIT
  • MONGI DREAMS
  • ISARIA MWENDE
  • CUNNING LINGUISTICA
  • ETHIOPUNDIT
  • MOCHALICIOUS
  • UNGANISHA
  • DEMOKRASIA KENYA
  • CHANUKA
  • BANKELE
  • MAARIFA/AKIEY
  • AFROMUSING
  • NEHANDA DREAMS
  • BLACK LOOKS
  • YUMMY WAKAME
  • AFRICAN OIL POLITICS
  • NUBIAN SOUL
  • SANAA
  • VIRTUAL INSANITY
  • MENTAL ACROBATICS
  • KENYA UNLIMITED
  • JIKUMBUSHE KAZI ZANGU ZA ZAMANI

    April 2006 May 2006 June 2006 October 2007 November 2007 December 2007 May 2008 July 2008 October 2008 July 2009 August 2012 October 2012

    Imetengenezwa na

    Ukibofya hapa utapelekwa katika Blogi ya msangimdogo

    na inawezeshwa na